PSSSF YATOA HUDUMA KWENYE KIKAO KAZI CHA WENYEVITI WA BODI NA WAKUU WA TAASISI ZA UMMA AICC-ARUSHA

August 29, 2024

 ARUSHA.


MFUKO wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), umeweka kambi kwenye viwanja vya Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), ili kutoa huduma kwa wajumbe wa Kikao Kazi cha Wenyeviti na Wakuu wa Taasisi za Umma ambacho kimefunguliwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Agosti 28, 2024.

Kwa mujibu wa Meneja wa PSSSF, Kanda ya Kaskazini, Bw. Venance Mwaijibe, amesema PSSSF imetehamisha huduma zake kutoka matumizi ya karatasi kwenda PSSSF Kidigitali, ambapo mwanachama atatumia Simu janja au Computer kupata huduma zote zinazohusiana na uanachama wake.

“Pamoja na kutoa huduma kwa wanachama, jambo kubwa tunalofanya hapa ni kuwaelimisha jinsi ya kutumia simu janja kupata huduma hizo ikiwemo, kupata taarifa za michango, taarifa za mafao, kuwasilisha madai mbalimbali, lakini na wastaafu nao wanaweza kujihakiki.” Amefafanua Bw. Mwaijibe.

Kikao hicho cha siku tatu, kimeandaliwa na Ofisi ya Msajili wa hazina kwa lengo la kuwaweka pamoja wakuu hao na kujadili mambo mbalimbali ikiwemo maboresho yanayoendelea katika kuimarisha usimamizi, uendeshaji na utendaji wa Taasisi za umma sambamba na kubadilishana uzoefu.

Washiriki wanatoka katika Mashirika ya Umma 248 ambayo yanamilikiwa na serikali kwa silimia 100 na wengine wanatoka katika Mshirika 58 ambayo serikali inamiliki hisa hadi asilimia 50.

Kikao hicho kinagusa uchumi wa nchi kutokana na uwekezaji mkubwa uliofanywa na serikali unaozidi trilioni 76.

























Share this

Related Posts

Previous
Next Post »