
Diwani wa kata ya Mzizima, Chiluba Fredrick akiwa kwenye ofisi za kata hiyo tayari kuchukua fomu, wa pili kulia kwake ni katibu wa kata hiyo Amiri Mligu.
Na Hamida Kamchalla, TANGA.
ALIYEKUWA Diwani wa Kata ya Mzizima kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Chiluba Fredrick amechukua fomu ya kuwania nafasi hiyo tena huku akiomba ushirikiano kwa wananchi na wanachama wote kwa ujumla kuhakikisha wanakipa chama hicho ushindi wa kishindo katika uchaguzi mkuu mwaka huu.
Chiluba ameyadema hayo wakati alipochukua fomu ya iuwania nafasi hiyo baada ya kupitia kwenye kura za maoni ambapo pia amewashukuru wananchi pamoja na wajumbe kwa kukuamini na kumpa nafasi hiyo.
"Nashukuru sana wana chama wa chama cha mapinduzi kwa kuendelea kuniamini na kunipa ridhaa tena ya kupeperusha bendera kwa kiti cha udiwani kata ya mzimaa,
"Naomba ushirikiane katika kampeni na pia kuhakikisha tunakipa chama Cha mapinduzi ushindi kwa kuwachagua Rais Mbunge na Diwani wa chama Cha mapinduzi" amesema.
EmoticonEmoticon