ESRF YARATIBU ZIARA YA WATAALAM WA UCHUMI KUTEMBELEA SHUGHULI ZA WAJASIRIAMALI WA SIDO

May 02, 2018


Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii. (ESRF), Dkt. Tausi Kida (kushoto) na Profesa Kaushik Basu (katikati), wakimsikiliza Mkurugenzi wa Kampuni inayojishughulisha na uuzaji wa asali , Fredy Swai , wakati wa ziara ya kutembelea Shirika la Uendelezaji Viwanda Vidogo (SIDO), ili kuona jinsi wajasiriamali wanavyoendesha shughuli zao. Ziara hiyo imefanyika jijini Dar es Salaam. (Picha na Abubakari Akida)

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi Kida, akimuelekeza jambo Profesa Joseph Stiglitz wakati wa ziara ya kutembelea Shirika la Uendelezaji Viwanda Vidogo (SIDO), ili kuona jinsi wajasiriamali wanavyoendesha shughuli zao. Ziara hiyo imefanyika jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Kampuni inayotengeneza bidhaa ya mafuta ya kupaka kwa kutumia malighafi ya mimea, Obed Musiba (kulia), akitoa maelezo juu ya bidhaa zake kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi Kida (aliyeshika losheni) na Profesa Joseph Stiglitz, wakati wa ziara ya kutembelea Shirika la Uendelezaji Viwanda Vidogo (SIDO), ili kuona jinsi wajasiriamali wanavyoendesha shughuli zao. Ziara hiyo imefanyika jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tafiti za Kiuchumi na Kijamii (ESRF), Dkt. Tausi Kida (katikati), akiwaongoza wageni kutembelea eneo la Shirika la Uendelezaji Viwanda Vidogo(SIDO), ili kuweza kukagua shughuli za wajasiriamali wanaojishughulisha na uzalishaji wa bidhaa mbalimbali.Kulia ni Profesa Kaushik Basu na Kushoto ni Profesa Sabina Alkire, ziara hiyo imefanyika jijini Dar es Salaam. (Picha na Abubakari Akida)

Geofrey Adroph BLOGGER P.O.BOX 24793, Mob: +255 755 274953 /+255 713 363965, Email: pamojapure@gmail.com. Blog: http://www.pamoja.co.tz/ DAR ES SALAAM, TANZANIA

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »