WASHIRIKI TTCL MISS HIGHER LEARNING WATOA ELIMU KUHUSU USALAMA BARABARANI

September 15, 2016



Washiriki wa TTCL Miss Higher Learning katika picha ya pamoja na wanafunzi wa shule ya Msingi Mbuyuni pamoja na Maofisa wa jeshi la polisi.
 Washiriki wa TTCL Miss Higher Learning wakipokea maellekezo toka kwa maofisa wa jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani makao makuu.
 Washiriki wa TTCL Miss Higher Learning wakiwavushabarabara wanafunzi wa shule ya msingi Uhuru mchanganyiko
Washiriki wa kinyang’anyiro cha kumsaka mrembo wa elimu ya juu kwa mwaka 20016 (TTCL Miss Higher Learning 2016) kwa kushrikiana na jeshi la pilisi kitengo cha usalama barabarani wametoa elimu ya matumuzi sahihi ya alama za barabarani pamoja na kuwavusha barabara baadhi ya wanafunzi toka katika baadhi ya shule zilizopo katika jiji la Dar es Salaam ikiwa ni siku moja kabla ya kufanyika kwa shindano hilo.


Miongoni mwa shule ambazo zimepata fursa ya kutembelewa na washiriki wa TTCL Miss higher learing ni Shule ya Msingi Mbuyuni, Shule ya msingi Osterbay, Shule ya Msingi Uhuru Mchanganyiko, Shule ya Msingi Mtoni, na Shue ya Msingi Mgulani.


Akizungumza na wanahabari muandaaji shindano la TTCL Miss higher learing, Maya Kitambo amesema lengo hasa la kufanya zoezi la kuwavusha barabara pamoja na maswali ya ufahamu juu ya sheria na alama za usalama barabarani kwa kushirikiana na jeshi la polisi kitengo cha usalama barabarani ni ili kutoa msisitizo kwa wanafunzi wa shule za msingi kuzifahamu alama na sheria ili kuepusha ajali ambazo huwahusisha wanafunzi wawapo barabarani.


“Sisi kama AJ Events tumeguswa katika utoaji wa elimu kwa wanafunzi pamoja na kuwavusha barabara kwani tunaamini kwamba kupitia washiriki wetu TTCL Miss higher learing, wanafunzi wataona umuhimu wa kuzijua sheria pamoja na kuwa makini wawapo barabarani” amesema Maya Kitambo.


Washiriki watakaoshiriki katika shindano hilo litakalofanyika katika ukumbi wa King Solomon Hall uliopo Namnaga ni Glory Gideon (Chuo cha Usimamizi wa fedha IFM), Lucy Ludy (TAASISI YA USTAWI WA JAMII), Jonatha Joram (Chuo cha Usimamizi wa fedha IFM), Clara Nyaki (TAASISI YA USTAWI WA JAMII), Rhoda Iddy (CBE), Evelyne Andrew (TAASISI YA USTAWI WA JAMII), Tamita Mwakitalu (CHUO CHA UTUMISHI WA UMA MAGOGONI), Jackline Everist (Chuo cha Usimamizi wa fedha IFM), Nasra Muna (Chuo cha Usimamizi wa fedha IFM) Laura Kwai (Iringa University), Mariam J Mwita (CHUO CHA UTUMISHI WA UMA MAGOGONI), Emmaculate Kasinsa (CHUO CHA UTUMISHI WA UMA MAGOGONI), Victoria Shiyo (CBE), Farida mlawa (UDOM), Lilian  Kaishozi (UDOM).


Wakati huohuo Msanii wa muziki wa kizazi kipya Hellen George Rubb pamoja na Navy Kenzo watatoa burudani katika shindano hilo kwa kiingilio katika shindano hili ni shilingi 50,000 kwa VIP pamoja na shilingi 10,000 kwa viti vya kawaida.

Kwa mawasiliano zaidi wasiliana na muandaaji wa TTCL Misss Higher Learning, Maya Kitambo - 0676806188

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »