Showing posts with label Nishati. Show all posts
Showing posts with label Nishati. Show all posts

DKT.BITEKO ATAKA WATUMISHI WIZARA YA NISHATI NA TAASISI ZAKE KUWA MFANO WA MATUMIZI NISHATI SAFI YA KUPIKIA

August 22, 2025 Add Comment


📌 *Lengo ni kutekeleza Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia kwa vitendo*


*📌Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia yapaa kutoka asilimia 6 hadi 20.3*


📌 *Agawa majiko yanayotumia umeme kidogo kwa Watumishi wa Wizara ya Nishati na REA*


*📌 Apongeza REA  kuhamasisha Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia nchini*


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko, amewataka watumishi katika Wizara ya Nishati na Taasisi zilizochini ya wizara hiyo kuwa mfano katika matumizi ya  Nishati Safi ya kupikia ili kuitekeleza kwa vitendo ajenda iliyoasisiswa na Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan  inayolenga kuhamasisha matumizi ya nishati safi na salama kwa afya


Maelekezo hayo ameyatoa tarehe 22 Agosti 2025 jijini Dodoma  wakati akigawa majiko yanayotumia umeme kidogo kwa watumishi wa Wizara ya Nishati na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ambapo amewataka Watumishi hao  wawe mabalozi katika  kutekeleza ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia.


" Leo tunagawa majiko haya kwa kuwa  nyinyi ndiyo wenye dhamana kuu ya kutekeleza Ajenda ya Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia hivyo wajibu wenu ni mabalozi wazuri kwa watu wanaowazunguka ili nao wahamasike kutumia nishati hii safi." Amesema Dkt. Biteko


Amesema kufuatia mwamko mkubwa unaoendelea sasa kwa wananchi kufahamu faida za matumizi ya nishati safi ya kupikia, kiwango cha watumiaji kimepanda kutoka asilimia 6 na  kufikia asilimia  20.3 huku lengo likiwa ni kufikia asilimia 80 ifikapo 2034.


Dkt. Biteko ametanabaisha kuwa Idadi ya watu wanaoendelea kutumia nishati isiyo safi na salama ya kupikia  bado ni kubwa duniani,  barani Afrika na hapa Tanzania  hivyo ni jukumu la watumishi wote wa Wizara ya Nishati na Taasisi zake  kuhakikisha watanzania wanapata elimu sahihi ili waweze kubadilika na kufikia lengo lililokusudiwa.



Akigawa  majiko 220 kwa watumishi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Dkt. Biteko  amepongeza Taasisi hiyo kwa kuendelea kuhamasisha matumizi ya  nishati safi ya kupikia hususan katika maeneo ya vijijini ambapo kumeonekana kuwa bado changamoto ya kufikiwa na Nishati Safi ya Kupikia.

Pia ameipongeza REA kwa kuhakikisha  Vijiji vyote 12,318 nchini vinafikiwa na umeme.



Kwa Upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati Mhandisi Felchesmi Mramba amemhakikisha  Dkt. Biteko kuwa atakahikisha agizo alilolitoa linatekezwa na Taasisi zote anazozisimamia.



Amesema  atahakikisha kwamba  Ajenda ya Nishati Safi ya Kupikia yanafikia malengo yaliyokusudiwa.


Amewasisitiza watumishi kutumia Majiko hayo waliyopewa na si kuyahifadhi.

AGIZO LA DKT.BITEKO LA MINADA YOTE NCHINI KUTUMIA NISHATI SAFI YA KUPIKIA LAANZA KUTEKELEZWA

August 21, 2025 Add Comment

📌 Wachoma nyama na Mama Lishe katika mnada wa Msalato Dodoma waanza kuonja matunda ya Nishati Safi ya Kupikia


📌 Dkt. Biteko asema ni matunda ya Rais, Dkt. Samia ambaye anayefahamu machungu ya kutumia Nishati isiyo safi ya Kupikia


📌 Atoa maagizo kwa Mkurugenzi Jiji la Dodoma kuweka miundombinu itakayohakikisha majiko ya Nishati Safi ya Kupikia ya Wachoma nyama yanakuwa salama


📌 Apongeza REA, Wizara ya Nishati kutekeleza agizo alilolitoa: STAMICO yatakiwa kuweka kituo cha kudumu cha mkaa mbadala Mnada wa Msalato


📌 Kituo kikubwa cha kusambaza umeme na kusimamia gridi ya Taifa kujengwa Dodoma


Agizo la Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko alilolitoa kwa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kuhakikisha kuwa minada yote nchini inakuwa na miundombinu itakayowawezesha Wachoma nyama, Mama Lishe na Baba Lishe kutumia nishati Safi ya Kupikia limeanza kufanyiwa kazi ikiwa ni utekelezaji wa ajenda ya Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha wananchi wote wanatumia Nishati iliyosafi ya kupikia.


Safari hiyo ya kuhakikisha minada yote nchini inatumia nishati safi ya kupikia, imeanzia katika Mnada wa Msalato jijini Dodoma ambapo tarehe 21 Agosti 2025, Dkt. Biteko amegawa majiko banifu kwa Mamalishe takriban 27 wanaohudumu katika mnada huo pamoja na majiko ya kuchomea nyama.

“Kama mnavyofahamu, Mhe. Rais alitoa maelekezo kuwa watanzania asilimia 80 ifikapo 2034 watumie nishati safi ya kupikia, maelekezo yake yanaendelea kutekelezwa, tulianza na taasisi zinazolisha watu zaidi ya 100  kuondoa matumizi ya kuni na mkaa ikiwemo  magereza yote nchini, shule za Sekondari , vyuo na taasisi nyinginezo lakini moja ya maeneo yaliyobaki ni pamoja na minada ambayo inahudumia watu wengi.” Amesema Dkt.Biteko

Dkt. Biteko ameeleza kuwa kazi ya kufunga mifumo ya Nishati Safi ya Kupikia kwenye minada ilianza na utafiti ili kupata hali halisi ya matumizi ya nishati hiyo ambapo katika utafiti huo, asilimia 89.5 ya wachoma nyama wote walisema hawana uelewa wowote kuhusu nishati safi ya kupikia, pia utafiti huo umeonesha asilimia 26.3 ya wachoma nyama wamewahi kutumia nishati safi ya kupikia na asilimia iliyobaki haijawahi kutumia. Hii ikionesha kuwa bado kuna kazi ya kufanya kuelekea kwenye matumizi ya Nishati Safi ya kupikia.

Amesisitiza kuwa, hatua hizo zinazochukuliwa na Serikali katika  Nishati Safi ya Kupikia, ni matunda ya Mhe. Rais, Dkt.Samia Suluhu Hassan ambaye amejipambanua kama kama kiongozi mwanamke anayejua machungu ya matumizi ya nishati isiyo safi na wakati wote anaelekeza kuwa yeye anachotaka kuona  ni watu wengi hawatumii nishati isiyo safi ya kupikia. 

Ameongeza kuwa, Tanzania ndiyo nchi pekee barani Afrika ambayo imezindua Mkakati wa Taifa wa matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia ambao umekuwa ni mfano barani Afrika na nchi nyingine zinakuja kujifunza hivyo lazima iwe mfano na kinara  kwa kuishi yale inayoyasema.

Katika hatua nyingine, Dkt. Biteko amemuagiza Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma kuweka miundombinu ambayo itafanya majiko ya nishati safi ya kupikia katika minada  mkoani Dodoma kuwa katika sehemu ya kudumu na zoezi hilo lianze mara moja.


Aidha, ameliagiza Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) kuweka kituo cha kudumu cha kuuza mkaa mbadala katika mnada wa Msalato ili wananchi wasikwame pale wanapohitaji nishati hiyo.


Vilevile ameitaka REA, kuhakikisha majiko makubwa ya kuchomea nyama ambayo yanatumia Nishati Safi ya Kupikia yanapatikana ili wananchi wanaochoma nyama na wanaofuata huduma wasipoate madhara ya afya kuanzia sasa kwenda mbele.

Dkt. Biteko ameipongeza REA na Watendaji wa Wizara ya Nishati  kwa kupoeka agizo lake kwa haraka na kulifanyia kazi, pia amewaasa kuendelea na ubunifu utakaowawezesha wananchi kutumia nishati safi ya kupikia na wasisahau kufanya tathmini ya matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia katika minada hiyo.

Pia, amewaasa Mama lishe na Baba lishe kuiunga mkono ajenda ta nishati safi ya kupikia na kuwa mabalozi wa nishati hiyo kwani watu wakiona faida zinazotokana na kutumia nishati safi ya kupikia  kutoka kwao nao watavutika kuitumia. 

katika hafla hiyo,  Dkt. Biteko amemshukuru Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kufanya kazi kubwa ya mfano katika sekta ya Nishati ambapo amesema Mkoa wa Dodoma  muda si mrefu utakuwa ni kitovu cha usambazaji umeme katika mikoa mbalimbali ikiwemo Singida, Shinyanga, Tabora, Kigoma na Arusha na  pia kitajengwa  kituo kikubwa cha kusambaza umeme na kusimamia gridi ya Taifa.


Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule kwa upande wake amesema walaji katika mnada wa Msalato  kwa wiki ni kati ya 2000 na 3000 hivyo kwa kutumia Nishati Safi ya Kupikia itawezesha kuokoa mazingira kwa kuondokana na kuni na mkaa ambao ulikuwa ukitumika kuhudumia idadi hiyo ya watu. 

Aidha ameomba a kampeni hiyo ya Nishati Safi ya Kupikia ifike kwenye masoko mbalimbali ambayo ina mama lishe na baba lishe.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba yeye amemshukuru Dkt. Biteko kwa maono yake ambayo yamewezesha Mnada wa Msalato kufikiwa na Nishati Safi ya Kupikia ikiwa ni mwanzo wa kusogeza huduma kwenye minada mingine.

Ameeleza kuwa kiwango cha matumizi ya nishati safi ya kupikia kimepanda kutoka asilimia 6.9  ya mwaka 2022 na hadi kufikia asilimia 20.3 na kusema kuwa kwa jinsi matumizi ya nishatil safi ya kupikia yanavyoongezeka Serikali itatimiza lengo lake ya kufikisha Nishati Safi ya Kupikia kwa watanzania wapatao asilimia 80 kama alivyoagiza Mhe.Rais.

Naye, Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amesema amesema katika mnada wa Msalato kuna wachoma nyama kati ya 45 na 50 ambao watapatiwa majiko makubwa ya kuchomea nyama, pia kuna mama lishe 27  ambao tayari wote wamepatiwa majiko banifu.

Mwenyekiti wa Wachoma nyama katika Mnada wa Msalato, Mathias Raphael  amesema baada ya kupata elimu ya nishati safi ya kupikia katika mnada huo  ameanza kutumia jiko linalotumia mkaa mbadala ambao amesema kuwa unatumika kidogo huku ukichoma nyama nyingi, unakaa muda mrefu na hauna moshi.


Mwisho

REA KUSAMBAZA MAJIKO BANIFU 10650 MKOANI PWANI

August 18, 2025 Add Comment


*📌RC Kunenge aipongeza REA kwa kuhamasisha matumizi nishati safi*


*📌Mifumo ya umeme jua kuchochea upatikanaji wa umeme

kwa asilimia 100 ifikapo mwaka 2030*


📍Pwani


Wakala wa Nishati Vijijini (REA), imetoa jumla ya Majiko Banifu 10,650 Mkoani Pwani ikiwa ni mwendelezo wa jitihada za Serikali za kuhakikisha  kila mwananchi anatumia Nishati Safi ya kupikia nchini. 


Akizungumza leo tarehe 18 Agosti, 2025 ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Meneja wa Teknolojia za Nishati kutoka REA, Mha. Michael Kyessi amesema mradi huo unalenga kuuza na kusambaza Majiko Banifu kwa bei ya ruzuku ambapo mwananchi atachangia asilimia ishirini (20%) za gharama ya jiko huku asilimia themanini (80%) zikitolewa na Serikali. 

“Mwananchi wa kawaida atachangia 20% tu za gharama za jiko ambapo bei ya jiko ni 56,000 na mwananchi atagharamika kuchangia shilingi 11,200 tu baada ya ruzuku kutolewa na Serikali” amesema Mha. Kyessi. 



Sambamba na hilo Mha. Kyessi amebainisha thamani ya mradi huo kwa ujumla ni milioni 596,400,00 ambapo Serikali kupitia REA imetoa ruzuku ya shilingi milioni 477,120,00 ambayo ni sawa na asilimia themanini. 

Katika hatua nyingine, REA inatekeleza lengo la Serikali ya Tanzania kufikia mpango wa Umoja wa Mataifa wa "Nishati Endelevu kwa Wote" (SE4ALL) wa upatikanaji wa nishati 

kwa asilimia 100 ifikapo mwaka 2030. Mradi huu utatumia nishati Jadidifu ili kuweza kufikia wananchi wa maeneo ya visiwani na utekelezaji wake ni kwa kupitia mradi wa Ufadhili unaotegemea Matokeo (RBF) kupitia Benki ya Dunia. 

"Serikali ya Tanzania kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umetenga fedha kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa kufunga mifumo ya umeme jua maeneo ya visiwani kwa 

kutoa ruzuku kwa bei ya mwisho ya mtumiaji wa mfumo wa Umeme Jua ili kufanikisha upatikanaji wa umeme katika maeneo hayo yaliyo mbali na Gridi ya Taifa, " Amesema Mha. Kyessi. 

Mha. Kyessi amesema katika Mkoa wa Pwani mradi wa umeme jua unategemea kuhudumia visiwa 13 na jumla ya watoa huduma wawili (2) wanategemea kuhudumia visiwa hivyo kupeleka jumla ya mifumo 2,243 ndani ya kipindi cha miaka miwili (2) na gharama za mradi kwa mkoa wa Pwani ni shilingi  bilioni 1.372 ambapo ruzuku ni shilingi milioni 935.7 sawa na asilimia 69 ya gharama zote ya mradi na shilingi milioni 436.6 ni fedha toka kwa wanufaika. 

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Abubakar Kunenge ameipongeza REA kwa mkakati wa kuendelea kuongeza matumizi ya Nishati safi na kuondoa kero kwa wananchi kuhusu matumizi ya kuni na mkaa ambayo ni hatarishi kwa afya zao. 

 

Mradi huo utatekelezwa kwa muda wa miezi 15 katika mkoa wa Pwani na jumla ya Majiko Banifu 10,650 yatasambazwa kwa wananchi.

WANANCHI WAKARIBISHWA NANENANE KUFAHAMU KWA KINA MPANGO MAHSUSI WA NISHATI 2025-2030

WANANCHI WAKARIBISHWA NANENANE KUFAHAMU KWA KINA MPANGO MAHSUSI WA NISHATI 2025-2030

August 05, 2025 Add Comment


*Ni uliosainiwa katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika wa Misheni 300*

Wizara ya Nishati imekaribisha wananchi kuendelea kutembelea Banda la Wizara ya Nishati katika Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima- NANENANE jijini Dodoma ili kufahamu masuala mbalimbali ikiwemo Mpango mahsusi wa Taifa wa Nishati wa mwaka 2025-2030.

Imeelezwa kuwa mpango huo uliosainiwa katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika wa Misheni 300 mwezi Januari 2025 unalenga kuunganisha umeme kwa wananchi milioni 8.3 ifikapo 2030 na kufikisha nishati safi ya kupikia kwa asilimia 75 ya Watanzania ifikapo 2030.

Mpango huo pia unalengai kiwemo kuongeza upatikanaji wa umeme na kuongeza ushiriki wa nishati jadidifu katika uzalishaji wa umeme.

WANANCHI WAKARIBISHWA BANDA LA WIZARA YA NISHATI NANENANE DODIMA

August 04, 2025 Add Comment


*📌 Kufahamu fursa na miradi inayoendelea kutekelezwa*



Wizara ya Nishati imeendelea kukaribisha wananchi kutembelea Banda la Wizara ya Nishati  katika Maonesho ya Kimataifa ya Wakulima (NANENANE) yanayoendelea katika Viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma.

 Fredrick Marwa, Mjiolojia kutoka Wizara ya Nishati amesema katika maonesho hayo Wizara inaeleza kuhusu  kazi mbalimbal zinaoendelea kufanyika ikiwemo za  utafutaji na uchimbaji wa mafuta na gesi katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo Bonde la Eyasi Wembere.

Marwa amesema wananchi watakapofika katika Banda la Wizara ya Nishati pia watajionea mafanikio mbalimbali yaliyofikiwa na Wizara  pamoja na Taasisi zake ikiwemo TANESCO, EWURA, REA na TPDC.

Rais Samia Suluhu Hassan Kinara wa Nishati Safi ya kupikia Duniani , aungwe Mkono - Sangweni

July 11, 2025 Add Comment

WhatsApp%20Image%202025-07-11%20at%2009.41.55


WhatsApp%20Image%202025-07-11%20at%2009.41.54%20(2)

WhatsApp%20Image%202025-07-11%20at%2009.41.54%20(1)

WhatsApp%20Image%202025-07-11%20at%2009.41.54

WhatsApp%20Image%202025-07-11%20at%2009.41.53



  • Apongeza kasi ya Dkt. Biteko na Uongozi Menejimenti ya Nishati katika kufanikisha Kampeni ya Nishati Safi ya Kupikia.
  • Amesifu juhudi za TANESCO  na REA katika kutekeleza  Kampeni ya Nishati Safi ya Kupikia.
  • Atoa Rai kwa Watanzania kuhamia kwenye Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia


Na Mwandishi Wetu,


Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) Mh. Charles Sangweni ametoa Rai kwa Wananchi wote kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mhe. Dkt. Samia Suhuhu Hassan katika Kampeni ya Kitaifa  ya kuhamia kwenye Nishati Safi ya Kupikia.

Rai hiyo imetolewa tarehe 09 Julai, 2025  na Mhe. Charles Sangweni alipotembelea Banda la TANESCO  katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar-es-Salaam yanayoendelea jijini Dar-es-Salaam.

Amesema Tanzania tuna bahati kuwa, Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jemedari Mkuu wa Majeshi ya nchi yetu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa ndiye Kinara wa Kampeni ya Nishati Safi ya Kupikia Duniani.

Amesema, Wizara ya Nishati na Watanzania wote kiujumla, ni muhimu tuunge mkono juhudi zinazofanywa na Rais wetu katika kuhakikisha Watanzania wanahamia katika Nishati Safi ya Kupikia kwanza kwa  kuhakikisha tunapokea na tunaendana na Kauli Mbiu ya Nishati Safi ya Kupikia na kuunga mkono jitihada alizozianzisha.

Amesema, "kama Watendaji, tumefurahi kuona, wenzetu wa TANESCO wameunga Mkono juhudi za Mheshimiwa Rais kwa kuja na kampeni ya kuhamasisha  matumizi ya vyombo mbadala vya umeme vinavyotumia umeme kidogo na ambavyo vinahakikisha Nishati inayotumika kwa ngazi ya kawaida kabisa majumbani inakuwa ni  Nishati Safi." Ameeleza kwa hisia za kuvutiwa na hatua hiyo Mha. Sangweni.

Mha. Sangweni ameeleza zaidi kuwa, katika kutembelea Banda la TANESCO, ameona vitu vingi, ikianzia kwa REA  Usambazaji wa Umeme unavyofanyika kwa kasi na hii inaonyesha kuunga mkono Juhudi za Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na Viongozi wengine wa Wizara akiwemo  Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Doto Mashaka Biteko

Pia, Mha. Sangweni amesema vilevile katika Banda la TANESCO amekuta Wadau wanauza majiko ya umeme yanayotumia Nishati ya umeme kidogo sana ikilinganishwa na majiko mengine ya kawaida.

Mkurugenzi Mkuu wa PURA ameeleza  kufurahishwa kwake zaidi na  majiko hayo yanayotumia mfumo wa sumaku kupitisha moto  kuwa na mfumo wa ku-sence  pale ambapo sufuria haiko jikoni na namna yanavyopunguza kabisa upotevu wa umeme ambao hautumiki.

"Tumeona kwamba, usipoweka sufuria basi hakuna moto ambao unatoka na wakati mwingine ukiwa umejisahau, kunakuwa na timer ambayo inaweza ikazima jiko kulingana na jinsi ulivyo- set." Amesema Mha. Sangweni.

Amefafanua kuwa, hiyo yote ni katika kuhakikisha kwamba bili iliyokuwa inakuja kwa kiasi kikubwa ambayo ilikuwa inakuja kutokana na majiko ambayo hayana control kama hizo, inaenda kupungua kwa kiasi kikubwa sana.

"Hatua hiyo itatufanya sisi ambao vipato vyetu sio vikubwa kuona kuwa kutumia umeme sio anasa tena bali ni Matumizi Bora Kabisa ya Nishati ambayo iko safi na inayofaa kwa matumizi na ulinzi wa mazingira kama ambavyo Viongozi wetu wa nchi wamekuwa wakituhimiza na kusisitiza ili kama nchi tuingie kwenye Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia." Amesema Mha. Sangweni.