Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi
amempongeza Theophil Makunga kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti mpya wa
Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) mwishoni mwa wiki.
Katika salamu hizo, Malinzi amempongeza Makunga kwa nafasi hiyo
aliochaguliwa na kusema imani waliyonayo wahariri wenzake juu ya
utendaji wake wa kazi ndio kumepelekea wao kumchagua kuongoza jukwa
hilo.
Aidha Malinzi amewapongeza Deodatus Balile aliyechaguliwa kuwa Makamu
Mwenyekiti na Neville Meena aliyechaguliwa kuwa Katibu Mkuu wa jukwaa
hilo na kuahidi kuwa TFF itaendelea kushirikiana nao.