Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Tanga (TANGA UWASA) inaendelea na utekelezaji wa Mradi wa Uboreshaji miundombinu ya maji na utunzaji wa mazingira awamu ya tatu kupitia ufadhili wa Hatifungani ya Kijani (TANGA WATER GREEN BOND).
![]() |
Ambapo kwa sasa kazi ya uchimbaji wa mitaro na ulazaji wa mabomba makubwa yenye kipenyo cha 600mm yanayolazwa kwa urefu wa kilomita 6 kutoka katika Mtambo wa kusukuma maji Mabayani kuelekea katika Kituo cha kuzalisha maji Mowe imekwishaanza na utekelezaji wake umefikia asilimia 20.
Mradi huu unatekelezwa na Mkandarasi Mzawa S.T.C Construction company Limited ambapo lengo kuu ni kuongeza uwezo wa kusukuma maji kutoka lita Milioni 42 zilizopo sasa hadi kufikia lita Milioni 60 ili kuwezesha upatikanaji wa huduma bora na ya uhakika kwa wakazi ya Jiji la Tanga pamoja na Miji ya Muheza na Mkinga.
EmoticonEmoticon