Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri
Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu Mhe. Jenista
Mhagama akikagua maandalizi ya maadhimisho ya sherehe za miaka 56 ya
Uhuru wa Tanzania Bara katika Uwanja wa Jamhuri leo Mjini Dodoma.
Onesho kutoka katika Kikundi cha
Komando wakionesha umahiri wao katika kutekeleza majukumu yao ikiwa ni
sehemu ya maandalizi ya Maadhimisho ya sherehe za miaka 56 ya Uhuru wa
Tanzania Bara katika Uwanja wa Jamhuri leo Mjini Dodoma.
Mkurugenzi wa Idara ya
Habari-MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbas akiteta
jambo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana,
Ajira na Watu wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama wakati wa ukaguzi wa
maandalizi ya Maadhimisho ya sherehe za miaka 56 ya Uhuru wa Tanzania
Bara katika Uwanja wa Jamhuri leo Mjini Dodoma.
Gwaride la Mkoloni kutoka Jeshi la
Polisi likionesha umahiri wake ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya
Maadhimisho ya sherehe za miaka 56 ya Uhuru wa Tanzania Bara katika
Uwanja wa Jamhuri leo Mjini Dodoma.
Maofisa wa Jeshi la Polisi
wanaoongoza misafara ya Viongozi wakionesha umahiri wao katika
kutekeleza majukumu yao ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Maadhimisho ya
sherehe za miaka 56 ya Uhuru wa Tanzania Bara katika Uwanja wa Jamhuri
Dodoma leo Mjini Dodoma.
Halaiki ya wanafunzi wa shule za
msingi na sekondari wakiunda umbo lililoonesha ramani ya Tanzania wakati
wa maandalizi ya Maadhimisho ya sherehe za miaka 56 ya Uhuru wa
Tanzania Bara katika Uwanja wa Jamhuri leo Mjini Dodoma.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma
Bibi Rehema Madenge akimueleza jambo Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu
Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu Mhe. Jenista
Mhagama wakati wa maandalizi ya Maadhimisho ya sherehe za miaka 56 ya
Uhuru wa Tanzania Bara katika Uwanja wa Jamhuri leo Mjini Dodoma.
Picha zote na Beatrice Lyimo, MAELEZO, DODOMA