SBL yazindua kinywaji kipya cha SMIRNOFF X1 Extra Pure Vodka

December 14, 2017



Meneja Ubunifu wa Kampuni ya Bia ya Serengeti, Wankyo Marando akifafanua ubora wa kinywaji kipya   cha Smirnoff X1 Extra Pure Vodka wakati wa  uzinduzi wa kinywaji hicho  mapema jana usiku wa jana.


 Wadau wakionesha chupa yenye kinywaji kipya cha Smirnoff X1 Extra Pure Vodka wakati wa hafla ya uzinduzi iliyofanyika Ukumbi wa LAPF Kijitonyama jijini Dar es Salaam jana.



 Mtaalamu wa kuchanganya vinywaji, Junior Charles akielekeza namna ya kuchanganya kinywaji hicho.
 Mafuriko ya wadau katika uzinduzi wa kinywaji hicho uliofanyika Ukumbi wa LAPF Kijitonyama jijini Dar es Salaam.
 Warembo wakiwa na kinywaji hicho kabla ya kwenda kupeleka kwa wadau
 Chupa ya kinywaji hicho ikiwa imeinuliwa juu na wadau.
 Mmoja wa wadau akiangalia chupa yenye kinywaji hicho.
 Uzinduzi ukiendelea.
 Wadau wakiwa kwenye hafla hiyo
 Muonekano wa kinywaji hicho katika chupa.
 Hapa ni furaha tupu katika hafla hiyo
 Wafanyakazi wa SBL wakigonganisha glasi wakati wa uzinduzi huo.
Wadau mbalimbali wakifurahia kichwaji hicho huku wakiburudika kwa muziki.


 Meneja Ubunifu wa Kampuni ya Bia ya Serengeti, Wankyo Marando akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya uzinduzi wa kinywaji kipya cha Smirnoff X1 Extra Pure Vodka mapema jana usiku wa jana.



Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) imetangaza kuingiza kinywaji kipya kinachojulikana kama SMIRNOFF X1 Extra Pure Vodka kwenye soko la Tanzania kwa mara ya kwanza

Kuingia kwa kinywaji hiki kipya, ni mwendelezo wa uwepo wa kinywaji maarufu aina ya SMIRNOFF ambacho wateja SBL wamekuwa wakikifurahia kwa miaka kadhaa hapa nchini.
Kikiwa kimechujwa kwa ustadi wa hali ya juu, SMIRNOFF X1 Extra Pure Vodka inakuja ikiwa na kilevi cha kiwango cha asilimia 43 huku ikiwa na ladha nzuri inayoweza kufurahiwa katika matukio mbali mbali
.
“Kinywaji hiki kipya cha Smirnoff X1 Extra Pure, ni kinywaji murua kwa wanywaji wote wanaokunywa kistarabu hasa wakati huu tunapoelekea kipindi cha sikukuu na mwisho wa mwaka,” alisema Wankyo Marando  ambaye ni Meneja Ubunifu wa SBL wakati wa uzinduzi wa kinywaji hicho uliofanyika jijini Dar es Salaam.”
“Kutokana na sikukuu za kitaifa, sherehe za nyama choma na muziki, wateja wetu wanaweza kujumuika pamoja kusherehekea matukio kama haya ambayo yanawaleta pamoja huku wakijiburudisha na kinywaji kipya na chenye kuvutia cha Smirnoff X1 Extra Pure,” aliongeza Marando.

Meneja huyo alisema, SMIRNOFF X1 Extra Pure Vodka imefungashwa kwenye chupa zenye ujazo waa mililita 750 na 200 na kuongeza kuwa zitakuwa zikipatika katika maduka ya kuuza vileo kwa bei elekezi ya shilingi 12,000/- kwa chupa yenye ujazo wa mililita 750 na  shilingi 4,000/- kwe chupa yenye ujazo wa mililita 200.

Bei hizi ambazo ni nafuu, zitawawezesha wateja wa SBL kufurahia kinywaji hiki chenye ubora wa hali ya juu na chenye ladha ya kipekee kinachowaleta watu pamoja kwa urahisi.


Kikiwa ni moja kati ya vinywaji aina ya vodka kilichoshinda tuzo nyingi duniani, SMIRNOFF inafahamika kwa ubora wake kote ulimwenguni huku kikitumiwa na wanywaji wastaarabu katika nchi 130 duniani.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »