Showing posts with label afya. Show all posts
Showing posts with label afya. Show all posts

GIZ YATOA MSAADA WA VIFAA TIBA VYENYE THAMANI YA SHILINGI MILIONI 975 KATIKA HALMASHAURI ZA MKO WA TANGA

May 01, 2025 Add Comment



Na Oscar Assenga, TANGA

SERIKALI ya Ujerumani kupitia shirika la  ufadhili wa kimataifa nchini humo (GIZ) limetoa msaada wa  vifaa tiba vyenye thamani ya shilingi Milion 975 vitakavyotumika katika hospitali 20 zilizopo kwenye hamashauri mbalimbali Mkoani Tanga hii ikiwa ni  utekelezaji wa programu yake ya  kusaidia na kuimarisha sekta ya afya hapa nchini.

GIZ ambayo inashirikiana na  Wizara ya afya pamoja ofisi ya Rais tawala za mikoa na Serikali za mitaa (TAMISEMI)kwa lengo la kuboresha utoaji wa huduma  bora kwa mama na mtoto pamoja na afya ya uzazi  utekelezaji wake umeleta mabadiliko chanya  katika vituo vya afya vilivyoguswa na mpango huo ambao umeanzishwa muda mrefu.



Akipokea vifaa hivyo Mkuu wa mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batilda Buriani ameipongeza Serikali ya Ujerumani  kupitia shirika la GIZ  ambapo kupitia msaada huo unakwenda kuongeza juhudi za Serikali katika kupambana kupunguza na kuondoa kabisa vifo vya wajawazito, wakinamama pamoja na watoto wachanga waliopo chini ya miaka mitano.

Alisema lengo kubwa la Rais ni kupunguza vifo vya wakina mama wajawazito na watoto wachanga chini ya miaka mitano na wameona mafanikio vifo vimepungua kwa kiasi kikubwa sana sasa wamewasaidia kupata vifaa hivyo ili kuongeza vifaa tulivyonavyo na kuhakikisha kwamba watoto wetu wanaozaliwa njiti , wanaozaliwa  na manjano , wanaozaliwa na changamoto ya upumuaji , wanakuwa salama wanapongeza na kuwashukuru kwa msaada huo



Aliongeza kuwa licha ya vifaa hivyo vilivyotolewa bado kuna uhitaji kutokana na idadi kubwa ya wananchi wanaohitaji kupatiwa huduma mbalimbali ambapo ametumia nafasi hiyo kuwaomba shirika la GIZ kuangalia uwezekano wa kuendelea kuwezesha upatikanaji wa wa vifaaa vingine.

" Tumekuwa na mazungumzo na tumekubaliana kwamba waongeze vifaa hivi ni kweli tumepata vingi lakini bado uhitaji ni mkubwa  tunaomba hivi vifaa vilivyopo viongezeke zaidi kutokana na idadi kubwa ya wahitaji tulionao katika vituo na hospitali zetu za halmashauri tuna imani kuwa tutaongezewa ili kuhakikisha kwamba huduma za wakina mama na watoto zinakwenda karibu zaidi na wananchi ikiwemo huduma za kibobezi" aliongeza.



Awali alizungumza Meneja wa  mradi huo hapa nchini Kai Strahler-Pohl  alipongeza juhudi za Serikali katika kuendelea kukabiliana na kupunguza  vifo vya watoto wachanga , kuboresha matokeo ya afya wakina mama na watoto, sambamaba na kuimarisha miundombinu ya vituo vya afya.

Alisema mpango huo umelenga katika  kuwezeshwa uwepo wa  vifaa tiba vya kutosha kwaajili ya kuanzisha vitengo vipya vya utoaji wa huduma  za utunzaji wa watoto wachanga (NCU) katika hospitali za wilaya zote zilizopo Mkoani Tanga .



" Tunafurahi sana kuimarisha  huduma katika halmashauri zote za mkoa wa Tanga hasa kuweza kuzipatia hospital vitengo  vya utunzaji wa watoto wachanga vinavyofanya kazi kikamilifu takribani wakazi 870,000 sasa wanaweza kuwa na uhakika  kwamba Kila mtoto mchanga mvulana na msichana atatunzwa  vizuri karibu na makazi yao"

" Tunathamini ushirikiano wa Serikali kupitia Wizara ya afya  , TAMISEMI, mikoa halmashauri za wilaya zote  pamoja na Serikali ya Ujerumani kukamilisha hili" alisema Meneja huyo.


Awali akizungumza Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt. Frank Shega alilishukuru shirika la GIZ kwa msaada huo ambao pia umeenda sambamaba na utoaji wa mafunzo ya utendaji wa kazi kwa baadhi ya watumishi kwa lengo la kuwaongezea maarifa na ujuzi katika utoaji wa huduma.



"Tunawashukuru na kuwapongeza sana wenzetu wa GIZ kwa  kutupatia msaada wa vifaa  hivi ambavyo vinakwenda kutusaidia kuhakikisha kuwa tunakuwa na vizazi hai na vyenye afya bora wamekuwa pia wakitoa mafunzo kwa watumishi kwaajili ya kuongeza weledi tumekuwa nao kwa muda mrefu na wamekuwa wadau wetu ambao wamwtusaidia sana" alisema Dkt Shega

Mwisho.

PAC YAIPONGEZA MSD KWA KUJENGA GHALA LA KISASA LA KUHIFADHIA BIDHAA ZA AFYA

March 14, 2025 Add Comment

 

 

Na Mwandishi Wetu.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) chini ya Mwenyekiti wake, Mhe. Naghenjwa Kaboyoka (pichani) imetembelea  na kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa ghala la kisasa la kuhifadhia bidhaa za afya linalojengwa na Bohari ya Dawa (MSD) katika eneo la Kizota, Mkoani Dodoma.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mhe. Kaboyoka ameipongeza MSD kwa kazi kubwa inayoifanya ya ujenzi wa ghala kubwa na kisasa ambalo litakwenda kutatua changamoto za utunzaji wa bidhaa za afya kwa kiasi kikubwa. 

"Kazi mnayoifanya inaonekana, leo tumeona uwekezaji mkubwa wa ghala la hili kubwa na la Kisasa ambalo lina Ubora wa kimataifa, serikali imewekeza hapa zaidi ya Bilioni 23.7 kujenga ghala hili lenye mita za mraba 7,200 sisi kama kamati tunategemea kuona changamoto za utunzaji wa bidhaa za afya zinapungua”.
Aidha pamoja na kupongeza ujenzi wa maghala Mhe. Kaboyoka amepongeza namna MSD inavyosambaza mashine za kusafisha damu kwa wagonjwa wa Figo ambazo zimepelekea kupunguza ghalama za huduma hiyo kwa wananchi. “Siku izi magonjwa ya figo yamekuwa mengi hadi watoto wadogo wanapata ugonjwa huo tunaishukuru MSD kwa kupunguza gharama ya huduma hii baada ya MSD kuanza kusambaza mashine za kusafisha damu sasahivi tunaona huduma hiyo imepungua gharama kwa kiasi kikubwa. 

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya MSD Bi. Rosemary Silaa amesema MSD itaendelea na ujenzi wa Maghala mapya kwa lengo la kutatua changamoto za utunzaji wa bidhaa za afya ambapo baada ya ujenzi huu wa Dodoma na Mtwara MSD itaanza ujenzi wa maghala mapya mkoani Chato, Kilimanjaro, Dar es Salaam, Mwanza na Ruvuma.   MSD kwasasa inauwezo wa kutunza bidhaa hizo kwenye mita za mraba 56,000 huku MSD ikiwa na uhitaji wa mita za mraba 100,000 kukidhi mahitaji yake ya utunzaji.

PAC imetembelea  na kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi wa ghala la kisasa la kuhifadhia bidhaa za afya linalojengwa na Bohari ya Dawa (MSD) katika eneo la Kizota, Mkoani Dodoma.

RAIS DKT SAMIA ATOA MAELEKEZO KWA WAZIRI MCHENGERWA

February 23, 2025 Add Comment


Na Oscar Assenga, HANDENI.

RAIS Dkt Samia Suluhu amemuagiza Waziri wa Tamisemi Mohamed Mchengerwa kuhakikisha wanapeleka kiasi cha Milioni 240 kwa ajili ya kujenga eneo maalumu la Upasuaji wa Mifupa katika Hospitali ya Halmashauri ya wilaya ya Handeni.

Dkt Samia aliyasema hayo leo mara baada ya kufungua Hospitali ya Halmashauri ya wilaya ya Handeni eneo la Mkata ikiwa ni ziara ya siku saba katika Mkoa wa Tanga yenye lengo la kukagua miradi ya maendeleo, kuweka mawe ya msingi na kuzungumza na wananchi.

Alisema kwa sababu wanataka Handeni kuwa eneo maalumu kwa ajili ya Hospitali ya Mifupa pamoja na kuwepo na tiba mbalimbali lakini libaki kuwa maalumu kwa ajili ya mifupa

Aidha alisema kwamba mpaka sasa Hospitali hiyo imeshapokea wajawazito 900 na 300 walijifungua kwa upasuaji na iwapo isingekuwepo lazima kungekuwa na Rufaa na hivyo uwepo wa hospitali hiyo umeokoa maisha ya watu wengi.

Alisema hospitali hiyo ipo barabarani na wakiweka lami kipande kinachotoka Barabarani kwenda hosputali itakuwa karibu na wameamua kujenga aeneo la kufanya upasuaji wa mifupa na ameilekeza Waziri Tamisema aleta fedha milioni 240 ili kujenga eneo la mifupa likamilike,

“Ukiangalie kuna maeneo ya upasuaji mawili eneo la upasuaji ,upauaji wa jumla na mifupa na hakuna wodi na wanalazwa na wagonjwa wengine hivyo ni vema sehemu ya mifupa ikabakia pekee yake na Handeni ikiwa Hospitali maalumu kwa ajili ya mifupa na mambo mengine na watu wengine wake na wagonwa wengine wa mifupa na maeneo mengine waje kupata huduma”Alisema

Rais Dkt Samia aliawapongeza wana kijiji na uongozi wa kijiji cha Mkata Mashariki kwa kutoa eneo la ekari 32 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali hiyo huku akieleza jambo hilo ni la kuigwa kwani kama wangesubiri Serikali itoe eneo pengine mradi ungeweza kuchelewa.

“Mbali na hayo awamu ya sita Serikali katika wilaya ya Handeni wamepeleka Bilioni 4.37 kwa ajili ya Hospitali hiyo na fedha walizipeleka kwa ajili ya kujenga vituo vya afya na zahanati 16 kwa hiyo ni dhamira ya serikali kuwakinga wananchi wasipatwe na magonjwa .

“Ikitokea wanahitaji matibabu wapate huduma za uhakika zilizokaribu nao ndio maana wameendelea ujenzi wa Hospitali hiyo na kuleta vifaa vya kisasa kwa mkoa wa mzima “Alisema

Alisema kwamba wananchi wa handeni wanamshukuru kwa kazi kubwa anayoifanya ya kuliunganisha Taifa na wannachi ikiwemo kuwapeleka wadau ambao waliwashika mkono wakajenga majengo mbalimbali na kuifanya hospitali hiyo kwa bora na yenye viwango vya hospitali ya mkoa.

Mchengerwa alisema ujenzi wa jengo hilo ni mpango wa Serikali kuendelea kusogeza huduma karibu na wananchi na maelekezo ya Rais Dkt Samia Suluhu ya kuelekeza kwamba yajengwe majengo kwa ajili ya kuwahudumia wananchi wa handeni na hiyo ni kazi kubwa ya kuunganisha Taifa na mahusiano na watu mbalimbali duniani.

“Wananchi walipata bahati ya kupata wadau wa maendeleo kutushika mkono na kujenga majengo mbalimbali na kuifanya Hospitali yetu kuwa bora na yenye viwango vya Hospitai ya mkoa na kazi hiyo imekwenda kuokoa maisha ya watoto, wakina mama wanaokwenda kujifungua na maisha ya wapiti njia”Alisema

Hata hivyo alisema kwamba Serikali imewezesha ujenzi wa Majengo 15 ya huduma za maabara, majengo muhimu za huduma za nje, huduma za dharura, huduma za mionzi,jingo la huduma za wuzazi ,jengo la dawa na kipindi cha muda mfupi umweza kuokoa maisha ya wakina mama na watoto.

“Mhe Rais Sekta ya Afya inafanya kazi kubwa ya kuokoa maisha ya wakina mama na watoto na wilaya ya Handeni hakuna kifo cha mama na mtoto na wahudumu katika sekta hii wamebadilika na wanafanya kazi kwa bidii kuhakikisha wanaokoa maisha ya watanzania.

Hata hivyo alisema katika Mkoa wa Tanga fedha ambazo zilitolewa na Serikali kwenye sekta ya afya wametoa Bilioni 65.6.


RAIS DKT SAMIA KUPOKEA TUZO YA "THE GATES GOALKEEPERS AWARD

February 03, 2025 Add Comment


Na WAF - Dar Es Salaam

 

Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan anatarajia kupokea tuzo ya “The Gates Goalkeepers Award” kama kielelezo cha matokeo makubwa ambayo yamepatikana kwenye uongozi wake kufuatia ripoti ya utafiti wa demografia na afya ya mwaka 2022 inayoonesha kupungua kwa vifo vitokanavyo na uzazi kwa asilimia 80.

 

Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama amesema hayo  Februari 3, 2025 wakati akitoa taarifa ya upokeaji wa tuzo hiyo ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan zinazoandaliwa na taasisi ya The Gates Foundation, mbele ya waandishi wa habari kwenye ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.


Waziri Mhagama amesema tukio hilo linafanyika nje ya Marekani nchini ya Tanzania kwa mara ya kwanza na Rais Samia ndiye kiongozi wa kwanza kupokea tuzo hiyo kwa bara la Afrika jambo lililochochewa na uongozi wake mahiri ulioleta mafanikio makubwa nchini hususani ni sekta ya afya kwa kuitendea haki na kusababisha mataifa makubwa duniani kutambua mchango wake.

 

Amesema kuwa mafanikio haya yametokana na mikakati mbalimbali iliyotekelezwa na inayoendelea kutekelezwa kutokana na utashi wa kisiasa chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia kuweka mazingira wezeshi kisera pamoja na  kuimarisha rufaa za akina mama na watoto. 

 

“Rais Samia ameongeza bajeti ya kuimarisha huduma ikiwemo upatikanaji wa dawa na vifaa tiba, kusogeza huduma za dharula za uzazi karibu na wananchi kwa kujenga zaidi ya vituo 530 vya upasuaji wa kutoa mtoto tumboni,” amesema Waziri Mhagama

 

Waziri Mhagama ameipongeza Taasisi ya The Gates Foundation kwa kutambua na kuunga mkono juhudi za serikali kwenye kupambana na vifo vitokanavyo na uzazi, Watoto wachanga na walio na umri chini ya miaka mitano (5).

 


“Kwa namna ya kipekee, tunatambua jitihada za kipekee za Amiri jeshi Mkuu Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mapambano ya vifo vya kina mama vinavyotokana na uzazi, vifo vya Watoto wachanga na Watoto walio chini ya miaka mitano, hivyo wananchi wenzangu tunayo kila sababu ya kumpongeza na kutembea kifua mbele kwa jinsi Mheshimiwa Rais anavyotung’arisha nchi yetu nje ya mipaka ya nchi yetu,” amesema Waziri Mhagama

KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA AFYA NA MASUALA YA UKIMWI YAKAGUA UTEKELEZAJI WA AFUA ZA UKIMWI NJOMBE

January 09, 2025 Add Comment




NA.MWANDISHI WETU

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Masuala ya UKIMWI, imetembelea miradi mbalimbali  mkoani Njombe leo tarehe  09 Januari, 2025.

Kamati hiyo imetembelea kituo cha Afya cha Njombe Mjini kilichopo katika Halmashauri ya mji wa Njombe kwa lengo la kujionea huduma zinazotolewa katika kituo hicho ikiwemo huduma za upimaji UKIMWI, pamoja na kutembelea Shirika lisilo la kiserikali "COCODA"  linalohudumia watu wanaishi na virusi vya UKIMWI.

Kamati hiyo imeongozwa na  Mhe. Dr. Elibariki Kingu Mwenyekiti wa kamati na Mbunge wa Singida Magharibi, akiambatana na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anaeshughulikia Masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Mheshimiwa Ummy Nderiananga


.

Aidha kamati imepokea taarifa ya mambukizi ya UKIMWI mkoani Njombe,  ambapo mkoa una watu 66,979 wanaishi na Virusi vya UKIMWI huku jitihada mbalimbali zikiendelea kufanyika ikiwa ni pamoja na ugwaji wa kondom.

Hata hivyo kamati imetoa pongezi kwa Mkoa wa Njombe, kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na Asasi zinazojihusisha na suala la kuhakikisha maambukizi ya VVU, yanapungua Mkoani Njombe.

Pamoja na hayo, Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Ummy Nderiananga, ametoa shukrani kwa kamati ya kudumu ya Bunge, huku akiahidi Serikali kuendelea kushirikiana na wadau kwani bado kuna changamoto kubwa ya maambukizi ya VVU kwa vijana.




MAAMBUKIZI YA VVU YAPUNGUA NCHINI TANZANIA-WAZIRI MHAGAMA

December 02, 2024 Add Comment

 

Leo ni tarehe 1 Desemba 2024, ambapo dunia inaadhimisha Siku ya UKIMWI Duniani. Kitaifa, maadhimisho haya yamefanyika Mkoani Ruvuma yakiongozwa na mgeni rasmi, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.  Dkt. Philip Mpango.

Akitoa taarifa yake, Waziri wa Afya nchini, Mheshimiwa Jenista Mhagama, ameeleza juhudi za serikali katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa UKIMWI. 

Amesema, Serikali imeendelea kugharamia dawa za kufubaza makali ya virusi vya UKIMWI (ARVs), hatua inayosaidia wananchi wanaoishi na maambukizi ya virusi hivyo kuendelea na maisha ya kawaida.

Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa, wananchi takriban milioni 1.7 wanaishi na maambukizi ya virusi vya UKIMWI nchini. 

Serikali imetumia shilingi bilioni 750 kununua dawa za ARVs, ambapo gharama ya matibabu kwa kila mgonjwa mmoja ni takriban shilingi 400,000 kwa mwaka.

"Maadhimisho haya ni fursa muhimu ya kuongeza uelewa kuhusu ugonjwa wa UKIMWI na kupunguza unyanyapaa" amesema Mhe. Jenista

Pamoja na hayo  amehimiza jamii kuchukua hatua za kinga na matibabu kwa ushirikiano wa karibu na wadau mbalimbali. 

Kaulimbiu ya mwaka huu inalenga kuimarisha mshikamano wa kidunia katika kukomesha maambukizi mapya na kuboresha huduma kwa walioathirika.

MAAMBUKIZI YA VVU YAPUNGUA NCHINI TANZANIA-WAZIRI MHAGAMA

December 01, 2024 Add Comment




Leo ni tarehe 1 Desemba 2024, ambapo dunia inaadhimisha Siku ya UKIMWI Duniani. Kitaifa, maadhimisho haya yamefanyika Mkoani Ruvuma yakiongozwa na mgeni rasmi, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.  Dkt. Philip Mpango.


Akitoa taarifa yake, Waziri wa Afya nchini, Mheshimiwa Jenista Mhagama, ameeleza juhudi za serikali katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa UKIMWI. 


Amesema, Serikali imeendelea kugharamia dawa za kufubaza makali ya virusi vya UKIMWI (ARVs), hatua inayosaidia wananchi wanaoishi na maambukizi ya virusi hivyo kuendelea na maisha ya kawaida.


Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa, wananchi takriban milioni 1.7 wanaishi na maambukizi ya virusi vya UKIMWI nchini. 


Serikali imetumia shilingi bilioni 750 kununua dawa za ARVs, ambapo gharama ya matibabu kwa kila mgonjwa mmoja ni takriban shilingi 400,000 kwa mwaka.


"Maadhimisho haya ni fursa muhimu ya kuongeza uelewa kuhusu ugonjwa wa UKIMWI na kupunguza unyanyapaa" amesema Mhe. Jenister


Pamoja na hayo  amehimiza jamii kuchukua hatua za kinga na matibabu kwa ushirikiano wa karibu na wadau mbalimbali. 


Kaulimbiu ya mwaka huu inalenga kuimarisha mshikamano wa kidunia katika kukomesha maambukizi mapya na kuboresha huduma kwa walioathirika.

SERIKALI YADHAMIRIA KUMALIZA TATIZO LA UKIMWI NCHINI

December 01, 2024 Add Comment


Siku ya Ukimwi Duniani, Imeadhimishwa Kitaifa leo tarehe 01/12/2024, maadhimisho yamefanyika katika Uwanja wa Majimaji, Manispaa ya Songea, mkoani Ruvuma. 

Hafla hii imeongozwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Mpango, ambaye amesisitiza azma ya serikali kuhakikisha inatokomeza maambukizi ya Virusi vya UKIMWI (VVU) nchini

Katika hotuba yake, Mhe. Dkt. Mpango, ameonesha dhamira ya dhati ya Serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kupambana na maambukizi mapya ya VVU.

Takwimu zinaonesha kwamba vijana, hasa wa kike, wako katika hatari kubwa ya kuambukizwa. Kwa mujibu wa Makamu wa Rais, serikali imeweka mkazo mkubwa katika kutoa elimu kwa vijana ili kuwasaidia kujitambua, kuchukua hatua za kujikinga, na kwa wale wanaoishi na VVU, kuhakikisha wanafuata taratibu kwa kutumia dawa za kupunguza makali ya virusi (ARVs).

Aidha, Mhe. Dkt. Mpango ametoa wito kwa jamii nzima kushirikiana, kuhakikisha kwamba maambukizi mapya yanapungua, kwa kuelimisha vijana kuhusu umuhimu wa afya ya uzazi, matumizi sahihi ya kinga, na upimaji wa afya mara kwa mara


WAZIRI MHAGAMA AZINDUA USAMBAZAJI WA RIPOTI YA UTAFITI WA VIASHIRIA NA MATOKEO YA UKIMWI 2022-2023

November 29, 2024 Add Comment




Na.Mwandishi Wetu -Ruvuma

Waziri Afya Mheshimiwa Jenista Mhagama amezindua Usambazaji wa Ripoti ya Utafiti wa Viashiria na Matokeo ya UKIMWI 2022-2023 Mkoani Ruvuma.


 Akizungumza katika uzinduzi huo uliofanyika Wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma tarehe 29 Novemba, 2024 Waziri Mhagama alieleza mafanikio makubwa yaliyopatikana katika juhudi za kudhibiti maambukizi ya UKIMWI nchini Tanzania ambapo imeelezwa kuwa kiwango cha Maambukizi Mapya kimepungua huku akipongeza juhudu zinazofanywa na Tume ya Kudhibiti UKIMWI Nchini 

"Kwa mujibu wa ripoti hiyo, kiwango cha maambukizi ya UKIMWI nchini kimepungua kwa kiasi kikubwa kutoka asilimia 7 mwaka 2022 hadi asilimia 4.4 mwaka 2023. Aidha, juhudi za kupunguza maambukizi ya mama kwenda kwa mtoto zimezaa matunda, ambapo kiwango cha maambukizi kimepungua kutoka asilimia 18 mwaka 2010 hadi asilimia 8.1 mwaka 2023," alisema Waziri Mhagama

Waziri Mhagama alieleza kuwa mafanikio haya yametokana na juhudi za Serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo, sekta binafsi, na jamii katika kuimarisha programu za utoaji elimu, upimaji wa hiari, na matumizi ya dawa za kufubaza makali ya virusi vya UKIMWI (ARVs).


Alisisitiza umuhimu wa kuendelea na juhudi hizi ili kufikia malengo ya kumaliza maambukizi mapya ya UKIMWI, hasa kwa watoto, ifikapo mwaka 2030. Vilevile, aliwahimiza wananchi kuendelea kuchukua hatua za kujikinga na maambukizi na kufuata ushauri wa kitaalamu.

Aidha alitoa wito kwa jamii kuunga mkono mikakati ya kitaifa ya kupambana na UKIMWI ili kuhakikisha maendeleo ya afya ya jamii na uchumi wa taifa kwa ujumla.


Kwa upande wake Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera, Bunge na Uratibu Mheshimiwa Ummy Nderiananga, amesema Watanzania wamepiga hatua kubwa katika mapambano dhidi ya maambukizi ya Virusi vya UKIMWI (VVU)ambapo asilimia 98 ya Watanzania wanaohitaji dawa za kufubaza makali ya virusi hivyo (ARVs) sasa wanatumia dawa hizo, hatua ambayo imevuka malengo yaliyowekwa kitaifa na kimataifa.

Mhe. Ummy alibainisha kuwa mafanikio haya ni matokeo ya jitihada za serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, ikiwemo utoaji wa elimu ya afya, upimaji wa hiari, na utoaji wa dawa kwa urahisi katika vituo vya afya.

Pia ametumia nafasi hiyo kuhimiza wananchi kuendelea kuchukua hatua za kujikinga na kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa kuendelea kutumia dawa kwa walioambukizwa ili kuboresha maisha yao na kupunguza maambukizi mapya.


Serikali inaendelea kuweka mikakati imara kuhakikisha kila Mtanzania anayehitaji huduma za matibabu anazipata kwa wakati.
Maadhimisho ya Wiki ya UKIMWI Duniani yanaadhimishwa Kitaifa mkoani Ruvuma yenye kauli Mbiu isemayo "Chagua Njia Sahihi, Tokomeza UKIMWI"

=MWISHO=

WAZAZI WENYE WATOTO WANAOISHI NA KIFAFA WALILIA TOTO AFYA CARD

November 26, 2024 Add Comment


Na Arodia PETER 


WAZAZI wenye watoto wanaougua ugonjwa wa kifafa wameiomba serikali kuangalia uwezekano wa kurudishia utaratibu wa Bima ya afya kwa watoto (Toto Afya Card) ili waweze kupata matibabu ya uhakika.


Walisema baada ya Serikali kusitisha utaratibu wa "Toto Afya Card" watoto wao wameacha kutumia dawa kutokana na gharama kubwa, hivyo kutishia uhai wao wa kuishi. 


Ombi hilo kwa serikali lilitolewa na baadhi ya wazazi wenye watoto wanaishi na hali ya kifafa waliohudhuria kongamano lililiandaliwa Chama cha Wazazi Wenye watoto wenye kifafa Tanzania (UWAKITA) kwa kushirikiana na Idara ya Afya ya Akili Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) Jumamosi Novemba 23 mwaka huu. 



Mmoja wa wazazi hao, Glory Elihuruma Mrema mkazi wa Dar es Salaam alisema mtoto wake ameacha kwenda hospitali kuhudhuria kliniki na kupata dawa zaidi ya miezi 9 sasa kutokana na yeye kushindwa kumudu gharama hizo tangu bima ya watoto ilipositishwa na serikali. 


Alisema gharama za matibabu kwa watoto wenye ukifafa zina gharama kubwa kwa mtu ambaye hana kipato cha kutosha, jambo ambalo linatishia uhai wa watoto hao pamoja na kuwasababishia wazazi msongo wa mawazo.


"Kwa mfano kidonge kimoja cha mil gram 500 kinauzwa shilingi 1500 kwa bei ya rejareja. Na kwa mujibu wa watabibu wetu, mtoto mmoja anapaswa kumeza vidonge vinne kila siku, yaani viwili asubuhi na viwili jioni, hapo bado dawa ya usingizi ambayo kidonge kimoja kinauzwa shilingi 500. Hivyo kwa siku moja mgonjwa wa kifafa anatumia Shilingi 6500.



"Kilio changu kwa Rais wetu, Samia Suluhu Hassan atuangalie kwa jicho la pekee, watoto wanaoishi na kifafa usalama wao ni dawa na chakula. Kama mtoto mwenye hali hiyo hajanywa dawa, ndani hapakaliki, wazazi tumebaki majumbani  tunashindwa kufanya shughuli za kujitafutia kipato kwa sababu huwezi kumwacha huyu mtoto peke yake ndani." alisema Glory. 


Mzazi mwingine, Avelia Said ambaye mtoto wake anaishi na kifafa kwa miaka 17 sasa, anasema kilio chake kwa serikali ni kupata matibabu ya uhakika kwa mtoto wake.


Alisema gharama za dawa kwa siku ni zaidi ya Shilingi 6000, na yeye hana kipato baada ya mumewe kufariki mwezi Agosti mwaka huu. 


Anasema kwa sasa mtoto wake anaishi kwa kutegemea misaada ambapo mtu akimwonea huruma anamnunulia dawa za ziku tano au nusu mwezi, na zinapokwisha hali ya mtoto inazidi kuwa mbaya. 


"Ombi langu kuu sisi wenye watoto wanaotegemea kuishi kwa dawa, serikali ituangalie kwa jicho la kipekee tupate hiyo bima ya watoto ili watibiwe kwa uhakika"alisisitiza Avelia.


Naye daktari bingwa wa magonjwa Afya ya akili wa hospitali ya Taifa Muhimbili, Dkt Kuganda Said alisema inahitajika elimu sahihi kwa jamii kuhusu ugonjwa wa kifafa kwamba dawa na wataalam wapo na unatibika.


Dkt.Kuganda ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Wazazi wa watoto wenye kifafa Tanzania  (UWAKITA), alisema chama hicho kinasisitiza elimu juu ya ugonjwa huo na jamii ielewe kwamba wataalam wa wapo, vifaa vya uchunguzi vipo na ugonjwa wa kifafa unatibika, hivyo watu waache unyanyapaa kwani ni kikwazo kwenye tiba ya ugonjwa huo.


