WIZARA YA NISHATI ENDELEENI KUWEZESHA UWEKEZAJI WA VITUO VYA MAFUTA VIJIJINI-WAZIRI SIMBACHAWENE

June 17, 2025


📌 *Atembelea Banda la Wizara ya Nishati na Taasisi zake katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma*


DODOMA


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,  Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe.George Simbachawene ameiasa Wizara ya Nishati kuendelea kuweka mazingira wezeshi yatakayowezesha uwekezaji zaidi wa vituo vya mafuta vijijini.


 Simbachaene amesema hayo tarehe 17 Juni, 2025, jijini Dodoma wakati alipotembelea Banda la Wizara ya Nishati katika Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma  yanayoendelea katika viwanja vya Chinangali ambayo leo yamefunguliwa rasmi

" Wafanyabiashara wengi wanataka kuwekeza kwenye vituo vya Mafuta vijijini kwakuwa bado  kuna uhaba wa vituo, hivyo angalieni masharti yanayowekwa kwenye uwekezaji yasiwe kikwazo kwenye huduma hii muhimu." Amesema Simbachawene

Pia, Simbachawene  ameishauri Wizara kuongeza kasi ya upatikanaji  wa Nishati Safi ya Kupikia Vijijini pamoja na kuhamasisha uwekezaji kwenye Nishati Safi ya Kupikia.


Vilevile, ameipongeza Wizara ya Nishati na  Taasisi zake kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuendelea kutoa huduma za Nishati kwa wananchi.

Share this

Related Posts

EmoticonEmoticon

:)
:(
=(
^_^
:D
=D
=)D
|o|
@@,
;)
:-bd
:-d
:p
:ng