Mkurugenzi
Mkuu wa Tume ya Ushindani, Dkt. Fredrick Ringo akitoa maelezo mafupi
kwenye hafla ya makabidhiano ya vifaa vya muziki kwa Uongozi wa Jeshi la
Magereza. Hafla hiyo ilifanyikia Bwalo Kuu la Maafisa Magereza, Ukonga
Jijini Dar es salaam, Januari 29, 2016.
Mkurugenzi
Mkuu wa Tume ya Ushindani, Dkt. Fredrick Ringo akimkabidhi Kamishna
Jenerali wa Magereza John Casmir Minja gitaa la muziki ikiwa ni moja
wapo ya vifaa vya muziki vilivyokabidhiwa kwa Jeshi la Magereza.
Kamishna
Jenerali wa Magereza akijaribisha kupiga gitaa la muziki baada ya
kukabidhiwa vifaa vya muziki katika hafla ya makabidhiano ya vifaa hivyo
kutoka kwa Mkurugenzi wa Tume ya Ushindani, Dkt. Fredrick Ringo(wa
kwanza kulia).
Kamishna
Jenerali wa Magereza John Casmir Minja akitoa neno la shukrani kwa
Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani, Dkt. Fredrick Ringo kwenye hafla
ya makabidhiano ya vifaa vya muziki ambavyo vitatumika kukuza vipaji vya
Wanamuziki wa Jeshi la Magereza.
Maafisa
Waandamizi wa Jeshi la Magereza wakisikiliza kwa makini hotuba ya
Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani, Dkt. Fredrick Ringo(hayupo
pichani).
Baadhi
ya vifaa vya muziki venye vilivyokabidhiwa kwa Jeshi la Magereza kama
vinavyoonekana katika picha. Vifaa hivyo vitatumika kukuza vipaji vya
Wanamuziki wa Jeshi hilo(Picha na Kitengo cha Habari, Makao Makuu ya
Jeshi la Magereza).