SIMIYU YAHAMASISHWA USAFI WA MAZINGIRA NA KUTUNZA MITI

May 01, 2016
Mhe Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Raisi Muungano na Mazingira Luhaga Mpina akifyeka majani katika eneo la kituo cha afya cha Mwandoya Kilichopo Wilayani Meatu, Mkoani Simiyu ikiwa ni JUmamosi ya mwisho wa mwezi. Jumamaosi Maalum ya Usafi.



Wananchi wa tarafa ya Mwandoya, wilayani Meatu Mkoani Simiyu wakifanya usafi wa mazingira kwa kufyeka katika eneo la kituo cha afya cha Wandoya  leo, ikiwa ni utekelezaji wa agizo la serikali la kufanya usafi wa mazingira na kutena jumamosi maalum ya mwisho wa mwezi kuwa ya usafi wa mazingira.

Katikati Naibu waziri Ofisi ya Makamu wa RAisi Muungano na Mazingira mhe LUhaga Mpina, pamoja na Diwani wa kata ya sakasaka (Chadema) bwana James Kazangula..wakielekea kumwaga majani yaliyofwekwa, Kulia ni Katibu waziri Bw. Dad Kolimba..pamoja na wanachi wa Mwandoya baada ya kufanya usafi katika kituo cha afya cha mwandoya mapema leo ikiwa ni utekelezaji wa agizo la serikali la kusafi wa mazingira kila jumamosi ya misho wa mwezi.



Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Raisi Muungano na Mazingira mhe. Luhaga Mpina akimwagilia mti baada ya kuupanda Wilayani Meatu Mkoani Simiyu Leo mara baada ya kuupanda.


EVELYN MKOKOI,SIMIYU 30/4/2016
 Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Raisi Muungano za Mazingira Mhe. Luhaga Mpina  ameshiriki usafi wa mazingira wa kila jumamosi ya mwisho wa mwezi, mara hii mkoani Simiyu katika wilaya ya Meatu  jimboni Kisesa.

Akizungumza na wananchi wa eneo la Mwandoya wilayani Meatu, Mhe. Mpina amewaasa wananchi wa mkoa wa Simiyu kwa ujumla kuitunza miti 4820  iliyopokelewa na kupandwa  wilayani hapo baada ya serikali ya awamu ya tano kutekeleza ahadi yake ya kuupatia Mkoa wa Simiyu idadi hiyo ya miti.

Naibu Waziri Mpina, alisema kuwa kwa kuwamkoa wa simiyu huko kwenye hatari kubwa ya kuwa janga na umesha wahi kukabiliwa na tatizo la uhaba wa chakula, kabla ya uchaguzi uliopita, kwa kuitunza miti hiyo ya matunda wakazi wa mkoa huo watanufaika na miti ya matunda  hayo ya muda mfupi kwa kufanya biashara ili kuweza kukuza uchumi na kuongeza kipato cha kila mmoja.

 Aliongeza kuwa, zoezi la upandaji miti mkoani simiyu katika ma shule, maeneo ya makazi ya watu na mashamba yanahitaji utunzani mkubwa kwani miti hiyo ina uwezo mkubwa wa kuboresha uoto wa asili ambao mpaka hivi sasa umetoweka.

Aidha Mhe. Mpina amewataka viongozi wa mkoa wa Simiyu kuchukua nafasi yao kusimamia wanachi wafanye usafi ikiwa ni agizo la serikali la kila mwisho wa mwezi kuwa siku ya usafi na kuwa viongozi ambao watakuwa wazembe katika suala zima la usimamiaji wa usafi wa mazingira watachukuliwa hatua.

Alipoongea na wanachi wa Jimbo La Kisesa, Naibu Waziri Mpina aliwaasa wananchi wa Kisesa wa sapoti jitihada za serikali za kupanda miti na kutunza mazingira, na kuwa hakikishia wapiga kura wake kuwa pamoja na kuwa Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, nafasi za kazi yake kama Mbunge wa jimbo hilo ipo pale pale na ataendelea kuwapigania wana Kisesa.

Aliwaomba wana Kisesa wawe mfano wa kupanda miti iliyotolewa na serikali na kuitunza na kwa aliokosa miche ya miti hiyo iliyogawiwa ame ahidi kuwapatia miche mingine kwani shabaya yake kubwa ni kuwezesha mkoa wa simiyu kupata miti hasa ya matunza na mbao ili kuboresha uchumi binafsi na pato la taifa.

Mhe. Mpina Amefanya usafi wa mazingira leo katika eneo la hospital ya Mwandoya pamoja na kupanda miti ikiwa ni sehemu ya utekekezaji wa kampeni ya kitaifa ya kupanda miti.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »