HANDENI, TANGA
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha National League for Democracy (NLD), Mhe. Doyo Hassan Doyo, amepokelewa kwa heshima ya kipekee na kufanyiwa dua maalum na wazee wa Kijiji cha Misima, Wilaya ya Handeni, mkoani Tanga.
Wazee wa kijiji hicho walijitokeza kwa wingi kumpokea Mhe. Doyo na kumfanyia dua za kumtakia kheri, baraka, na mafanikio katika safari yake ya kisiasa ya kuwania nafasi ya juu kabisa ya uongozi wa taifa.
Akizungumza kwa niaba ya wazee wa Misima, mmoja wa viongozi wa kidini alisema, “Misima ni sehemu yenye historia kubwa ya mapambano ya ukombozi wa taifa hili. Tunamwona Mhe. Doyo kama kijana aliyepita katika nyayo zile zile za wazee wake waliopigania uhuru. Uthubutu wake ni wa kipekee na utakumbukwa na vizazi vijavyo hapa Misima.”
Kwa upande wake, Mhe. Doyo aliwashukuru wazee hao kwa mapokezi yao yenye heshima na maombi yao ya baraka.
EmoticonEmoticon