“WATANZANIA WAASWA KUJIUNGA NA MIFUKO YA HIFADHI ZA JAMII”

January 26, 2016



.
WATANZANIA wameshauriwa kujiunga na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii iliyopo hapa nchini iili kuweza kupunguza ukali wa maisha kwani itawasaidia kuepukana na gharama za matibabu ambazo zitakuwa zikilipwa na mifuko husika wakati wanapokumbana na majanga mbalimbali.

Hayo yalisemwa mwishoni mwa wiki na Afisa Mwandamizi Rasilimali Watu na Utawala wa Mamlaka ya Usimamizi na Uzibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii nchini (SSRA),Amina Ally wakati wa semina ya kuhamasisha maafisa wa mageraza mkoani Tanga kuhusu umuhimu wa kujiunga na mifuko ya Hifadhi ya Jamii.


Alisema kuwa mifuko hiyo ina manufaa makubwa pamoja na kupunguza ukali wa maisha kwa watumishi wa kada mbalimbali na kulinda maslahi yao yakiwemo mahitaji ya kijamii ili kuweza kuondokana na gharama za matibabu wanapokuwa wakiugua na majanga mengine.

Aidha licha ya hivyo mifuko hiyo imekuwa na faida kubwa kwenye nchi katika uwekezaji inawafanya wanachama wa mifuko husika kupata unafuu katika upatikanaji wa masuala yote ya msingi wakati panapokuwa pamejitokeza mambo ya dharura na kwamba hukabiliana nayo bila kujali hali ya kipato au michango ya muhusika.

   “Ukiangali mifuko hii ya hifadhi ya Jamii imekuwa mkombozi mkubwa sana kwa jamii lakini pia inasaidia kuweza kukabiliana na ugumu wa maisha uliopo sambamba na kupunguza umaskini kwa watanzania waliojiunga nayo kwenye kunufaika na mambo mbalimbali ikiwemo huduma za matibabu “Alisema Amina.

Hata hivyo alitaja mifuko ambayo alidaia kuwa ndio kimbilio kubwa la watanzania walio wengi hapa nchini kuwa ni Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF), Mfuko wa Pensheni kwa watumishi wa Umma (PSPF),Mfuko wa Pensheni wa (PPF),Mfuko wa Pensheni wa Wafanyakazi wa Serikali (GEPF),Mfuko wa Pensheni wa (LAPF) na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF).

Alisema kuwa licha ya kupatikana mafanikio kwenye mifuko lakini zipo changamoto ambazo zinawakabili ikiwemo wafanyakazi wa sekta zisizokuwa rasmi kushindwa kujiunga kwenye Mifuko ya Hifadhi za Jamii hivyo aliwashauri washiriki wa semina hiyo kuhakikisha wanakuwa mabalozi wazuri kuielimisha jamii namna wanavyoweza kujiunga nayo ili waweze kunufaika.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »