Showing posts with label habari. Show all posts
Showing posts with label habari. Show all posts

UDOM Yaja na Mashine ya Kuuza Vinywaji Inayojiendesha

July 03, 2025 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), kupitia Ndaki ya Sayansi za Kompyuta na Elimu Angavu, kimebuni mashine ya kisasa ya kuuza vinywaji baridi inayojiendesha yenyewe bila kuhitaji uwepo wa mtu kwa ajili ya kutoa huduma kwa mteja.

NEEC WAJA NA FURSA ZA KIUCHUMI KATIKA MAONEHO YA 49 YA KIMATAIFA YA BIASHARA (SABA SABA)

July 03, 2025 Add Comment
Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) linashiriki katika maonesho ya 49 ya kimataifa ya Biashara katika banda la Ofisi ya Waziri Mkuu na watakuwepo hapo kipindi chote cha maonesho ili kuwawezesha Watanzania.

MRADI WA BOMBA LA GESI NTORYA–MADIMBA KUGHARIMU SHILINGI BILIONI 120

July 03, 2025 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SHIRIKA la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limesaini mkataba wa makubaliano na kampuni ya China ya CPP na CPTDC kwaajili ya ujenzi wa bomba la gesi asilia kutoka Ntorya hadi Madimba mkoani Mtwara kwa kipindi cha miezi 12.

TBS YAWASILISHA UTEKELEZAJI WA SERA YA KURUDISHA KWA JAMII

July 03, 2025 Add Comment
EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limepokea tuzo kutoka Taasisi ya Foundation for Disabilities Hope, kutokana na desturi waliyojiwekea kutoa mchango wao kwa watu mbalimbali hususani jamii ya watu wenye ulemavu.

NAIBU WAZIRI UMMY AMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUGHARAMIA MAZISHI WALIOFARIKI SAME

July 03, 2025 Add Comment


Na Mwandishi Wetu - KILIMANJARO


Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera,Bunge na Uratibu) Mhe. Ummy Nderiananga amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa moyo wake wa upendo  kwa kugharamia mazishi ya  miili  42 ya watu waliofariki dunia kufuatia  ajali iliyotokea  Wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro.

Mhe. Nderiananga ametoa shukrani hizo  tarehe 03 Julai, 2025 wakati aliposhiriki tukio la kuaga miili 35 katika viwanja vya Hospitali ya Kilimanjaro Christian Medical Centre (KCMC) akisema miili Saba ilichukuliwa na ndugu zao na miili miwili bado vipimo vya DNA vinafanyiwa kazi ili kutambulika.

Tukio hilo lilioongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Bw. Nurdin Babu ambapo Mhe. Nderiananga alimpongeza kwa kujitoa kwa kiasi kikubwa tangu ilipotokea ajali hiyo akishirikiana na watendaji wake wote.

Amesema Serikali  kupitia Idara ya Menejimenti ya Maafa iliyopo Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na Kamati ya Ulinzi na Usalama Mkoa wa Kilimanjaro kwa juhudi kubwa zilizofanyika kuokoa manusura wa ajali hiyo pamoja na miili ya walioungua kwa moto mara baada ya ajali kutokea.

Vilevile ameipongeza Serikali kupitia Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali kwa kuchukua  sampuli za miili hiyo (DNA)  kuhakikisha ndugu wanatambua miili ya wapendwa wao.

Hata hivyo  Mhe. Nderiananga ameendelea kutoa pole kwa Serikali, ndugu, jamaa na marafiki kufuatia msiba huo mzito kwa Taifa  huku akiwaomba kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu hadi watakapokamilisha kuwahifadhi wapendwa wao. 



Aidha, ajali hiyo iliyotokea Juni 28 2025 katika Kitongoji Mahuu, Kata ya Same, takribani kilomita nne kutoka Same mjini, ililihusisha basi kubwa la abiria, Mali ya Kampuni ya Chanel One, lenye namba za usajili T 179 CWL na basi dogo la abiria aina ya Toyota Coaster, lenye namba T 199 EFX linalomilikiwa na Kampuni ya Mwami Trans.




Coaster hiyo, ilikuwa ikitokea Same kuelekea Manispaa ya Moshi, wakati basi la Chanel One lilikuwa likitokea Arusha kuelekea Tanga.

PROF. CAROLYNE NOMBO ARIDHISHWA NA KASI YA UJENZI WA KAMPASI YA MZUMBE TANGA

July 03, 2025 Add Comment
Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Carolyne Nombo ametembelea eneo la ujenzi wa Kampasi mpya ya Chuo iliyopo Wilaya ya Mkinga mkoani Tanga, mnamo tarehe 2 Julai 2025 na kuridhishwa na kasi ya ujenzi huo. Ziara hiyo imelenga kufuatilia maendeleo ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa kampasi hiyo ikiwa ni ufadhili wa Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET).

REA YAJA NA MPANGO KABAMBE WA KUWEZESHA UJENZI WA VITUO VYA MAFUTA VIJIJINI

July 03, 2025 Add Comment
-Mkopo wa hadi Shilingi Milioni 133 kwa riba ya 5%-7% kutolewa

EWURA YAENDELEA KUTOA ELIMU KWENYE MAONESHO SABASABA

July 02, 2025 Add Comment
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu majukumu yake na namna ya kushiriki katika ufuatiliaji wa huduma za nishati na maji nchini, kupitia ushiriki wake kwenye Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere.

WMA Yatoa Onyo Kali kwa Wafanyabiashara Wahujumu Vipimo vya Mafuta

July 02, 2025 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

MENEJA wa Wakala wa Vipimo Tanzania (WMA) Kitengo cha Bandari, Alfred Shungu amesema kuwa wafanyabiashara wanaobainika kuhujumu vipimo vya mafuta, hasa kwa kutumia vifaa visivyotimiza viwango, watachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwemo kifungo au faini isiyozidi Shilingi Milioni 20 kwa kosa la kwanza.

MTENDAJI MKUU ADEM ASISITIZA UMUHIMU WA MAAFISA ELIMU KATA NCHINI KUJENGEWA UWEZO KUHUSU USIMAMIZI WA SHUGHULI ZA ELIMU

July 02, 2025 Add Comment
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM), Dkt. Maulid J. Maulid, ameeleza Maafisa Elimu Kata wanawajibika kusimamia shughuli za elimu kwenye ngazi ya Kata, hivyo ni muhimu Maafisa hao kujengewa uwezo kuhusu usimamizi fanisi wa shughuli za elimu ili kuchagiza maendeleo ya sekta ya elimu katika ngazi ya Kata.

WAZIRI MCHENGERWA AWAFUNDA MA RC WAPYA

June 28, 2025 Add Comment

Na John Mapepele

Mara baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwaapisha na kutoa maelekezo kwa viongozi kadhaa aliowateua ikiwa ni pamoja na Wakuu wa Mikoa, Waziri wa TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa amekutana na kuwafunda.

MWENYEKITI TUGHE MKOA WA DAR ES SALAAM AJITOSA MBIO ZA UBUNGE KIVULE

June 28, 2025 Add Comment


































Hali ya joto la kisiasa katika mtanange wa mbio za Ubunge katika Jimbo jipya la Kivule Mkoani Dear es Salaam, imeanza kupanda, baada ya Mjumbe wa Kamati Kuu Taifa ya Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya Tanzania (TUGHE) *Komredi Brendan Maro, pichani kulia ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama hicho Mkoa wa Dar es Salaam, kujitosa kuchukua fomu ya kuomba kuteuliwa kugombea Ubunge katika Jimbo hilo jipya.


Komredi Maro anakumbukwa kwa jitihada zake za kuwaunganisha Wafanyakazi wa Serikali na Afya (Umma na Sekta Binafsi) Katika kutekeleza wajibu wao kwa waajiri, lakini pia katika kujenga hoja za kulindwa kwa Utu, haki na maslahi ya wafanyakazi. Pamoja na nafasi hizo, Komredi Maro amewahi kuhudumu pia kama Mwenyekiti wa Mkoa wa Shirisho la Vyama huru vya Wafanyakazi (TUCTA) Mkoa wa Dar es Salaam, ambako anakumbukwa kwa kushiriki kikamilifu Katika hoja za maboresho ya Sheria na Kanuni za mafao (Kikotoo), huku akifanikiwa kuwaunganisha na kuwashawishi Wafanyakazi kuendelea kuwa watulivu na kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi, akiwahakikishia TUCTA inaendelea na majadiliano na Serikali Katika kutafuta mwafaka.


 Hivi Karibuni, kupitia Sherehe za MeiMosi, Mhe.Rais *Dkt. Samia Suluhu Hassan,* alitangaza maboresho ya Kanuni hiyo na kupandisha kima cha chini cha mshahara na nyongeza ya mshahara kwa Watumishi wa Umma, kama matokeo ya majadiliano baina ya Serikali na TUCTA.


Komredi Maro, ambaye ni Mkazi wa Kata ya Kitunda, Jimboni Kivule, anatajwa kuwa mmoja kati ya vijana wasomi waliolelewa katika Chama cha Mapinduzi, aliyeshiriki katika kampeni mbalimbali za chama, wenye upeo na uwezo wa uchambuzi, kujenga hoja na kutoa ushawishi kwa watu, sifa zinazopelekea aonekane kuwa mmoja wa watu sahihi sana kwa changamoto za Jimbo la Kivule.


 Aidha, kawaida yake ya ushirikiano siyo tu na viongozi wenzake lakini pia na watu anaowaongoza inatajwa kuwa turufu muhimu kwake Katinka mbio hizo.

Hata hivyo, licha ya uwezo wake wa kuimudu nafasi hiyo, changamoto inayoweza kumkabili ni kuwa mtu aliyetokea kwenye Familia ya kawaida kabisa kiuchumi, hali inayoweza kukwamisha mpambano wake mbele ya watia nia wenye uchumi mkubwa. 


Juhudi za kumpata ili kuelezea jinsi alivyojiandaa na mpambano huu hazikuzaa matunda, baada ya kujibu kwa ufupi kuwa "Chama chetu na Wanakivule wenyewe wanakijua wanachokitaka na namna ya kukipata."

KANISA LA ANGLIKANA DAYOSISI YA DAR YAANDAA BONANZA KUCHANGIA UJENZI WA JENGO LA KITEGA UCHUMI

June 28, 2025 Add Comment
NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Kanisa la Anglikana Tanzania, Dayosisi ya Dar es Salaam kupitia Mtaa wa Mtakatifu Andrea Magomeni, limeandaa Bonanza maalum la kuwakutanisha waumini wake kwa ajili ya kufanya mazoezi ya pamoja, likiwa ni lengo la kuimarisha afya ya kimwili na kupambana na magonjwa yasiyoambukiza.

WATUMISHI WA MAGEREZA MANYARA WAPATIWA MAJIKO YA GESI

June 26, 2025 Add Comment




📌Mifumo ya uzalishaji wa bayogesi 126 mbioni kuanza


📌REA, Jeshi la Magereza kununua mashine 61 za mkaa mbadala


📌REA kuwajengea uwezo magereza uendelezaji miradi ya nishati safi


📌Mha. Saidy amewataka magereza kuwa mabalozi wa nishati safi


Serikali imewapatia watumishi wa Jeshi la Magereza mitungi ya gesi na majiko ya gesi ya kupikia ili kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa watumishi na wananchi iliyolenga kufikia malengo yaliyoainishwa kwenye mkakati wa kitaifa wa matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini.


Hayo yamebaibishwa leo Juni 26, 2025 na Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu Jacob Kingu wakati wa  uzinduzi wa kugawa majiko ya gesi kwa watumishi wa magereza iliyofanyika gereza la Babati mkoani Manyara.


Amesema kuwa, katika mkoa wa Manyara tayari Serikali imegawa mitungi ya gesi na majiko ya gesi yapatayo 330 kwa watumishi wa jeshi la magereza na katika gereza la Babati jumla ya majiko na mitungi 150 wamegawiwa watumishi hao wa magereza. 

Amesema kuwa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeingia makubaliano na Jeshi la Magereza ya kuwawezesha magereza kuhama kutoka katika matumizi ya nishati isiyo salama kwenda katika matumizi ya nishati safi na salama ya kupikia katika magereza yote nchini. 


"Kuanzia mwanzoni wa mwezi januari 2025 jeshi la magereza walishaingia kwenye matumizi ya nishati safi na salama na tayari wameachana na nishati isiyo salama na chafu kwa afya na mbaya kwa mazingira yetu, " Ameongeza. 

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mha. Hassan Saidy amewataka watumishi wa jeshi la magereza  kuibeba ajenda ya Mhe. Rais Samia ya kuwa mabalozi wa nishati safi ya kupikia hapa nchini. 

Katika hatua nyingine Mha. Saidy ameeleza kuwa, mifumo ya uzalishaji wa bayogesi ipatayo 126 tayari ipo mbioni kuanza kwa kushirikiana na jeshi la magereza ambayo itawezesha ununuzi wa mashine za kutengeneza mkaa mbadala 61, vile vile kuwajengea uwezo watumishi wa jeshi la magereza ya kuendeleza miradi hiyo ya nishati.

Kwa upande wake, Mkuu wa Magereza mkoa wa Manyara ACP Solomon Mwambingu amemshukuru Rais Samia kwa kuwapatia watumishi wa magereza majiko ya gesi na mitungi ya gesi na kusisitiza kuwa wataendelea kuwa mabalozi wa nishati safi ya kupikia katika jamii yote inayowazunguka.


SERIKALI YAWAREJESHA WATANZANIA 42 KUTOKA NCHINI IRAN NA ISRAEL.

June 25, 2025 Add Comment
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imefanikiwa kuwarejesha salama nchini Watanzania 42 kutoka nchini Israel na Iran kufuatia vita vilivyokuwa vikiendelea baina ya mataifa hayo mawili.

NIDHAMU, UWAJIBIKAJI CHACHU YA MAFANIKIO KATIKA SEKTA YA ELIMU: MTENDAJI MKUU ADEM

June 25, 2025 Add Comment
Hayo yamesemwa leo tarehe 25 Juni, 2025 na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu – ADEM Dkt. Maulid J. Maulid alipokuwa akifungua rasmi mafunzo ya Utawala Bora wa Elimu kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa yanayotolewa na ADEM kwa Maafisa Elimu Kata 352 kutoka Mkoa wa Dodoma na Kilimanjaro.

Mafunzo hayo yamelenga kuwawezesha Maafisa Elimu Kata kusimamia kwa ufanisi shughuli zote za elimu katika ngazi ya Kata.

Dkt. Maulid J. Maulid amesema Maafisa Elimu Kata wana wajibu wa kutambua na kutafsiri kwa vitendo maono ya Serikali kwa kuhakikisha wanakuwa wasimamizi wa kwanza wa maboresho makubwa yaliyofanyika katika sekta ya elimu kwa kuboresha Sera ya Elimu na Mafunzo ya 2014 Toleo la 2023 na Mtaala ulioboreshwa ili kufikia lengo la Serikali la kuboresha na kuimarisha sekta ya elimu nchini.

“Mabadiliko na mageuzi yanayotegemewa kutokea kwa utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mtaala ulioboreshwa yako kwenye meza zenu kama wasimamizi wa kwanza wa shughuli za elimu katika ngazi ya Kata. Tunawaomba mwende mkasimamie ipasavyo mageuzi hayo na tuone matokeo kuanzia kwenye ngazi ya Shule na Kata kwa kwenda kutekeleza kwa vitendo yale mtakayojifunza kwenye mafuzo haya kwani hayo ndio yatakuwa dira ya kuwasaidia kufanya usimamizi fanisi wa shughuli zote za elimu katika ngazi ya Kata na hatimaye lengo la Serikali kufikiwa”. Amesema Dkt. Maulid.

Aidha, Dkt. Maulid amesisitiza Maafisa Elimu Kata hao kuitambua, kusoma, kuelewa na kutekeleza miongozo yote inayotolewa na Mamlaka zinazosimamia elimu nchini ikiwa ni pamoja na Ofisi ya Kamishna wa elimu ili iwasaidie katika utekelezaji wa majukumu yao ya usimamizi wa shughuli za elimu kwenye ngazi ya Kata kwa ufanisi.

Vilevile Dkt. Maulid amesisitiza usimamizi wa nidhamu, uwajibikaji, ufundishaji na ujifunzaji mahiri wenye kuinua ubora wa elimu inayotolewa shuleni.

Nae Makamu Mkuu wa Chuo Taaluma Dkt. Alphonce J. Amuli amesema washiriki wa mafunzo hayo watajengewa uwezo katika maeneo ya Uongozi, Usimamizi na Utawala katika Elimu, Utawala Bora katika Elimu, Uandaaji wa Mpango wa Jumla wa Maendeleo ya Elimu Ngazi ya Serikali za Mitaa, Ufuatiliaji na Usimamizi Fanisi wa Shule, Usimamizi wa Ujenzi wa Miundombinu ya Shule, Ukaguzi wa Ndani, na Ushirikishwaji wa Jamii na Utatuzi wa Malalamiko katika Elimu. Dkt. Amuli pia amesema kuwa ni dhahiri kwamba, maeneo hayo yatakayowezeshwa yatasaidia kuimarisha usimamizi na uendeshaji wa shule kwa ufanisi.

Mafunzo ya Utawala Bora wa Elimu katika Mamlaka za Serikali za Mitaa yanafanyika kwa siku tatu kuanzia tarehe 25 – 27 Juni, 2025 ADEM Bagamoyo na yamefadhiliwa na mradi wa BOOST chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 






TANZANIA KUTOATHIRIKA MOJA KWA MOJA NA UMOJA WA BRICS.

June 25, 2025 Add Comment

 


Na. Saidina Msangi, WF, Dodoma.

Serikali imesema kuwa Tanzania haitapata athari za moja kwa moja kutokana na mafanikio au changamoto zozote katika Umoja wa BRICS (Brazil, Russia, India, China na Afrika Kusini), zinazoweza kutokea katika sekta ya kiuchumi na fedha hususani ya kujiondoa kwenye Dolarisation kwa kuwa sio nchi mwanachama wa BRICS.

Hayo yalisemwa bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), alipokuwa akijibu swali la Mheshimiwa Zahor Mohammed Haji (Mwera), aliyeuliza faida na hasara ya Tanzania kutokana na msimamo wa nchi za BRICS ambazo zimejipanga kujiondoa kwenye mfumo wa Dolarisation.

Alisema Serikali ya Tanzania imekuwa na ushirikiano wa muda mrefu na nchi za BRICS (Brazil, Russia, India, China na Afrika Kusini) katika nyanja mbalimbali ikijumuisha masuala ya kiuchumi, biashara na diplomasia kwa kuendelea kuwepo kwa balozi za nchi hizo hapa nchini na Tanzania kuwa na balozi katika nchi hizo.

’’Kwa sasa Tanzania sio mwanachama wa BRICS ila inashiriki katika mikutano ya BRICS kama observer, hivyo mafanikio au changamoto zozote katika umoja huo zinazoweza kutokea katika sekta ya kiuchumi na fedha hususani ya kujiondoa kwenye Dolarisation, hatutakuwa na athari za moja kwa moja kwa kuwa sio wanachama wa BRICS,’’ alifafanua Mhe. Chande.

Mhe. Chande alisema mahusiano ya Tanzania na nchi hizo yanadumishwa kwa kuendelea kuwepo kwa balozi za nchi hizo hapa nchini na Tanzania kuwa na balozi katika nchi hizo.

Aliongeza kuwa mahusiano hayo yanaendelea kuleta mafanikio chanya kwa Serikali ya Tanzania kwa kutumia fursa za kiuchumi zinazopatikana katika nchi hizo ambazo pia zinaimarisha mahusiano ya uwili baina yake (bilateral engagement).