Tunakumbushana #SiUchochezi (Kipindi cha kwanza)

November 01, 2017
Kipindi cha Tunakumbushana #SiUchochezi ni kipindi kipya cha kila wiki kinacholenga kuibua na kuonyesha masuala mbalimbali katika jamii ambapo kitakuwa katika mfumo wa sauti, picha mnato pamoja na picha jongefu (video).

Kipindi hiki kimejikita kukosoa, kuonya na kusifia masuala mbalimbali ya kimaendeleo katika jamii yakiwemo ya kiutendaji, kisiasa, kiuchumi pamoja na kijamii nchini Tanzania.

Kinaandaliwa na kurushwa na mitandao ya kijamii ya Binagi Media Group (www.bmghabari.com) pamoja na mitandao mingime rafiki kote nchini, lengo likiwa ni kuamsha ari ya kimaendeleo katika jamii.

Rai ni kwa wadau wote wapenda maendeleo kuungana na BMG katika kuhakikisha kipindi hiki ambacho kimeanza kuruka hewani kwa mara ya kwanza hii leo Novemba Mosi, 2017 kinaleta matokeo chanya katika jamii.

Binagi Media Group
0757 43 26 94
Mwanza
#PamojaDaima!

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »