Showing posts with label michezo. Show all posts
Showing posts with label michezo. Show all posts

DKT. TULIA AKOSHWA NA CRDB BANK MARATHON IKIKUSANYA BILIONI 2 KUSAIDIA AFYA NA UWEZESHAJI JAMII

August 17, 2025 Add Comment

 


Dar es Salaam, 17 Agosti 2025 - Maelfu ya wakimbiaji na wapenda michezo kutoka ndani na nje ya Tanzania wamejitokeza leo katika viwanja vya The Green, Oysterbay, kushiriki CRDB Bank Marathon 2025, mbio za hisani ambazo mwaka huu zimekusanya Shilingi Bilioni 2 ili kusaidia matibabu ya watoto wenye matatizo ya moyo, wakinamama wenye ujauzito hatarishi, na vijana kupitia programu ya iMBEJU.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson Mwansasu, aliongoza maelfu ya washiriki kwenye msimu huu wa sita wa CRDB Bank Marathon.
Akitoa salamu zake, Dkt. Tulia alipongeza ubunifu wa CRDB Bank Foundation katika kuunganisha jamii kupitia michezo na kusaidia wenye uhitaji, akieleza kuwa mbio hizo ni mfano wa vitendo vya huruma vinavyogusa maisha ya wengi.

“Ushiriki wetu katika CRDB Bank Marathon ni tendo la huruma linaloleta faraja kwa watoto na wakinamama na familia zao. Ni ushahidi kwamba tukishirikiana, tunaweza kubadilisha maisha,” alisema.
Akitoa salamu zake, Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi, aliipongeza Benki ya CRDB na CRDB Bank Foundation kuendelea kuandaa mbio hizo.

Alisema, “CRDB Bank Marathon si tu imekuwa ikikuza afya na mshikamano wa kijamii, bali pia imekuwa ikifungua milango ya ajira na fursa za kiuchumi kwa vijana wetu. Michezo ni sekta inayoweza kubadili maisha, na ninapongeza sana kitendo cha kuweka zawadi nono kwa washindi. Hizi ni fursa ambazo zinaweza kuwa mtaji wa kuanzisha biashara na kuimarisha maisha ya vijana wetu. Serikali itaendelea kushirikiana na wadau kama CRDB Bank Foundation kuhakikisha michezo inakuwa chachu ya maendeleo ya taifa.”

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela, alibainisha kuwa msimu wa sita wa CRDB Bank Marathon umefanyika sambamba na maadhimisho ya miaka 30 ya Benki ya CRDB, na kuendelea kupanua wigo wa matokeo yake ndani na nje ya Tanzania. Kwa mara ya pili, mbio hizi zimefanyika pia nchini Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), zikikusanya fedha kwa ajili ya miradi ya afya na ustawi wa jamii katika nchi hizo.

Nsekela alisema kuwa mbio za mwaka huu zimeweza kuvutia zaidi ya washiriki 16,000, na kufanikisha lengo la kukusanya shilingi bilioni 2 ambapo pamoja na kusaidia maandalizi ya mbio hizo, shilingi milioni 450, zimeelekezwa kusaidia wenye uhitaji katika jamii.

Kati ya hizo shilingi milioni 100 zimekwenda hospitali ya CCBRT kusaidia wakinama wenye ujauzito hatarishi kujifungua salama, shilingi milioni 100 zimekwenda Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) kusaidia upasuaji wa Watoto wenye matatizo ya moyo, na shilingi 250 zitaelekezwa katika uwezeshaji wa vijana.
Akizungumza wakati wa kutangaza matokeo ya mbio hizo, Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Bank Foundation, Tully Esther Mwambapa, alieleza kuwa safari ya msimu wa sita imeanzia Lubumbashi, DRC, ambako zilikusanywa Dola za Marekani 70,000 kwa ajili ya kuboresha huduma za afya katika hospitali ya Jeshi la Ruashi, na kuendelea Bujumbura, Burundi, ambapo zilipatikana Faranga za Burundi milioni 175 kusaidia bima ya afya kwa zaidi ya watu 58,000 wasiojiweza.

Mwambapa alisisitiza kuwa mafanikio haya ni matokeo ya mshikamano wa kipekee wa serikali za nchi shiriki, wadhamini na washiriki, akiwashukuru wadau wote waliotoa jitokeza kuchangia ikiwamo kampuni za bima za Sanlam Life na Alliance Life ambao wamekuwa sehemu ya mbio hizi tangu kuanzishwa kwake.

Washindi wa mbio za mwaka huu upande wa Tanzania kwa Kilometa 42 upande wa wanawake ni Joyloyce Kemuma kutoka Kenya, upande wa wanaume mshindi ni Abraham Kiptum kutoka Kenya. Kilometa 21 upande wa wanawake ni Catherine Syokau kutoka Kenya, na upande wa wanaume ni Joseph Panga kutoka Tanzania. Kilometa 10 upande wa wanawake ni Silia Ginoka kutoka Tanzania, na upande wa wanaume ni Boayi Maganga kutoka Tanzania.

Joseph Panga mshindi wa mbio za Kilometa 21 upande wa wanawake ameeleza furaha yake kushiriki katika mbio hizo na kusema kuwa ushindi wake ni sehemu ya kusaida matibabu ya watoto wenye matatizo ya moyo na matibabu ya wakinamama wenye ujauzito hatarishi hospitali ya CCBRT.

“Mimi kama Mtanzania najisikia fahari kubwa kushiriki kusambaza tabasamu kwa watoto na wakinamama. Ni muhimu watu kufahamu kuwa afya bora ni haki ya kila mtoto, na hakuna mama anayestahili kupoteza maisha wakati wa kujifungua. Tunawashukuru CRDB Bank Foundation kwa kutuleta pamoja katika harakati hizi za kuokoa maisha,” amesema.
CRDB Bank Marathon imekuwa jukwaa muhimu la kuchochea ustawi wa kijamii katika ukanda huu wa Afrika ya Mashariki na kati hivi karibuni ikipata heshima ya kutambuliwa kimataifa kwa kushinda tuzo ya jukwaa bora la taasisi za fedha katika kusaidia kusaidia jamii.

KILIMANJARO YA SWEDEN YATWAA UBINGWA WA BONANZA LA SERENGETI NCHINI UBELGIJI

August 17, 2025 Add Comment

Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mhe. Mobhare Matinyi (kushoto) na Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji, Mhe. Jestas Nyamanga, wakimkabidhi kombe la ubingwa wa Bonanza la Serengeti nahodha wa timu ya Kilimanjaro kutoka Sweden, Abbas Bachu, baada ya kushinda fainali ya michuano hiyo iliyofanyika jijini Antwerp, Ubelgiji, tarehe 15-16 Agosti, 2025.


Na Mwandishi Wetu, Antwerp, Ubelgiji.


Timu ya soka ya Watanzania iitwayo Kilimanjaro kutoka Sweden imetwaa tena kwa mara ya nne mfululizo ubingwa wa kombe la Bonanza la Serengeti katika michuano iliyofanyika tarehe 15-16 Agosti, 2025, jijini Antwerp, Ubelgiji.


Kilimanjaro ilitetea ubingwa wake baada ya kuifunga timu nyingine ya Watanzania kutoka Uingereza iitwayo Leeds Swahili mabao 2-1 kwenye mchezo mkali wa fainali. Magoli ya Kilimanjaro yalifungwa na Feisal Amir na Fryad Sabri huku la Leeds likifungwa na Murtaza Fuad. Hii ni mara ya tatu kwa timu hizi kukutana fainali.


Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji, Mhe. Jestas Nyamanga, alimkabidhi kombe la ubingwa nahodha wa Kilimanjaro, Abbas Bachu, ambaye naye alimkabidhi Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mhe. Mobhare Matinyi, na kuibua shwange za washabiki wao. Kilimanjaro hushiriki ligi ya daraja la sita nchini Sweden katika mfumo wa madaraja saba.


Michuano hiyo iliyofanyika kwa mara ya nne tangu mwaka 2021 na kudhaminiwa na Benki ya NBC na kampuni ya ASAS, zote za Tanzania, huandaliwa kwa lengo la kuwaunganisha Watanzania Ughaibuni, kukuza vipaji vya soka na kuitangaza Tanzania kimataifa. Mkurugenzi wa Diaspora kutoka Tanzania, Salvatory Mbilinyi; Balozi wa Tanzania nchini Uholanzi, Mhe. Caroline Chipeta; na Mabalozi wa Kenya, Sudan Kusini na Somalia nchini Ubelgiji nao walishuhudia.


Jumla ya timu 15 za Watanzania na watu wa Afrika Mashariki waishio barani Ulaya zilimenyana. Waandaaji Tanzania walikuwa na timu kumi kutoka Sweden, Ubelgiji, Uholanzi, Uingereza, Scotland, Ujerumani na Ufaransa huku Burundi ikiwa na timu tatu na moja moja kutoka Rwanda na Somalia.

USHIRIKI WA WATUMISHI KATIKA MICHEZO NI CHACHU KUJENGA MSHIKAMANO NA KUBORESHA AFYA ZAO-MHANDISI HILLY

July 20, 2025 Add Comment


Na Oscar Assenga, TANGA


USHIRIKI wa Watumishi katika michezo umetajwa kwamba ni njia nzuri ya kujenga amani na mshikamano ambao unaweza kuboresha afya zao na hivyo kuongeza ufanisi na tija mahala pa kazi.

Hayo yalisemwa leo na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watumia Huduma ya Maji nchini (ATAWAS) Mhandisi Geofrey Hilly wakati akifungua Fainali za Mashindano ya Sekta ya Maji maarufu kama Maji Cup yanayoendelea kwenye viwanja vya CCM Mkwakwani Jijini Tanga.

Mhandisi Hilly alisema watumishi wanaposhiriki michezo wanatekeleza maelekezo ya Serikali kuhakikisha wafanyakazi wanashiriki michezo kadri inavyowezekana ili kuimarisha afya zao lakini na kuongeza ufanisi kazini

Alisema kwamba wanafanya hivyo ili kuhakikisha wanakuwa na afya njema na kufanya kazi zao kwa tija kutokana na kwamba wanaposhiriki michezo inaweza kuwaondolea mambo mbalimbali ikiwemo msongo wa mawazo.

“Tunafanya michezo yetu tufahamiane vizuri Mamlaka na Mamlaka ili tuweze kupeana changamoto na
utatuzi kwenye maeneo yetu tunayofanya kazi.

Aidha alisema kwamba mamlaka hiyo imeonyesha mfano bora wa kuweza kutafuta fedha nje ya njia zilizozoeleka ya kufanya miradi ya maendeleo wanaishukuru serikali kuwapa sapoti na kutoa ruhusa ya kufanikisha jambo hilo walitoa hati fungani yenye thamani ya Bilioni 53.12.

Alisema kutokana na hilo walifanikiwa na Taasisi ya kwanza ya umma Afrika Mashariki na kati kutoa hati fungani kama taasisi ya serikali ni miongoni mwa mafanikio ya serikali.

Mhandisi Hilly alisema kwamba katika michezo hiyo ya mwaka huu walivyoanza mpaka sasa wanaangalia mafanikio ya serikali ya awamu ya sita katika sekta ya maji chini ya Rais Dkt Samia Suluhu .

Alisema katika ilani ya CCM walipanga kuwafikishia huduma ya maji asilimia 85 vijijini na 95 mijini sasa wanavyozungumza licha ya miradi mingi inayoendelea nchini asilimia 83 vijijini na asilimia 93 mijini hivyo miradi inayoendelea ifikapo mwezi Desemba watakuwa zaidi ya asilimia 85 vijijini na mijini zaidi 95.

Hata hivyo alisema kwamba katika utekeleza ilani miradi ya maendeleo umefanyika vizuri wanatoa pongezi kwa viongozi huku akieleza namna Waziri wa Maji Jumaa Aweso anavyopambana na kwa juhudi za Rais Dkt Samia Suluhu wamefanikisha.

Awali akizungumza Mtendaji Mkuu wa Jumuiya ya Watumia Huduma ya Maji nchini (ATAWAS) Constantino Chiwaligo alisema mashindano hayo yana umuhimu mkubwa kutokana na sehemu ya kuongeza hamasa,mshikamano na kubadilishana uzoefu.

Alisema tokea mashindano hayo yalipoanzishwa mwaka 2021 na Waziri wa Maji Jumaa Aweso ambaye alitoa maelekezo ya kuwaeleza wajaribu kushirikisha jamii katika shughuli mbalimbali zinazohusiana na utoaji wa huduma ya maji na usafi wa mazingira.


Alisema pale wanaposhiriki jamii watumie michezo kupeleka huo ujumbe ikiwemo kuwapa maelekezo ya kuwaeleza waanzisha Michezo ya Maji Cup na wamekuwa waktekeleza pale na kutoa kauli mbiu kila mwaka.

Huu ni mwaka wa tano katika mashindano hayo na mwaka huu ujumbe wa mwaka huu ni kuangalia mafanikio ya sekta ya maji serikali ya awamu ya sita na wakaanza maji cup lig na kushirikisha timu kutoka kanda nane Tanzania na wametembea Tanzania nzima

Hata hivyo afisa Raslimali watu wa Tanga Uwasa Benard Wambura alisema kuwa jumla ya taasisi 14 zimeweza kushiriki katika michuano hiyo katika mpira wa miguu kwa wanaume na na netball kwa wanawake.

“ushiriki wa timu hizo ulikuwa kwa mfumo wa kanda na sasa wapo kwenye fainali ili kutafuta mshindi katika ligi hiyo ambayo imehusisha na mamlaka za maji zilizopo Tanzania bara na visiwani”alisema Wambura






DKT.BITEKO MGENI RASMI NISHATI BONANZA 2025

June 27, 2025 Add Comment


📌 *Pamoja na kuimarisha afya za Watumishi; Linalenga kuhamasisha ushiriki wa Uchaguzi Mkuu 2025*


📌 *Ni la pili kufanyika tangu kuasisiwa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko*


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe Dkt Doto Biteko anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika  Bonanza la Wizara ya Nishati na Taasisi zake litakalofanyika jumamosi Juni  28, 2025  jijini Dodoma.

Akizungumzia maandalizi ya Bonanza  hilo, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Nishati, Bi. Neema Mbuja amesema kuwa, Nishati Bonanza litafanyika kwenye Viwanja vya Jamhuri mjini Dodoma na kushirikisha taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati na wadau kutoka Wizara nyingine.

‘’ Nipende kuchukua fursa hii kuzikaribisha taasisi zilizo chini ya  Wizara ya Nishati  kushiriki kikamilifu  bonanza ambalo linaleta fursa ya kufahamiana na kubadilishana mawazo baada ya muda wa kazi pamoja na  kufanya mazoezi ili kujenga afya." Amesema Mbuja

Ameongeza kuwa, kwa  mwaka huu Nishati Bonanza  linaongozwa na kauli mbiu ya "Michezo kwa Afya bora, Shiriki uchaguzi 2025 ikiwa na lengo pia la kuhamasisha wafanyakazi na wananchi kwa ujumla kutumia haki yao ya kikatiba kupiga kura katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 .

Amesema maandalizi yote yameshakamilika na timu zitakazoshiriki michezo mbalimbali zimeshawasili Dodoma kushiriki bonanza hilo litakaloshirikisha watu takribani 1000.

Ametaja michezo itakayoshindaniwa kuwa ni  ni pamoja na Mpira wa miguu, Mpira wa Pete, Mpira wa Wavu, Mpira wa Kikapu, Kuvuta Kamba, pamoja na  michezo ya jadi kama vile bao na drafti, pia   kufukuza kuku.

Taasisi zitakazoshiriki Bonanza hilo la  Nishati ni pamoja na TANESCO, REA, TPDC, PURA, EWURA, TGDC, ETDCO, TCPM, TANOIL, GASCO, PBPA.



Hili ni Bonanza la pili kufanyika tangu kuasisiwa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe.  Dkt Doto Biteko mwaka jana.

DKT.BITEKO MGENI RASMI NISHATI BONANZA 2025

June 27, 2025 Add Comment


📌 *Pamoja na kuimarisha afya za Watumishi; Linalenga kuhamasisha ushiriki wa Uchaguzi Mkuu 2025*


📌 *Ni la pili kufanyika tangu kuasisiwa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko*


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe Dkt Doto Biteko anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika  Bonanza la Wizara ya Nishati na Taasisi zake litakalofanyika jumamosi Juni  28, 2025  jijini Dodoma.


Akizungumzia maandalizi ya Bonanza  hilo, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Nishati, Bi. Neema Mbuja amesema kuwa, Nishati Bonanza litafanyika kwenye Viwanja vya Jamhuri mjini Dodoma na kushirikisha taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati na wadau kutoka Wizara nyingine.


‘’ Nipende kuchukua fursa hii kuzikaribisha taasisi zilizo chini ya  Wizara ya Nishati  kushiriki kikamilifu  bonanza ambalo linaleta fursa ya kufahamiana na kubadilishana mawazo baada ya muda wa kazi pamoja na  kufanya mazoezi ili kujenga afya." Amesema Mbuja


Ameongeza kuwa, kwa  mwaka huu Nishati Bonanza  linaongozwa na kauli mbiu ya "Michezo kwa Afya bora, Shiriki uchaguzi 2025 ikiwa na lengo pia la kuhamasisha wafanyakazi na wananchi kwa ujumla kutumia haki yao ya kikatiba kupiga kura katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 .


Amesema maandalizi yote yameshakamilika na timu zitakazoshiriki michezo mbalimbali zimeshawasili Dodoma kushiriki bonanza hilo litakaloshirikisha watu takribani 1000.

Ametaja michezo itakayoshindaniwa kuwa ni  ni pamoja na Mpira wa miguu, Mpira wa Pete, Mpira wa Wavu, Mpira wa Kikapu, Kuvuta Kamba, pamoja na  michezo ya jadi kama vile bao na drafti, pia   kufukuza kuku.


Taasisi zitakazoshiriki Bonanza hilo la  Nishati ni pamoja na TANESCO, REA, TPDC, PURA, EWURA, TGDC, ETDCO, TCPM, TANOIL, GASCO, PBPA.


Hili ni Bonanza la pili kufanyika tangu kuasisiwa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe.  Dkt Doto Biteko mwaka jana.

CCM TANGA KUSHIRIKIANA NA TFF KUBADILISHA MUONEKANO WA UWANJA WA CCM MKWAKWANI

May 15, 2025 Add Comment

 






Na Oscar Assenga,TANGA

KAMATI ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tanga wamefanya ziara maalumu ya ukaguzi wa uwanja wa CCM Mkwakwani ambao umefanyiwa maboresho makubwa na hivyo unaweza kutumika kwenye mchezo wa nusu fainali wa CRDB Federation Cup kati ya timu ya Yanga na JKT.

Akizungumza mara baada ya kuutembelea uwanja huo,Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tanga Rajab Abdurhaman alisema kwamba uwanja huo kutokana na maboresho makubwa upo tayari kwa ajili ya mchezo huo utacheza Mei 18 mwaka huu.

Alisema kwamba walifanya maboresho makubwa ya uwanja huo sehemu ya kuchezea ambayo ilikuwa na changamoto awali kwa jitihada walizifanya viongozi kwa kushirikiana na TFF kupitia Rais Karia waliwaunga mkono CCM kwa jitihada za kufanya ukarabati wa uwanja wao na TFF kugharamia majani sasa mambo yapo vizuri.

Aidha alisema lakini matarajio yao kwa kushirikiana na TFF wameshaandaa michoro namna ya kuubadilisha muonekano wa uwanja huo uwanja wa Mkwakwani kwa kuweka viti na kutengeneza jukwaa la kisasa.

“Lakini pamoja na hilo pia tutabadilisha muonekano wa vyumba vya kubadilisha nguo,vyoo nk na sasa hivi tumeshakamilisha michoro na tupo kwenye mchakato wa kutafuta wadau ili waweze kutuunga mkono

Hata hivyo alisema kwamba mchezo wa Nusu Fainali hiyo kuchezwa kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani Jijini Tanga ni heshima kubwa kwao na wapo tayari kwa ajili ya mchezo huo.

Mwenyekiti huyo alitoa wito kwa wapenzi wa soka nchini kujitokeza kwa wingi kwenye mchezo huo ili kuweza kuipa sapoti nusu fainali hiyo .

Mwisho.