Showing posts with label siasa. Show all posts
Showing posts with label siasa. Show all posts

HAMADI –NITAFANYA KAZI KWA UADILIFU KUHAKIKISHA WANANCHI WANAPATA MAENDELEO

August 18, 2025 Add Comment


KADA ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Hamadi Shamisi Hamadi leo amechukua fomu ya kuwania Udiwani Kata ya Msambweni Jijini Tanga huku akihaidi kufanya kazi kwa uadilifu.

Hamadi aliyasema hayo leo mara baada ya kuchukua fomu katika Ofisi ya Mtendaji Kata ya Msambweni huku akiwa amesindikizwa na wanachama wa chama hicho wakiwemo wananchi.

Alisema kwamba lengo lake ni kuhakikisha anawatumikia wananchi wa kata hiyo na kuwa kiungo cha maendeleo ya wananchi na hivyo kuchochea ukuaji wa maendeleo.

“Nawaambia tutafanya kazi kwa dhati na kutanguliza uaminifu na uadilifu kuhakikisha wananchi wanapata maendeleo na shahidi ni Baba yangu mzazi ambaye ananisindikiza hapa”Alisema

Awali akizungumza Mwenyekiti wa CCM kata ya Msambweni alisema kwamba hicho ni kishindo cha kwanza ila Agosti 28 wanaanza kampeni zao na wanafungua kwenye tawi la Msambweni B eneo la Komesho watakuwa na Mbunge wa Tanga Jijini kampeni za wilaya zitafunguliwa hapo.

Alisema Agosti 29 utakuwa uzinduzi wa kampeni wa Diwani wa Kata ya Msambweni na zitazinduliwa Mtaa wa Madina eneo la Mabanda ya Papa huku akiwataka wananchi kujitokeza kwa wingi katika uzinduzi huo.

Naye kwa upande wake Mwenyekiti wa zamani wa Mtaa wa Madina Godfrey Mazimu alisema kwamba amefurahi kuona wanachama wenzake na wananchi wa Msambweni huku akiwataka kuendelea kuunganisha nguvu za pamoja mpaka mwisho na wasiachane.


MGOMBEA NCCR MAGEUZI AJITOKEZA KUCHUKUA FOMU ZA UTEUZI

August 15, 2025 Add Comment

 

Mgombea wa Kiti cha Rais kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya Chama cha National Convention for Construction and Reform – Mageuzi (NCCR-MAGEUZI), Mhe. Haji Ambar Khamis akiwa na Mgombea Mwenza, Mhe. Dkt. Eveline Wilbard Munisi wakionesha begi la fomu za uteuzi baada ya kukabidhiwa na Tume leo Agosti 15,2025.
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa Jacobs Mwambegele akimkakabidhi mkoba wenye fomu za kuomba kuteuliwa kuwa Mgombea wa Kiti cha Rais na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya Chama cha National Convention for Construction and Reform – Mageuzi (NCCR-MAGEUZI), Mhe. Haji Ambar Khamis. Mgombea huyo waaliambatana na Mgombea Mwenza, Mhe. Dkt. Eveline Wilbard Munisi (kushoto) alichukua fomu hizo leo Agosti 15, 2025 ambapo Tume inataraji kufanya uteuzi Agosti 27 mwaka huu. (Picha na INEC).
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa Jacobs Mwambegele akimkakabidhi mkoba wenye fomu za kuomba kuteuliwa kuwa Mgombea wa Kiti cha Rais na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya Chama cha National Convention for Construction and Reform – Mageuzi (NCCR-MAGEUZI), Mhe. Haji Ambar Khamis. Mgombea huyo waaliambatana na Mgombea Mwenza, Mhe. Dkt. Eveline Wilbard Munisi (kushoto) alichukua fomu hizo leo Agosti 15, 2025 ambapo Tume inataraji kufanya uteuzi Agosti 27 mwaka huu. Kulia ni Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume, Ndg. Ramadhan Kailima. (Picha na INEC).

SWAUMU WA UDP ACHUKUA FOMU INEC KUWANIA KITI CHA RAIS KATIKA UCHAGUZI MKUU 2025

August 15, 2025 Add Comment

 


Mgombea wa Kiti cha Rais kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya Chama cha United Democratic Party (UDP), Mhe. Saum Hussein Rashid akiwa na Mgombea Mwenza, Mhe. Juma Khamis Faki (kushoto) wakionesha beki la fomu za uteuzi walililokabidhiwa na Tume.
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa Jacobs Mwambegele akimkakabidhi mkoba wenye fomu za kuomba kuteuliwa kuwa Mgombea wa Kiti cha Rais na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya Chama cha United Democratic Party (UDP), Mhe. Saum Hussein Rashid. Mgombea huyo waaliambatana na Mgombea Mwenza, Mhe. Juma Khamis Faki (kushoto) alichukua fomu hizo leo Agosti 15, 2025 ambapo Tume inataraji kufanya uteuzi Agosti 27 mwaka huu. Kulia ni Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume, Ndg. Ramadhan Kailima.  (Picha na INEC).



Mgombea wa Kiti cha Rais kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya Chama cha United Democratic Party (UDP), Mhe. Saum Hussein Rashid akielekezwa na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa INEC, Ndg Ramadhani Kailima namna ya kusaini kitabu.

Mgombea wa Kiti cha Rais kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya Chama cha United Democratic Party (UDP), Mhe. Saum Hussein Rashid akielekezwa na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa INEC, Ndg Ramadhani Kailima namna ya kusaini kitabu.
Mgombea wa Kiti cha Rais kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya Chama cha United Democratic Party (UDP), Mhe. Saum Hussein Rashid akisaini kitabu.

Mgombea Mwenza, Mhe. Juma Khamis Faki akisaini kitabu.

Wajumbe wa Tume wakiwa katika utoaji fomu.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa INEC, Ndg. Ramadhani Kailima akizungumza wakati wa utoaji fomu za uteuzi kwa wagombea wa Chama cha UDP.
Wagombea wa Chama cha UDP wakiwa ukumbini.
Baadhi ya wanachama wa UDP wakiwa katika ukumbi wa utoaji fomu.

Baadhi ya wanachama wa UDP wakiwa katika ukumbi wa utoaji fomu.
Baadhi ya wanachama wa UDP wakiwa katika ukumbi wa utoaji fomu. 

Baadhi ya wanachama wa UDP wakiwa katika ukumbi wa utoaji fomu. 



Mgombea wa UDP akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukabidhiwa fomu.

MGOMBEA ADC ACHUKUA FOMU ZA UTEUZI

August 14, 2025 Add Comment

 

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa Jacobs Mwambegele akimkakabidhi mkoba wenye fomu za kuomba kuteuliwa kuwa Mgombea wa Kiti cha Rais na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC), Mhe. Wilson Elias Mulumbe. Mgombea huyo waaliambatana na Mgombea Mwenza, Mhe. Shoka Khamis Juma (kushoto) alichukua fomu hizo leo Agosti 14, 2025 ambapo Tume inataraji kufanya uteuzi Agosti 27 mwaka huu. (Picha na INEC).
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa Jacobs Mwambegele akimkakabidhi mkoba wenye fomu za kuomba kuteuliwa kuwa Mgombea wa Kiti cha Rais na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC), Mhe. Wilson Elias Mulumbe. Mgombea huyo waaliambatana na Mgombea Mwenza, Mhe. Shoka Khamis Juma (kushoto) alichukua fomu hizo leo Agosti 14, 2025 ambapo Tume inataraji kufanya uteuzi Agosti 27 mwaka huu. Kulia ni Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume, Ndg. Ramadhan Kailima.  (Picha na INEC).

NEEMA LUGANGIRA ATEULIWA BRUSSELS

August 13, 2025 Add Comment

 ** 


Aliyekuwa Mbunge Viti Maalum, Neema Lugangira amenza kazi jijini Brussels kama Katibu Mkuu wa Women Political Leaders (WPL) — Jumuiya ya Kimataifa ya Viongozi Wanawake: Marais, Makamu wa Rais, Mawaziri Wakuu, Mawaziri, Wabunge na Mameya/Wenyeviti wa Halmashauri; ambapo wanalenga kuongeza uwakilishi wa wanawake katika siasa na kuimarisha sauti, ushawishi na aina ya uongozi wao katika nyanja na sekta mbalimbali. #UongoziUnaopimika

CUF WAMTUMA GOMBO KUCHUKUA FOMU ZA UTEUZI INEC KUWANIA KITI CHA RAIS UCHAGUZI MKUU 2025

August 13, 2025 Add Comment

 

Mgombea wa Kiti cha Rais kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya Chama cha Wananchi (CUF), Mhe. Gombo Samandito Gombo na Mgombea Mwenza, Mhe. Husna Mohamed Abdalla wakionesha mkoba wa fomu baada ya kukabidhiwa na Tume leo Agosti 13, 2025.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa Jacobs Mwambegele akimkakabidhi mkoba wenye fomu za kuomba kuteuliwa kuwa Mgombea wa Kiti cha Rais na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya Chama cha Wananchi (CUF), Mhe. Gombo Samandito Gombo. Mgombea huyo waaliambatana na Mgombea Mwenza, Mhe. Husna Mohamed Abdalla (kushoto) alichukua fomu hizo leo Agosti 13, 2025 ambapo Tume inataraji kufanya uteuzi Agosti 27 mwaka huu. Kulia ni Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume, Ndg. Ramadhan Kailima.  (Picha na INEC).
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa Jacobs Mwambegele akimkakabidhi mkoba wenye fomu za kuomba kuteuliwa kuwa Mgombea wa Kiti cha Rais na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia tiketi ya Chama cha Wananchi (CUF), Mhe. Gombo Samandito Gombo. Mgombea huyo waaliambatana na Mgombea Mwenza, Mhe. Husna Mohamed Abdalla (kushoto) alichukua fomu hizo leo Agosti 13, 2025 ambapo Tume inataraji kufanya uteuzi Agosti 27 mwaka huu. 
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume, Ndg. Ramadhani Kailima akimuelekeza namna ya kujaza kitabu Mgombea wa kiti cha Rais kutoka Chama cha Wananchi (CUF), Mhe. Gombo Samandito Gombo.
Mgombea wa kiti cha Rais kutoka Chama cha Wananchi (CUF), Mhe. Gombo Samandito Gombo akijaza kitabu kuonesha amekabidhiwa fomu hizo. 
Mgombea Mwenza, Mhe. Husna Mohamed Abdalla akaisaini kitabu.
Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa Jacobs Mwambegele  akizungumza.
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume, Ndg. Kailima Ramadhani akizungumza wakati wa utoaji huo wa fomu.

Mgombea wa kiti cha Rais kutoka Chama cha Wananchi (CUF), Mhe. Gombo Samandito Gombo.
Mgombea Mwenza, Mhe. Husna Mohamed Abdalla.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa Jacobs Mwambegele  akizungumza.

Wanachama wa CUF wakiwa ukumbini kushuhudia utoaji wa fomu za uteuzi kwa wagombea wa chama chao.



DP WAIBUKA NA SERA YA KUBORESHA KANUNI ZA KIKOKOTOO ENDAPO WATAPATA RIDHAA YA KUONGOZA NCHI

August 13, 2025 Add Comment


MGOMBEA Urais kupitia tiketi ya Chama Cha Siasa cha Democratic Party (DP),Abdul Mluya,amesema endapo chama hicho kitapata nafasi ya kuongoza Nchi moja ya kipaumbele chao ni kwenda kusimamia suala la Kikokotoo.

Mluya ambaye aliambatana na mgombea mwenza Saodun Abraham Khatibu ameyazungumza hayo mbele ya waandishi wa habari mara baada ya kuchukua fomu ya kuwania nafasi hiyo katika ofisi za Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi iliopo jijini Dodoma.

Amesema suala la Kikokotoo kwa watumishi imekuwa changamoto kubwa sana kwa watumishi hivyo DP inakwenda kulifanyia kazi suala hilo ili watumishi waweze kupata mafao yao bila changamoto yeyote

"Tunakwenda kufuta kilio cha Kikokotoo kwa watumishi,haiwezekani mtu afanye kazi ndani ya miaka 33 halafu alipwe mafao sh milioni 13 hadi 14 hilo tunakwenda kuliondoa,"amesema Mluya.

Amesema serikali ya DP itakwenda kuwajengea nyumba watumishi ambao wamekaa ofisini zaidi ya mwaka bila kashfa ya kosa lolote lile ili kusaidia kuondoa rushwa katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

Mbali na hayo pia amesema DP itashughulikia na kuboresha maslahi ya Jeshi la Magereza pamoja na majeshi mengine ili kuhakikisha wanafanya kazi katika mazingira bora na kuongeza kuwa wataboresha pia suala zima la Magereza ya wafungwa hapa nchini.

Mluya amesema vipaumbele vingine kwao ni suala la Afya,ambapo kinamama watajifungua bure na mtoto atapewa lishe kwa miezi mitatu huku akisema marehemu hatadaiwa hela ya matibabu,ndugu watapewa mwili ili wakazike na kwenye kilimo watahimiza kilimo cha umwagiliaji.