Showing posts with label siasa. Show all posts
Showing posts with label siasa. Show all posts

KADA WA CCM MACRINA AJITOSA UBUNGE VITI MAALUMU MKOA WA TANGA

June 29, 2025 Add Comment

 

KADA wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Tanga Macrina Clemens (kulia ) akikabidhiwa fomu na Katibu wa UWT Mkoa wa Tanga Anastazia Aman

Na Mwandishi Wetu,TANGA.

KADA wa Chama cha Mapinduzi CCM Mkoa wa Tanga Macrina Clemens amechukua fomu ya kuomba ridhaa ya kuteuliwa kugombea Ubunge wa viti Maalumu Mkoa huku akihaidi kushirikiana na wananchi katika kuleta maendeleo.

Akizungumza mara baada ya kuchukua fomu alisema ameamua kuchukua fomu ili kuweza kutoa mchango wake kwa wananchi hususani Jumuiya wa Wanawake wa Chama cha Mapinduzi  (UWT) Mkoa wa Tanga.

Zoezi la kuchukua fomu limeanza katika ofisi za Chama cha Mapinduzi linaendelea nchi nzima ambapo watia nia tofauti wameendelea kujitokeza kwa ajili ya kuchukua fomu za Ubunge na Udiwani.




DKT.BITEKO AWAASA CCM BUKOMBE KUDUMISHA AMANI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU

June 14, 2025 Add Comment


📌 Azindua maduka ya kisasa 31 Ushirombo


Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa,  Mbunge wa Jimbo la Bukombe, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko amewaasa wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Jimbo la Bukombe wasikubali kuvutana na kugombana bali wadumishe amani, kuendelea kuheshimiana na kulinda utu wao hususan katika kipindi cha kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Rais, wabunge na madiwani.

Dkt. Biteko amesema hayo Juni 14, 2025 wilayani Bukombe, mkoani Geita mara baada ya kuzindua maduka 31 ya kisasa yaliyopo katika eneo la Ofisi za CCM wilayani humo.

“Naomba niwakumbushe tena kwa sasa tunaukaribia mwezi wa Oktoba, 2025. Tunakaribia kuingia katika zoezi la Uchanguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani, niwaombe tu kwamba, zoezi la uchaguzi ni zoezi la mara moja, lakini maisha yetu sisi yanadumu na yataendelea kudumu na kuna maisha baada ya kampeni na baada ya Uchanguzi. Hivyo, kwa heshima, nawaomba tuendelee kudumisha umoja, upendo na undugu uliopo baina yetu,” amesema Dkt. Biteko.


Katika hatua nyingine, amezungumzia ujenzi wa maduka hayo ya kisasa kuwa ni hatua kubwa kwa maendeleo ya wananchi wa eneo hilo la Ushirombo na maeneo mengine ya jirani kwa kuwa ni chanzo cha maendeleo na mzunguko wa fedha katika eneo hilo.

Amesisitiza “ Maduka haya yataongeza mvuto na hivyo kuongeza thamani ya eneo hili la ardhi pamoja na thamani ya jengo. Ukuaji wa eneo letu hili huchangiwa zaidi na shughuli za madini na shughuli nyingine za kiuchumi. Taarifa zinaonesha kuwa, Mkoa wa Geita umeonesha kasi kubwa zaidi ya ukuaji kutokana na shughuli za madini, na watu wanaochimba watapata huduma kwenye hili,”

Aidha, amewapongeza na kuwashukuru Mwenyekiti na Katibu wa CCM Wilaya ya Bukombe na Madiwani 23 kwa ushirikiano wao na kusema kuwa wamefanya kazi kubwa ya kuchangia ujenzi wa maduka hayo na kusema kuwa anafurahishwa kufanya kazi nao akiongeza kuwa wajumbe wa kata wanazotoka wanaweza kuwapima kwa kazi walizofanya. 

Dkt. Biteko amesema kuwa CCM katika wilaya hiyo itaendelea kuunga mkono mawazo mapya yatakayotolewa kwa ajili ya kusaidia maendeleo ambapo ametaja baadhi ya miradi ya ujenzi wa soko, stendi na barabara inayoendelea kujengwa wilayani humo inalenga kukuza uchumi wa wilaya na mkoa kwa ujumla.

Vilevile, Dkt. Biteko awaomba wanachama wa CCM kumuunga mkono kwa kumchagua Rais Samia na mgombea mwenza Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu.


Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Geita, Nicholous Kasendamila  amewapongeza CCM Wilaya ya Bukombe kwa ujenzi wa maduka hayo na kusema kuwa hilo ni darasa na siasa ni uchumi na ni wajibu wa CCM kukiimarisha chama chao. 


Naye, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa, Mkoa wa Geita, Evarist Gervas amepongeza Dkt. Biteko kwa kuimarisha Chama katika wilaya  hiyo na kushirikiana vizuri na viongozi wa Chama kwa kuimarisha wilaya hiyo kiuchumi.


Awali akitoa taarifa ya ujenzi wa maduka hayo ya kisasa, Katibu wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Bukombe, Leonard Mwakalukwa amesema kuwa Wilaya hiyo  inatimiza sera ya CCM ya miradi ya uwekezaji na kwa kutambua kauli mbiu ya siasa na uchumi, ilitekeleza wazo la ujenzi wa maboresho ya vibanda hivyo 21 vilivyokuwepo awali liliasisiwa na Mbunge wa jimbo la Bukombe Dkt. Biteko.


Amesema Dkt. Biteko alitoa wito wa kuwa na vitega uchumi zaidi vya Chama cha Mapinduzi na kutunza na kuboresha mandhari ya eneo la CCM la Wilaya ya Bukombe. Ndipo Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Bukombe ikapitisha pendekezo hilo.


Ametaja faida za mradi kuwa ni pamoja na CCM wilayani humo kukusanya mapato kwa wingi.


MWISHO

MBOGGO ACHUKUA FOMU YA KUWANIA UBUNGE JIMBO LA TANGA KUPITIA ACT- WAZALENDO HUKU AKIHAIDI KUIREJESHA TANGA YA VIWANDA

May 27, 2025 Add Comment
Katibu wa Chama cha ACT -Wazalendo  Wa Jimbo la Tanga Mohamed Salim Ponda (kushoto)  akimkabidhi fomu ya kuomba kuteuliwa kuwa mgombea Ubunge Jimbo la Tanga mwanachama wao John Charles Mboggo  (katikati)  kulia ni Mwenyekiti wa Wazee Jimbo la Tanga (ACT Wazalendo) Zaharan Mohamed


Na Oscar Assenga, Tanga.

KADA wa Chama Cha ACT –Wazalendo Mkoani Tanga John Charles Mboggo amechukua fomu ya kuomba kuteuliwa kuwania Ubunge katika Jimbo la Tanga kupitia chama hicho huku akihaidi kuirejesha Tanga ya Viwanda ambayo ni ndoto kubwa ya wananchi wa mkoa huo.

Akizungumza leo na waandishi wa habari mara baada ya kuchukua fomu hiyo alisema lenbgo la kuchukua fomu ya kuwania Ubunge ni kutaka kuhakikisha anatoa mchango wake katika kurejesha viwanda vya Tanga ambavyo wananchi wamekuwa na kiu navyo.

Alisema kwamba kwa sababu viwanda ni ajira  na nguvu kazi ya Tanga wanaongelea kuna vijana asilimia 68 ya vijana wakitumika kwenye viwanda watakuwa na uchumi kwenye Jimbo hilo na Mkoa kwa Ujumla.

“Tanga tunaamini sisi ni watu tunaamini watu wa kuleta maendeleo na ndio maana tunawahamasisha wananchi wenye sifa za kupiga kura kujitokeza kwa wingi kushiriki kwenye zoezi la kura  kwa lengo la kuwachaguoa viongozi watakaowaongoza”Alisema



Aidha alisema kwamba wasione aibu kutokana na uwepo wa hila mbalimbali wanajua namna ya kubaliana nayo ili kuhakikisha hazijitokezi kwenye mchakato huo.

Awali akizungumza Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Jimbo la Tanga  Anasi Mohamed Rweymamu alisema kwamba wanaendelea kuwakaribisha wagombe na kura zao wa maoni ndani ya chama ndizo zitakazoamua nani anaweza kupeperusha tiketi ya chama hicho kwenye nafasi ya Ubunge.

Alisema kwamba ACT Wazalendo ndio chama pekee ambacho kinaweza kupeperusha vyema Bendera yake katika kuibuka na ushindi kwenye nafasi ya Ubunge Jimbo la Tanga na Tanzania kwa upekee.

Naye kwa upande Katibu wa ACT  WaaJimbo la Tanga Mohamed Salim Ponda alisema kwamba wapo kwenye maandalizi ya uchaguzi kama chama hicho Taifa kilipotangaza kwamba zoezi la kuchukua fomu kutoka Aprili 18 mwaka huu mpaka 31 mwezi Mei katika nafasi za Ubunge na Udiwani.

Alisema kwamba katika uchaguzi huo wamejipanga kwamba wagombea watakao wapitisha katika kinyang’anyiro cha Ubunge katika Jimbo hilo watakuwa imara kuhakikisha wanapeperusha vyema bendera hiyo.

Mwisho.

MBUNGE NEEMA LUGANGIRA-AKILI MNEMBA INA TIJA NA FURSA NYINGI IKITUMIKA IPASAVYO

May 11, 2025 Add Comment

Na Mwandishi Wetu,DODOMA

MBUNGE wa Viti Maalumu Kupitia Kundi la Asasi za Kiraia Tanzania (NGOs) Neema Lugangira amesema kwamba akili mnemba (artificial intelligence - AI) ina tija na fursa nyingi katika sekta mbalimbali ikiwemo Afya,Kilimo na Elimu na nyenginezo hapa nchini.

Aliyasema hayo wakati akizungumza katika Semina ya Akili Mnemba kwa Wabunge Wanawake iliyoandaliwa kwa Ushirikiano na Shirika ambalo alilianzisha la Omuka Hub pamoja na Bunge la Tanzania kupitia Mradi wa Female Al Leaders chini ya Women Political Leaders (WPL) na GIZ unaolenga kuimarisha Utawala Bora wa Akili Mnemba “Artificial Intelligence #Al” kwa kuimarisha Wanawake Wanasiasa barani Afrika ili waweze kuibeba ajenda hiyo na kuwa Vinara.

Alisema katika Semina hiyo wamejadiliana mambo mengi na imeonyesha akili mnemba inafursa nyingi lakini alitoa angalizo pia isipotumika kwa usahihi ina changamoto ikiwemo ukatili wa kijinsia, kurubuni watoto na inaweza kupelekea kufifisha uwezo wa kufikiria kutokana na kutufanya sisi kuwa tegemezi sana.

“Katika semina hii, akili mnemba imetushangaza sisi kama Wabunge sababu niliamua kufanya jaribio la kuiuliza hii AI swali kuwa mimi ni Mbunge na naelekea kwenye uchaguzi, naomba inisaidie kuniandalia mkakati wa kampeni na baada ya dakika chache AI ikanipa mkakati kabambe kwa usahihi hadi mwenyewe unashangaa na inakuwa na uwezo wa muda mfupi wa kupima kila kilicho kwenye mitaandao yote yenye uwezo nayo inakupa picha pana”, Alisema Mbunge Neema Lugangira.

Alisema kwamba Akili Mnemba ni kitu ambacho kina tija lakini tija hiyo ili iweze kupatikana lazima itumike kwa ufasaha na wao kama Wabunge ni kitu ambacho wanakwenda kukiangazia; ni lazima kama Tanzania iwepo sera ya akili mnemba pamoja na sheria ili kama taifa linufaike na faida zake na pia kujikinga na kudhibiti na madhara yanayoweza kupatikana kwenye eneo hilo la akila memba.

Awali akizungumza Mbunge wa Jimbo la Iringa Mjini (CCM) Jesca Msambatavangu alisema niwaondolee hofu akili mnemba haijaja kupora ajira za watu  bali imekuja kuboresha ajira na  kukuanzisha ajira na haijaja kumbagua mtu yoyote lakini lazima tutambue dunia ina mambo mazuri na mabaya hayo mambo wanatakiwa kujifunza mambo muhimu hivyo tunashukuru kuletewe semina hii ambavyo tunaamini itakuwa na tija”.

Naye kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii Fatma Toufiq alisema Bunge linatambua fursa na changamoto za akili mnemba hivyo Bunge wanajipanga kuandaa Sheria za Usimamizi.

Mbunge Fatma ambaye alimwakilisha Spika wa Bunge Dkt Tulia Ackson kwenye Semina hiyo ya Wabunge Wanawake kuhusu Akili Mnemba “Artificial Intelligence” ambapo alisema kwamba Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limefurahi kuwa sehemu ya kunufaika na mafunzo ya teknolojia ya akili mnemba.

Mhe Neema Lugangira (MB) ni mwakilishi Afrika wa Women Political Leaders (WPL)amefanikiwa kufanikisha mradi wa Female Al Leaders kuja hapa Tanzania ambapo sehemu ya kwanza ilikuwa ni kuandaa Semina ya Wabunge Wanawake kwa kushirikiana na Shirika ambalo alilianzisha la Omuka Hub pamoja na Bunge la Tanzania.


MWISHO.

MCC LAILAH NGOZI MGENI KONGAMANO LA NASIMAMA NA MAMA LITAKALOFANYIKA JIJINI TANGA

May 09, 2025 Add Comment
Na Mwandishi WETU,TANGA.

MJUMBE wa Kamati Kuu ya CCM Taifa Lailah Burhan Ngozi anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Kongamano linalohusu Mchango wa Rais Samia Suluhu kwa mabinti na Wanawake wa Tanzania katika miaka minne ya uongozi wake litakalofanyika Mei 11 mwaka huu Jijini Tanga .

Kongamano hilo linatarajiwa kufanyika kwenye ukumbi swa Regail Naivera Jijini Tanga Mei 11 ambayo ni siku ya Mama Duniani ambalo litaanza saa tatu hadi saa kumi jioni

Akizungumza na waandishi wa habari leo Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwanamke na Uongozi ambao wameandaa Kongamano hilo Shamira Mshangama alisema lengo ni kuonesha mchango wa Rais Dkt Samia Suluhu kwa mabinti na wanawake wa Tanga na Tanzania kwa ujumla.

Alisema kwamba kongamano hilo limejikita katika kutambua jitihada zilizofanywa na Rais Dkt Samia Suluhu katika Sekta ya Afya,Elimu,Uchumi na Uongozi.

Shamira alisema kwamba Kongamano hilo linatarajiwa kuhudhuriwa na mabinti na wanawake takribani 400 kutoka mkoa wa Tanga na mikoa ya Jirani .

CCM TANGA YASAJILI ZAIDI WANACHAMA 500,000 KIELETRONIKI KWA MUDA WA SIKU 10

April 24, 2025 Add Comment

Na Oscar Assenga, TANGA

CHAMA cha Mapinduzi Mkoa wa Tanga (CCM) wamefanikiwa kusajili zaidi ya wanachama 550,000 kwa mkoa wa huo kwa mfumo wa kieletroniki kwa muda wa siku 10 wakiziita siku 10 za moto, katika zoezi hilo wamefanikiwa kuhakiki Taarifa za wanachama wao na sasa wako kwenye siku 10 za moto za kugawa kadi za kieletroniki kwa Wilaya za Mkoa huo baada ya usajili na uhakiki kukamilika.

Akizungumza na Mtandao huu,Katibu wa Siasa,Uenezi na Mafunzo Mkoa wa Tanga Ndugu Samwel Kiondo Mngazija alisema kwamba wanaendelea na zoezi hilo katika Wilaya mbalimbali za mkoa huo huku usajili nao ukiwa unaendelea na kwa sasa kwenye mfumo wana wanachama zaidi ya 700,000 mpaka 800,000 ambao wamesajiliwa.

“Zoezi hili la uhakiki wa wanachama wetu tunalifanya kwa umakini mkubwa na weledi na tunazunguka Mkoa mzima kwa siku 10 za moto kugawa kadi za kieletroniki za CCM kwa wanachama wetu na tunaendelea na uhakiki wa Taarifa na usahihishaji wa taarifa za wanachama wetu na zoezi la usajili wanachama wapya linaendelea”Alisema



Aidha alisema kwamba awali kwenye mkoa wa Tanga walikuwa na zaidi ya wanachama 200,000 wanatarajia kufikiwa na mfumo wa kadi za kieletroniki ambao usajili ulianza 2018 na mwaka huu walihuisha zoezi kwa maana watu wengi walikuwa hawajaingia kwenye mfumo na usajili ulikuwa unaendelea.

“Kutokea mwaka huu tulikuwa na siku 10 za moto ambapo wilaya zote za Mkoa wa Tanga tumezifikia kwa Maelekezo ya Mwenyekiti wetu wa CCM Taifa Dkt Samia Suluhu Hassan kuleta Vitendea Kazi kila kata kwa ajili ya kurahisisha usajili na kwenda na kasi kutokana na uhitaji wa kadi kwa wanachama wetu hivyo kupelekea zoezi la siku 10 za moto kuwa na tija kubwa pamoja na Usimamizi wa Jemedari wa Vita Ustadhi Rajab Abrahamani Abdallah Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Tanga na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa” Alisema  

Hata hivyo alisema kwamba kila siku wanachama wanajiunga nao kutokana na maendeleo makubwa yanayofanywa na Serikali inayoongozwa na CCM chini ya Daktari Samia Suluhu Hassan Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na wasaidizi wake. 

BALOZI NCHIMBI AFUNGA KAZI RUVUMA

April 07, 2025 Add Comment

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, amehitimisha ziara yake ya siku tano mkoani Ruvuma, akisisitiza kuwa CCM itaendelea kuwa chama cha wanachama, kwa ajili ya kuwatumikia wananchi wote na kuwa mtetezi wa wanyonge.

Balozi Nchimbi amesema kwamba katika kuendeleza nafasi yake kama taasisi imara inayohusika na uongozi wa nchi, CCM hakina budi kuendeleza misingi ya sera zake zinazolenga kubadilisha hali za maisha ya watu, kuendana na mahitaji ya nyakati, na kuzingatia maslahi ya taifa.

Dkt. Nchimbi aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na wanaCCM na wananchi wa mji wa Songea, waliokusanyika kumpokea alipofika kufungua mradi wa kitega uchumi wa Tawi la CCM la Mshangano mjini Songea, Jumapili tarehe 6 Aprili 2025, ikiwa ni siku ya tano tangu alipoanza ziara hiyo tarehe 2 Aprili 2025.

Katika ziara hiyo aliyoanzia katika Wilaya ya Tunduru, Namtumbo, Nyasa, na hatimaye Songea mjini, Balozi Nchimbi alitoa pongezi kwa Serikali ya CCM, inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM, kwa jinsi inavyotafsiri kwa vitendo na ufanisi, Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya 2020-2025, kupitia miradi ya maendeleo na huduma kwa wananchi.

Balozi Nchimbi alitoa maelekezo kwa Serikali kuendelea kusimamia na kubuni mipango inayolenga kuongeza matokeo chanya kwenye shughuli za uzalishaji mali, ikiwemo kilimo na madini, ili wakulima na wachimbaji madini waendelee kuzalisha kwa tija itakayoongeza pato la taifa na kuboresha maisha ya wananchi.


Aidha, Balozi Nchimbi alitembelea na kutoa maelekezo mahsusi katika miradi kadhaa ya maendeleo na ya kimkakati inayotekelezwa na Serikali kupitia wizara na taasisi zake, ikiwemo mradi wa uzalishaji mbegu chini ya Mamlaka ya Mbegu Nchini (ASA) na ujenzi wa Bandari ya Nyasa, kwa lengo la kuendelea kutafsiri utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM.


Katika mikutano ya hadhara katika wilaya mbalimbali, pamoja na kusalimia wananchi katika maeneo ya Songea Vijijini, Mbinga na Songea mjini, Balozi Nchimbi alipokea taarifa za utendaji wa kazi kutoka kwa viongozi wa Chama na Serikali, na pia alipokea maoni ya wananchi kuhusu changamoto zinazowakabili, kupitia kwa wabunge na wananchi moja kwa moja, kisha kutoa maelekezo ya kutatuliwa kwa kero hizo.


Balozi Nchimbi, ambaye amehitimisha rasmi ziara yake kwa kuondoka mkoani humo Jumatatu tarehe 7 Aprili 2025, alitumia nafasi hiyo kuwashukuru wanaCCM na Watanzania wote kwa ujumla kwa ushirikiano wao na Serikali ya CCM katika kulinda tunu za taifa, ikiwemo amani na utulivu. Alitoa wito wa kuendeleza hali hiyo wakati nchi inapoelekea kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu.


#Ends

DKT.SAMIA AMETENDA MAAJABU SEKTA YA NISHATI MIAKA MINNE YA UONGOZI -DKT.BITEKO

March 24, 2025 Add Comment


📌 Mashine ya 9 yakabidhiwa, yakamilisha MW 2115 - JNHPP


📌 Aitaka Jumuiya ya Wazazi ieleze Watanzania mafanikio ya Serikali


📌 Asema kuongezeka kwa mahitaji ya umeme nchini kunachochea ukuaji wa viwanda


📌 Atoa wito kwa Watanzania kuzingatia matumizi bora ya umeme


Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati


Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan sekta ya nishati imepiga hatua kubwa nchini sambamba na kuzalisha umeme wa ziada dhidi ya mahitaji ya Watanzania.

Dkt. Biteko amesema hayo Machi 23, 2025 jijini Arusha wakati akitoa takwimu kuhusu  ongezeko la mahitaji  ya umeme nchini katika Kikao cha Baraza Kuu la Wazazi Taifa.


“ Rais Samia amefanya kazi kubwa katika sekta ya nishati nchini na hivi karibuni, tulikuwa nchini Barbados kueleza  mafanikio yetu katika sekta hii kwa kuwa Rais Samia amefanya jitihada kubwa sana katika ya nishati,” amesema Dkt. Biteko.

Ameongeza “Ili uchumi wa nchi yoyote duniani upatikane lazima kuwe na sekta ya nishati. Aidha, katika sekta ya nishati ili viwanda viweze kuendelea umeme unaohitajika ni asilimia 40 na katika sekta ya madini umeme unaohitajika ni asilimia 30,” 


Dkt. Biteko amesema mwaka 2017 hadi 2018 mahitaji ya juu ya umeme nchini yalikuwa megawati 1045, mwaka 2018 hadi 2019 mahitaji ya juu ya umeme yalikuwa megawati 1,116 mwaka 2021 hadi 2022 megawati 1,340.7.

“ Mwaka 2022 hadi 2023 mahitaji ya juu yaliyoongezeka na kufikia  megawati 1,470 na mwaka 2024 hadi kufikia sasa mwaka 2025 ni megawati 1,908 ikiwa ni sawa na megawati 262, ongezeko la mahitaji ya namna hii haliwezi kutokea kama hakuna uwekezaji katika sekta ya nishati,” amesema Dkt. Biteko.


Aidha, Dkt. Biteko amesema kuwa Mashine ya tisa ya mtambo wa kuzalisha umeme katika Bwawa la Julius Nyerere Machi 22, 2025 imekabidhiwa na kuunganishwa kwenye Grid ya Taifa. Amesisitiza kuwa kutokana na ongezeko hilo la megawati za umeme Bwawa la Kuzalisha Umeme la Julius Nyerere pekee linaweza kutosheleza mahitaji ya nchi licha ya kumalizika kwa muda uzalishaji wa umeme kwa kutumia mitambo ya Songas.

 “Katika kipindi cha miaka minne ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan sekta ya nishati imefanya kazi kubwa, Rais Samia ametenda maajabu katika sekta hii na ameweza kuvutia wawekezaji wengi sana kuja kuwekeza nchini,” amesema Dkt. Biteko.

Aidha, amesema kuwa Jumuiya ya Wazazi nchini ina wajibu wa malezi na mazingira na kuwa nishati safi ni eneo mojawapo hivyo Wizara ya Nishati ina wajibu wa kushirikiana  na wadau mbalimbali ikiwemo Jumuiya hiyo, sambamba na kushirikiana nayo katika kampeni zake za kupeleka ujumbe kwa jamii.

Pamoja na hayo, Dkt. Biteko amewaasa Watanzania kuzingatia matumizi bora ya umeme kwa kuacha mazoea yanayosababisha upotevu wa umeme ikiwemo kuwashaa taa bila kuwa na matumizi nazo.


Ametolea mfano kuhusu matumizi mabaya ya umeme kupitia utafiti uliofanywa na Wakala wa Nishati wa Kimataifa (International Energy Agency) ambapo asilimia 30 ya umeme unapotea kutokana na mazoea.


Katika hatua nyingine, taasisi mbalimbali ikiwemo Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (TANAPA) zimewasilisha mada mbalimbali katika semina hiyo.


Pia, Wizara ya Nishati kupitia taasisi zake za TPDC, REA na TANESCO zimetoa semina kwa wajumbe wa kikao hicho kuhusu Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia 2024 hadi 2034, Matumizi Sahihi ya Nishati Safi ya Umeme.


Ambapo, Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Nishati Safi ya Kupikia, kutoka Wizara ya Nishati, Bw. Ngeleja Mugejwa ameeleza faida mbalimbali za matumizi ya nishati safi ya kupikia hususan kwa watoto wa kike ambapo  kupitia matumizi ya nishati hiyo itawasaidia kupata muda mwingi wa kujisomea kuliko kuandaa na kupika chakula.

SHAMIRA AKABIDHI SHILINGI MILIONI 1 UJENZI WA NYUMBA YA KATIBU KASKAZINI UNGUJA

March 24, 2025 Add Comment

Mjumbe wa Baraza kuu UVCCM Viti vitatu Bara Ndg. Shamira Mshangama @shamiramshangama akiwa kwenye muendelezo wa ziara yake ya kuimarisha uhai wa Jumuiya ya Vijana CCM na kuhamasisha ushiriki wa vijana kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka huu 2025.

Shamira alitembelea ofisi ya UVCCM Mkoa wa Kaskazini Unguja, Zanzibar kufanya kikao kifupi cha ndani, na kukabidhi shilingi milioni moja kwa kamati ya Utekelezaji na viongozi wa Baraza la UVCCM Mkoa wa Kaskazini Unguja iliyopokelewa na Katibu wa UVCCM Mkoa huo Comrade Rished Khalfan pamoja na wajumbe wengine ngazi ya mkoa na Wilaya.


Shamira amewasisitiza kuwa pamoja na kazi zote tunazofanya lakini viongozi tunajukumu la kuzingatia ujenzi wa CCM na Jumuiya zake.

“Ujenzi wa Chama ni jukumu letu sote”.