Kwa upande wake,  Dkt. Nuruel Kitomary ambaye pia ni bingwa Afya na magonjwa ya akili wa Hospitali ya Taifa Muhimbili -Upanga Dar es Salaam, alisema zaidi ya watu milioni 50 duniani wanaishi na hali ya ukifafa; ambapo asilimia 80 wanatoka nchi zenye hali duni barani Afrika na Tanzania ikiwemo.


"Kati ya hao, watu milioni 10 wanaishi Afrika, na Tanzania  inakadiriwa kuwa na watu 450, 000 mpaka 500,000 wanaoishi na hali ya ukifafa ambapo ni asilimia 3.7 tu ndiyo wapo  kwenye matibabu.


"Hata hivyo hawa ni wale wenye usajili rasmi hospitalini, lakini kuna kundi kubwa nje ya hao ambao wamefichwa majumbani au wapo kwa waganga wa kienyeji, makanisani nakadhalika." alisema Dkt Kitomary.


Naye Mkurugenzi Msaidizi wa magonjwa yasiyoambukiza na afya ya akili kutoka Wizara ya Afya, Omary Ubuguyu alisema mkakati wa Serikali ni kuhakikisha vipimo na dawa ya msingi iitwayo phinobabitol inapatikana katika hospitali na vituo vya afya nchi nzima.


"Ingawa kuna dawa nyingine zaidi ya hiyo, lakini angalau hiyo ya msingi ambayo inasaidia kwa asilimia 70 wagonjwa wa kifafa inawasaidia.


Kuhusu bima ya afya, Dkt Ubuguyu alisema serikali ipo mbioni kukamilisha mpango wa afya kwa wote ambapo kila mtanzania atanufaika na huduma hiyo.


TRILIONI 6.7 YAFANYA MAGEUZI MAKUBWA SEKTA YA AFYA

November 08, 2024 Add Comment

 Na WAF - Dodoma


Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Godwin Mollel amesema Shilingi Trilioni 6.7 zilizotolewa na Serikali inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan zimechangia kuleta mageuzi makubwa ya upatikani wa huduma bora za afya ikiwemo matibabu ya kibingwa nchini.

Dkt. Mollel amesema hayo wakati akichangia hoja kwenye Kamati ya Mipango na Uwekezaji Novemba 07, 2024 bungeni jijini Dodoma.

“Uwekezaji wa kiasi cha Shilingi Trilioni 6.7 umeleta mabadiliko makubwa katika huduma za afya, hali ya ubora wa huduma za afya umeendelea kuimarika nchini na hospitali zote za rufaa sasa zimepata vifaa vya kisasa, ikiwemo CT Scan, huku hospitali za kanda zikifungwa mashine ya MRI, hatua inayomuweka Rais Samia katika rekodi za kihistoria,” amesema Dkt. Mollel.

Dkt. Mollel amesema kiwango cha vifo vya kina mama kimepungua kutoka 556 hadi 104, akieleza kuwa mafanikio hayo yanaonesha upunguzaji wa asilimia 81.2 katika vifo vya uzazi.

Ameongeza kuwa Serikali imepunguza vifo vya wagonjwa wa kansa kwa asilimia 78, kutokana na upatikanaji wa matibabu ya kisasa ndani ya nchi.

Dkt. Mollel ameeleza kuwa kwa sasa Watanzania wengi hawalazimiki kwenda nje ya nchi kutibiwa, tofauti na ilivyokuwa kipindi cha nyuma ambapo mgonjwa aliyetakiwa kwenda India kupata matibabu alihitaji zaidi ya milioni 100, lakini sasa gharama zimepungua hadi milioni 10, huku huduma hizo zikitolewa ndani ya Tanzania. Kutokana na maboresho haya, rufaa za matibabu nje ya nchi zimepungua kwa asilimia 97.

Aidha, Naibu Waziri huyo amesema kuwa vifaa vya kisasa kama PET CT Scan vimewekwa ili kugundua kansa mapema, hata ile inayoweza kuibuka miaka 10 ijayo. Mafanikio haya yamewezesha wagonjwa 10,931 kutoka nje ya Tanzania kufika nchini kwa ajili ya matibabu, jambo linalodhihirisha uwekezaji mzuri uliofanywa na Rais Dkt. Samia katika sekta ya afya.