IBADA NA MAZISHI YA MWANAHABARI CHARLES SOKORO WA BARMEDAS TV YAFANYIKA JIJINI MWANZA.

July 20, 2016

Ibada ya Mazishi ya aliekuwa Mkuu wa Vipindi na Afisa Mahusiano katika kituo cha runinga cha Barmedas Tv cha Jijini Mwanza, Mwalimu Charles Sokoro, imefanyika jana katika Kanisa la AICT Makongoro na kufuatiwa na mazishi yaliyofanyika katika Makaburi ya Kitangiri.
 
Mwalimu Sokoro ambae pia alikuwa mwalimu wa muziki wa Injili na Mwenyekiti wa Kwaya ya AICT Makongoro, alifariki jumamosi Julai 16,2016 majira ya saa mbili usiku katika Hospitali ya Rufaa Bugando baada ya kuugua kwa miezi kadhaa.
Alizaliwa mwaka julai mosi mwaka 1965 katika Kijiji cha Kahunda Wilaya ya Sengerema mkoani Mwanza na hadi mauti yanamkuta alikuwa na umri wa 51 ambapo ameacha watoto wanne, alikuwa mgane.
Na BMG
Kwaya ya AICT Makongoro ikiimba katika ibada ya mazishi ya Sokoro
Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la AICT Makongoro akitoa salamu za rambirambi katika ibada ya mazishi ya marehemu Sokoro.
Baba Askofu Mkuu Mstaafu wa Kanisa la AICT Makongoro, akitoa salamu za rambirambi katika ibada ya mazishi ya marehemu Sokoro.
Mmoja wawanafamilia wa marehemu Sokoro akisoma wasifu wa marehemu Sokoro.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »