MALINZI AMLILIA SIR GEORGE KAHAMA

March 13, 2017


Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Emil Malinzi, ametuma rambirambi kwa familia ya marehemu Sir George Kahama aliyefariki dunia Jumapili akiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili jijini Dar es Salaam.

Rais Malinzi amesema taifa limepoteza mmoja wa watu waliotoa mchango mkubwa katika kupigania maendeleo ya mpira wa miguu baada ya kupigania Uhuru ambao Watanzania leo wanajivunia amani.

Pamoja na familia ya marehemu, ndugu, jamaa na marafiki, Rais Malinzi Dkt Magufuli amewapa pole wanachama wote wa Chama Cha Mapinduzi, akisema ni kielelezo cha kiongozi aliyetukuka.

“Kabla ya Uhuru Mzee wetu, Mzee Kahama alikuwa kiongozi shupavu na mzalendo, alama ambayo ametuachia sisi Watanzania leo hii tunajivunia amani,” alisema Rais Malinzi.

Rais Malinzi ambaye katika vikao vyake vya jana hapa Dar es Salaam, alikuwa akitoa nafasi ya kumkumbuka Sir George, akisema msiba huo pia ni wa TFF kwa kuwa mmoja wa watoto wake, Joseph ni Mjumbe wa Mfuko wa Bodi ya Maendeleo ya Mpira wa Miguu wa TFF.

Mwenyezi Mungu aipumzishe roho yake mahali pema peponi, Amina.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »