RC GAMBO AFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA UFARANSA KUBORESHA UTALII MKOANI ARUSHA

June 13, 2017
unnamed
*RC Gambo afanya mazungumzo na balozi wa Ufaransa kuboresha utalii mkoani Arusha*
Mkuu wa mkoa wa Arusha Mhe Mrisho Gambo akiwa Ufaransa, amefanya mazungumzo na Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa Mhe Samwel W Shelukindo. Ufaransa ni moja ya zinazoleta watalii wengi nchini Tanzania. Pamoja na mambo mwingine wamejadiliana Yafuatayo:-
1. Mambo ya Msingi ya kufanya ili kuongeza watalii kutoka Ufaransa kuja Arusha
2. Kupata wawekezaji kutoka Ufaransa kuja Arusha (Fursa za uwekezaji zilizopo Mkoani Arusha )
3. Kuanzisha tukio la kimataifa la kutangaza utalii mkoani Arusha kila mwaka
Mkuu wa mkoa wa Arusha Mhe Mrisho Gambo yupo katika ziara ya mafunzo nchini Ufaransa pamoja na mafunzo hayo amekua akiutangaza mkoa wa Arusha kama kitovu cha utalii nchini Tanzania.
1 2

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »