KIWANDA CHA KUTENGENEZA NGUO CHA NIDA TEXTILES INDUSTIES CHATOZWA FAINI YA SHILINGI MILIONI THELATHINI, KWA UCHAFU NA UCHAFUZI WA MAZINGIRA

August 05, 2016
 Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh Luhaga Mpina akipata Maelezo kutoka kwa mmoja wa Maafisa wa kiwanda cha Urafiki Ttextile kilichopo jijini Dar es salaam mara baada ya kufanya ziara katika kiwanda hicho mapema hii leo.
 Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh Luhaga Mpina akikagua mto kibangu ambao umechafuliwa na maji yanayotiririshwa na kiwanda cha nguo cha Nida kilichopo tabata jijini dare s salaam.      
 Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mh. Luhaga Mpina (katikati)akitembezwa ndani ya kiwanda cha Urafiki Textile mara baada ya kufanya ziara katika kiwanda hicho mapema hii leo

                 EVELYN MKOKI AFISA HABARI
                    OFISI YA MAKAMU WA RAIS
                            DAR ES SALAAM
                                              4/8/2016

Kiwanda cha kutengeneza nguo cha Nida Textile Industries kilichopo Tabata Jijini Dar es Salaam kimetozwa faini ya shilingi milioni Thelathini kwa kosa la uchafuzi w a mazingira kwa kutiririsha maji taka na yenye sumu katika mto kibangu kuhatarisha maisha ya mazingira na viumbe hai  pamoja na kiwanda hicho kuwa na mazingira machafu na hivyo kuatarisha maisha ya wafanyakazi kiwandani hapo.

Faini hiyo inayotakiwa kulipwa ndani ya siku saba kwa Baraza la Taifa na Hifadhi na Usimamizi waMazingira NEMC imetokana na ziara ya Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina ya kukagua viwanda na mazingira nchini ambapo sambamba na adhabu hiyo kiwanda hicho kimetakiwa kufanya usafi mara moja katika mazingira kiwandani hapo, pamoja kupeleka repoti ya upimaji wa moshi, vumbi litokanalo na makaa ya mawe na maji yanayotoka kiwandani hapo ili serikali kujiridhisha kama si hatarishi kwa mazingira. 

‘’Ili kujiridhisha NEMC waje nao wachukue vipimo vya maji haya yanayotiririka ili tuone kama ni salama kwa mazingira na viumbe hai, na kiwanda kiwasilishe cheti cha utirishaji maji kwa Baraza.” Alisisitiza Naibu Waziri Mpina.

Kwa upande wake Meneja wa kiwanda hicho Bwana Mohamed Rajabu alipoulizwa kama ameikubali adhabu hiyo, alitupia lawama kwa NEMC na kusema kuwa wao ndo walitoa kibali cha athari ya tathimini ya mazingira kwa kiwanda hicho na ndiyo maana kinaendelea kufanya kazi na kuwa wangekuwa wanapita kwanza na kutoa onyo kwa wenye viwanda kabla ya kutoa adhabu kali ya mamilioni ya fedha, na kuongeza kuwa kukabiliana na faini kubwa hivyo kwa kiwanda hicho kunaweza kupelekea wafanyaki kupoteza ajira zao kwa kupunguzwa kazini.

Akiitimisha katika zoezi hilo Naibu waziri Mpina aliwataka wawekezaji na wenye viwanda nchini kutii sheria na kuthamini maisha ya wafanyakazi kwa kuyaweka mazingira safi na salama.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »