RUNALI YATATUA CHANGAMOTO YA MAJI KITUO CHA AFYA MARAMBO

December 31, 2025

 

Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa Hassan Ngoma aliyemwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea katika hafla ya kukabidhi kisima cha maji kilichojengwa na RUNALI katika kituo cha afya Marambo kwa uongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Nachingwea Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa Hassan Ngoma aliyemwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea katika hafla ya kukabidhi kisima cha maji kilichojengwa na RUNALI katika kituo cha afya Marambo kwa uongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Nachingwea Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa Hassan Ngoma aliyemwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea akifungua maji wakati hafla ya kukabidhi kisima cha maji kilichojengwa na RUNALI katika kituo cha afya Marambo kwa uongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Nachingwea 


Na Fredy Mgunda, Nachingwea 

Chama Kikuu cha Ushirika RUNALI kimetatua changamoto ya upatikanaji wa maji katika Kituo cha Afya Marambo, changamoto iliyodumu kwa miaka mingi na kusababisha baadhi ya huduma kushindwa kutolewa ipasavyo katika kituo hicho.


Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kisima hicho cha maji, Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Ushirika RUNALI, Odas Mpunga, alisema kuwa lengo kuu la mradi huo ni kusogeza huduma muhimu kwa jamii inayohudumiwa na Kituo cha Afya Marambo.


Mpunga alisema chama hicho kilipokea maombi ya kusaidia kutatua changamoto ya maji katika kituo hicho cha afya, hali iliyopelekea RUNALI kuchukua jukumu hilo kwa dhamira ya kuisaidia jamii.


Aliongeza kuwa kisima hicho kimekamilika na kuanza kutoa huduma, hivyo ni jukumu la wananchi pamoja na viongozi wa eneo hilo kuhakikisha wanakitunza ili kiwe mradi endelevu wenye manufaa ya muda mrefu.


Kwa upande wake, Meneja wa RUNALI, Jahida Hassan, alisema kuwa utekelezaji wa mradi huo ni sehemu ya kutimiza msingi wa saba (7) wa vyama vya ushirika, unaohimiza vyama hivyo kurudisha mchango kwa jamii inayowazunguka.


Jahida aliongeza kuwa kisima hicho ni kirefu na kina maji ya kutosha, hivyo kinapaswa kutumika kwa malengo yaliyokusudiwa, hususan kuhudumia Kituo cha Afya Marambo.


Alisema kuwa RUNALI imetumia zaidi ya shilingi milioni 15 kuchimba kisima hicho hadi kukamilika kwake na kuanza kutoa huduma za maji katika kituo hicho cha afya.


Naye mgeni rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa, akimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea, Hassan Ngoma, aliwataka wananchi na viongozi wa eneo hilo kuhakikisha wanauhudumia na kuutunza mradi huo ili uwe na manufaa ya kudumu kwa jamii na serikali kwa ujumla.


Ngoma alisema kuwa fedha nyingi zimewekezwa katika mradi huo wa kisima cha maji kwa lengo la kutatua kero ya maji kwa wagonjwa, wahudumu wa afya pamoja na wananchi wanaohudumiwa na kituo hicho, hivyo ni muhimu kulinda na kuutunza uwekezaji huo.


Aidha, aliwahimiza wananchi na wakulima ambao bado hawajajiunga na vyama vya ushirika kufanya hivyo kwa ajili ya maendeleo yao binafsi na maendeleo ya taifa kwa ujumla.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »