TAIFA
STARS KUCHEZA NA ALGERIA NA DR CONGO MWEZI HUU
Timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars inatarajia kucheza
michezo miwili ya kirafiki mwezi huu wa Machi kwenye tarehe za kalenda ya FIFA.
Taifa Stars itakuwa ugenini nchini Algeria Machi 22,2018
kucheza dhidi ya Algeria kabla ya kucheza na DR Congo Machi 27,2018 Uwanja wa
Taifa Dar es Salaam,Tanzania.
Tayari mechi hizo zimethibitishwa na pande zote mbili
kuchezwa katika tarehe hizo.
UPANGAJI
RATIBA ROBO FAINALI NA NUSU FAINALI KOMBE LA SHIRIKISHO LA AZAM WAFANYIKA
Upangaji wa ratiba kwa hatua ya robo fainali na nusu
fainali ya mashindano ya Kombe la Shirikisho la Azam umefanyika leo Ijumaa
Machi 2, 2018 kwenye Makao Makuu ya Azam Tv.
Droo hiyo imehusisha timu saba za Ligi Kuu ya Vodacom
Tanzania Bara na timu moja ya Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara.
Timu zilizochezeshwa kwenye droo hiyo ni Young Africans,Azam
FC,Singida United,Tanzania Prisons,Njombe Mji,Stand United,JKT Tanzania na
Mtibwa Sugar.
Mechi za hatua hiyo zitapangiwa tarehe ya kuchezwa baada
ya tarehe za awali kuingiliana na mechi za timu ya Taifa ya Vijana chini ya
miaka 20 zilizotajwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Africa CAF.
Ratiba
Nane bora
Singida United vs Young Africans Uwanja wa Namfua
Tanzania Prisons vs JKT Tanzania Uwanja wa Sokoine
Azam FC vs Mtibwa Sugar Azam Complex
Stand United vs Njombe Mji
Uwanja wa Kambarage
Nusu
Fainali
Stand United/Njombe Mji vs Azam FC/Mtibwa
Singida United/Young Africans vs Tanzania Prisons/JKT
Tanzania
Fainali
Singida United/Young Africans vs Tanzania Prisons/JKT
Tanzania vs Stand United/Njombe Mji vs Azam FC/Mtibwa
LIGI
KUU YA VODACOM TANZANIA BARA MZUNGUKO WA 20 KUENDELEA KESHO
Mzunguko wa 20 wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania bara
unaendelea kesho Jumamosi Machi 3,2018 kwa kuchezwa mechi nne.
Njombe Mji watakuwa nyumbani Uwanja wa Sabasaba kucheza na
Ruvu Shooting mchezo utakaochezwa saa 8 mchana wakati Kagare Sugar wao watakuwa
nyumbani Uwanja wa Kaitaba kuwakaribisha Majimaji ya Songea mchezo utakaochezwa
saa 10 jioni.
Mechi nyingine Tanzania Prisons ya Mbeya watakuwa nyumbani
Uwanja wa Sokoine kucheza dhidi ya Mbao FC ya Mwanza saa 10 jioni,Azam FC
watakuwa Azam Complex ikiwakaribisha Singida United saa 1 jioni.
LIGI
KUU YA WANAWAKE YA SERENGETI PREMIUM LITE HATUA YA NANE BORA KUENDELEA KUTIMUA
VUMBI KESHO
Ligi Kuu ya Wanawake ya Serengeti Premieum Lite hataua ya
Nane bora inataraji kuendelea kesho Jumamosi Machi 3,2018 na Jumapili Machi
4,2018.
Jumamosi,Machi
3,2018
Panama FC vs JKT Queens Uwanja wa Samora
Jumapili
Machi 4,2018
Simba Queens vs Evergreen Uwanja wa Karume
Mlandizi vs Kigoma Uwanja wa Mabatini
Baobab vs Alliance Uwanja wa Jamhuri
IMETOLEWA
NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA TFF