Showing posts with label michezo. Show all posts
Showing posts with label michezo. Show all posts

DKT.BITEKO MGENI RASMI NISHATI BONANZA 2025

June 27, 2025 Add Comment


📌 *Pamoja na kuimarisha afya za Watumishi; Linalenga kuhamasisha ushiriki wa Uchaguzi Mkuu 2025*


📌 *Ni la pili kufanyika tangu kuasisiwa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko*


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe Dkt Doto Biteko anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika  Bonanza la Wizara ya Nishati na Taasisi zake litakalofanyika jumamosi Juni  28, 2025  jijini Dodoma.

Akizungumzia maandalizi ya Bonanza  hilo, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Nishati, Bi. Neema Mbuja amesema kuwa, Nishati Bonanza litafanyika kwenye Viwanja vya Jamhuri mjini Dodoma na kushirikisha taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati na wadau kutoka Wizara nyingine.

‘’ Nipende kuchukua fursa hii kuzikaribisha taasisi zilizo chini ya  Wizara ya Nishati  kushiriki kikamilifu  bonanza ambalo linaleta fursa ya kufahamiana na kubadilishana mawazo baada ya muda wa kazi pamoja na  kufanya mazoezi ili kujenga afya." Amesema Mbuja

Ameongeza kuwa, kwa  mwaka huu Nishati Bonanza  linaongozwa na kauli mbiu ya "Michezo kwa Afya bora, Shiriki uchaguzi 2025 ikiwa na lengo pia la kuhamasisha wafanyakazi na wananchi kwa ujumla kutumia haki yao ya kikatiba kupiga kura katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 .

Amesema maandalizi yote yameshakamilika na timu zitakazoshiriki michezo mbalimbali zimeshawasili Dodoma kushiriki bonanza hilo litakaloshirikisha watu takribani 1000.

Ametaja michezo itakayoshindaniwa kuwa ni  ni pamoja na Mpira wa miguu, Mpira wa Pete, Mpira wa Wavu, Mpira wa Kikapu, Kuvuta Kamba, pamoja na  michezo ya jadi kama vile bao na drafti, pia   kufukuza kuku.

Taasisi zitakazoshiriki Bonanza hilo la  Nishati ni pamoja na TANESCO, REA, TPDC, PURA, EWURA, TGDC, ETDCO, TCPM, TANOIL, GASCO, PBPA.



Hili ni Bonanza la pili kufanyika tangu kuasisiwa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe.  Dkt Doto Biteko mwaka jana.

DKT.BITEKO MGENI RASMI NISHATI BONANZA 2025

June 27, 2025 Add Comment


📌 *Pamoja na kuimarisha afya za Watumishi; Linalenga kuhamasisha ushiriki wa Uchaguzi Mkuu 2025*


📌 *Ni la pili kufanyika tangu kuasisiwa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko*


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe Dkt Doto Biteko anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika  Bonanza la Wizara ya Nishati na Taasisi zake litakalofanyika jumamosi Juni  28, 2025  jijini Dodoma.


Akizungumzia maandalizi ya Bonanza  hilo, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Nishati, Bi. Neema Mbuja amesema kuwa, Nishati Bonanza litafanyika kwenye Viwanja vya Jamhuri mjini Dodoma na kushirikisha taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati na wadau kutoka Wizara nyingine.


‘’ Nipende kuchukua fursa hii kuzikaribisha taasisi zilizo chini ya  Wizara ya Nishati  kushiriki kikamilifu  bonanza ambalo linaleta fursa ya kufahamiana na kubadilishana mawazo baada ya muda wa kazi pamoja na  kufanya mazoezi ili kujenga afya." Amesema Mbuja


Ameongeza kuwa, kwa  mwaka huu Nishati Bonanza  linaongozwa na kauli mbiu ya "Michezo kwa Afya bora, Shiriki uchaguzi 2025 ikiwa na lengo pia la kuhamasisha wafanyakazi na wananchi kwa ujumla kutumia haki yao ya kikatiba kupiga kura katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 .


Amesema maandalizi yote yameshakamilika na timu zitakazoshiriki michezo mbalimbali zimeshawasili Dodoma kushiriki bonanza hilo litakaloshirikisha watu takribani 1000.

Ametaja michezo itakayoshindaniwa kuwa ni  ni pamoja na Mpira wa miguu, Mpira wa Pete, Mpira wa Wavu, Mpira wa Kikapu, Kuvuta Kamba, pamoja na  michezo ya jadi kama vile bao na drafti, pia   kufukuza kuku.


Taasisi zitakazoshiriki Bonanza hilo la  Nishati ni pamoja na TANESCO, REA, TPDC, PURA, EWURA, TGDC, ETDCO, TCPM, TANOIL, GASCO, PBPA.


Hili ni Bonanza la pili kufanyika tangu kuasisiwa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe.  Dkt Doto Biteko mwaka jana.

CCM TANGA KUSHIRIKIANA NA TFF KUBADILISHA MUONEKANO WA UWANJA WA CCM MKWAKWANI

May 15, 2025 Add Comment

 






Na Oscar Assenga,TANGA

KAMATI ya Siasa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tanga wamefanya ziara maalumu ya ukaguzi wa uwanja wa CCM Mkwakwani ambao umefanyiwa maboresho makubwa na hivyo unaweza kutumika kwenye mchezo wa nusu fainali wa CRDB Federation Cup kati ya timu ya Yanga na JKT.

Akizungumza mara baada ya kuutembelea uwanja huo,Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tanga Rajab Abdurhaman alisema kwamba uwanja huo kutokana na maboresho makubwa upo tayari kwa ajili ya mchezo huo utacheza Mei 18 mwaka huu.

Alisema kwamba walifanya maboresho makubwa ya uwanja huo sehemu ya kuchezea ambayo ilikuwa na changamoto awali kwa jitihada walizifanya viongozi kwa kushirikiana na TFF kupitia Rais Karia waliwaunga mkono CCM kwa jitihada za kufanya ukarabati wa uwanja wao na TFF kugharamia majani sasa mambo yapo vizuri.

Aidha alisema lakini matarajio yao kwa kushirikiana na TFF wameshaandaa michoro namna ya kuubadilisha muonekano wa uwanja huo uwanja wa Mkwakwani kwa kuweka viti na kutengeneza jukwaa la kisasa.

“Lakini pamoja na hilo pia tutabadilisha muonekano wa vyumba vya kubadilisha nguo,vyoo nk na sasa hivi tumeshakamilisha michoro na tupo kwenye mchakato wa kutafuta wadau ili waweze kutuunga mkono

Hata hivyo alisema kwamba mchezo wa Nusu Fainali hiyo kuchezwa kwenye uwanja wa CCM Mkwakwani Jijini Tanga ni heshima kubwa kwao na wapo tayari kwa ajili ya mchezo huo.

Mwenyekiti huyo alitoa wito kwa wapenzi wa soka nchini kujitokeza kwa wingi kwenye mchezo huo ili kuweza kuipa sapoti nusu fainali hiyo .

Mwisho.

TANGA YETU NA BODI YA FILAMU WATOA MAFUNZO KWA WAANDAAJI WA FILAMU MKOANI TANGA

May 05, 2025 Add Comment






Na Oscar Assenga, Tanga

 

Tanga Yetu kupitia mradi wa Fursa kwa Vijana (GOYN TANGA ) kwa kushirikiana na Bodi ya Filamu Tanzania wametoa mafunzo kwa ajili ya utengenezaji wa filamu kwa wasanii mkoani Tanga ili waweze kuwa waandaaji wazuri ambao watafanya vizuri kupitia tasnia hiyo.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo Afisa Maendeleo ya Filamu kutoka Bodi ya Filamu Tanzania Ally Makata kwa niaba ya Serikali alisema kwamba wamekuja Tanga mara ya pili kutoa mafunzo kuhusu utengenezaji wa filamu kwa wasanii wa filamu mkoani Tanga.

Alisema kwamba mafunzo hayo waliyatoa kwa awamu tatu ambapo ya kwanza ilikuwa ni watu wakwenda kufanya utafiti watu wapate wazo kwamba endapo watapata muongozo nani anaweza kucheza na bajeti ya kiasi gani na nani anaweza kufadhili ikiwemo kutengeneza hadithi fupi fupi lazima mdau yoyote kwenye filamu aweza kufanya hivyo ili aweze kufanya vizuri.

 

Aidha alisema kwamba baada ya hapo awamu ya pili na tatu ni kushika Kamera kuona namna kutengeneza mwanga na watu kwenda kwenye maeneo husika na uhariri pamoja na namna ya kupanga na kutengeneza sauti ili uweza kupata picha kamili na viti vyengine.

“Tunawashukuru Tanga Yetu kwa kuweza kufadhili na kushirikiana na Bodi ya Filamu nchini kwa watayarishaji wa Mkoa wa Tanga waweze kupata maarifa kutokana na kwamba Tanga kwa asilimia kubwa  ipo chini na watayarishaji wa Tanga wanalalamika kwenye media wanaoka kazi za mikoa mengine na ikitokea tuzo mikoa mwengine inashika tuzo”Alisema

“Wakati ukiangalia Tanga kuna rasimali za kila kitu ukiangalia mandhara wana sehemu za vivutio wana mazingira mazuri tamaduni wana vyakula tamaduni watu wanaishi kila siku kwanini tusipate Filamu inayoakisi Jamii ya Mkoa wa Tanga “Alisema

Alisema kwamba ukiangalia Marehemu King Majuto ameshaandoka ambaye alikuwa anaiwakilisha vizuri mkoa wa Tanga ikiwemo Marehemu Bauji tunapata stori kulikuwa na waandishi wazuri na waigizaji wazuri lakini sasa haifanyiki hivyo shabaha kubwa ya Dkt Omari na Taasisi ya Tanga Yetu ni kuona namna Tanga inarudi upya.

 

Aliongeza kwamba ukiachana na hayo mafunzo wanaandaa mpango mkakati wa kuona mtayarishaji wa Tanga endapo ataomba Fedha DW na Taasisi mbalimbali ataulizwa historia ya sehemu alipo sasa wakipata mpango mkakati itakuwa rahisi watayarishaji wa mkoa wa Tanga kuchukua mpango mkakati na kuandaa kila wanachokiandaa na kwenda kuombea fedha.

 

Alisema wanawapatia mafunzo na maarifa ili kesho na kesho kutwa waweze kufanya vizuri mkoa wa Tanga ili waweze kufanya vziuri na kurejesha katika hali yake ya kawaida na kung’ara vziuri.

 

Awali akizungumza Mkurugenzi wa HD Consalt Omari Bakari ambao wanatekeleza mradi wa Fursa kwa vijana wa Tanga (GOYN) kupitia program ya Tanga Yetu alisema lengo kubwa ni kuhakikisha vijana wa Jiji la Tanga wanapata fursa ya kuajiriwa au kujiajiri wenyewe.

 

Alisema uchambuzi ambao waliifanya na ofisi ya Taifa ya Takwimu vijana walionekana kutokuea na mahotaji sawa kutokana kila mmoja na uwezo wake na chaguo lake mpango huo wanaoshirikiana na Bodi ya Filamu ni inalenga kusaidia kufikia lengo kwa vijana wale ambao walisema wanapenda kuwa kwenye filamu.

 

Alisema waliamua kushirikiana na Bodi ya Filamu kama Taasisi ya Serikali waliamini kama wana majukumu ya kusimamia,kuhamasisha na kutangaza hiyo sekta kwa hiyo walikubaliana  kuendelea na kusaidia hayo mafunzo yaliyoanza kwenye uzalishaji na wazo kubwa ni kuhakikisha vijana wanapata uzoefu kwenye sekta binafasi ambazo zinashirikiana na bodi ya filamu.

 

“Leo imefikia mwisho wa awamu ya pili na tutaenda kwenye awamu ya tatu kuzalisha filamu ambazo zitakwenda kwenye soko hivyo niwaombe wadau mbalimbali hao vijana wapo vizuri ni kuwaamini na kuwapa kazi ambazo wanaweza kufanya nao wataweza kuwasaidia”Alisema


MNGEZA B BINGWA WA ERASTO CUP MUHEZA,HALMASHAURI KUWAUNGA MKONO MADIWANI WATAKAOANZISHA LIGI KWENYE MAENEO YAO

April 28, 2025 Add Comment


Na Oscar Assenga,MUHEZA.

HALMASHAURI ya wilaya ya Muheza Mkoani Tanga imesema kwamba itaendelea kuwaunga mkono madiwani ambao watakaoanzisha Ligi mbalimbali katika maeneo yao kwa lengo la kuhamasisha michezo na kufungua fursa za ajira kupitia sekta hiyo.



Hayo yalisemwa mwishoni mwa wiki na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Muheza Issa Msumari wakati Fainali ya Ligi ya Erasto Cup ambayo imeanzishwa na Diwani wa Kata ya Tongwe Erasto Mhina ambaye pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri kwa lengo la kuhamasisha vijana kushiriki kwenye michezo.

Msumari ambaye ni Mkuu wa Kitengo cha Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira wilayani Muheza alimpongeza Diwani huyo kwa kuonyesha udhubutu na kupambana kuhakikisha anawapelekea burudani vijana wa Kata hiyo.

Katika mchezo huo wa fainali timu ya Mngeza B iliibuka na ushindi wa penati 5-4 dhidi ya Kwevumo FC katika mchezo ambao ulikuwa na upinzani mkubwa baada ya kutoka sare ya kufungana bao 1-1 katika dakika 90 mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa Pongwe kata ya Tongwe wilayani Muheza.

“Kwa wastani ligi hii imeongeza uchangamfu mkubwa na vijiji 6 na vitongoji 27 kuna badhi ya vijana walikuwa hawatambuani na ligi hiyo hivyo uwepo wake umekuwa chachu ya kuwaleta vijana pamoja na kufahamiana na inakuwa rahisi kuhamasisha mambo ya kijamii”Alisema

Aidha alisema ushiriki wa watu unakuwa ni mkubwa sana ambapo wilaya hiyo wanaunga mkono michezo kwa sababu inatengeneza ajira na kuondoa tatizo la vijana kukaa mtaani bila kazi ya kufanya hivyo wanaipa kipaumbele kama ya vijana watacheza na kutokea kwenye ligi mbalimbali watatengeneza vijana wengi ambao wataitangaza wilaya hiyo kupitia soka.

“Tutaendelea kuunga mkono michezo kwa sababu kupitia huko vijan a wanaweze kutengeneza pesa kama ilivyo kwa vijana wengine waliotokea wilaya ya Muheza Mzize na Semtawa na nieleze kwamba diwani ambayo ataanzisha michezo tutamuunga mkono kutokana na kwamba kupitia michezo inaweza kuwasaidia kuweza kujikwamua kiuchumi wao na jamii “Alisema






CCM TANGA WAMSHUKURU MBUNGE UMMY MWALIMU KWA KUWEKEZA KWA VIJANA KUPITIA MICHEZO

April 14, 2025 Add Comment



Na Oscar Assenga,Tanga. 

Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Tanga, Shabani Hamisi, amemshukuru Mbunge wa Jimbo la Tanga Mjini, Ummy Mwalimu, kwa kuandaa mashindano ya Oddo Ummy Cup kwa kushirikiana na chama cha mpira mkoa wa Tanga (TRFA) akisema kuwa ni hatua muhimu katika kukuza vipaji vya vijana jijini humo.

Akizungumza kama mgeni rasmi kwenye fainali ya mashindano hayo, Hamisi alisema kuwa michezo ni ajira kwa vijana kama zilivyo ajira nyingine, na ni njia mojawapo ya kuimarisha mahusiano na kuwaepusha na vitendo viovu.
"Kwa niaba ya Mheshimiwa Mbunge, nipo hapa kama mgeni rasmi kuhakikisha kuwa mashindano haya yanakuwa chachu kwa vijana katika kujikwamua kiuchumi. Michezo ni ajira, na pia ni njia bora ya kujenga nidhamu na mahusiano bora katika jamii," alisema.
Aidha Alisema kuwa Ummy Mwalimu amekuwa mstari wa mbele kuhakikisha vijana wa Tanga wanashiriki katika michezo mbalimbali na kutumia fursa zinazojitokeza. Alisisitiza kuwa mbunge huyo yuko tayari kushirikiana na vijana katika nyanja tofauti ili kuwawezesha kufikia ndoto zao.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Soka Mkoa wa Tanga (TRFA), Martin Kibua, aliwataka wachezaji na makocha kuzingatia sheria za mchezo, huku akipiga marufuku wachezaji kuhama hama katika timu bila kufuata utaratibu rasmi.
Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Tanga Mjini, Hassan Nyelo, alieleza kuwa ligi ya mwaka huu imekuwa ya kihistoria kutokana na udhamini mkubwa uliotolewa na Mbunge huyo, ikiwa ni mara ya kwanza kwa ligi ya wilaya kupata udhamini wa asilimia 100, ikijumuisha michezo 98 na zawadi zote.
"Mheshimiwa Mbunge amekuwa akiunga mkono jitihada za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, hasa katika sekta ya michezo. Ameahidi kuendeleza juhudi hizi kwa michezo mingine zaidi baada ya mpira wa miguu," aliongeza.
Nyelo alihitimisha kwa kuwaomba vijana na wakazi wa Tanga kuendelea kumuunga mkono Mhe. Oddo Mwalimu kwa juhudi zake za kukuza maendeleo ya vijana kupitia michezo.