DK. JOHN POMBE MAGUFULI AUNGURUMA JIJINI DAR ES SALAAM

October 22, 2015

????????????????????????????????????
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Dk. Jakaya Kikwete akiongozana na Dk. John Pombe Magufuli Mgombea Urais kupitia CCM wakati alipokutana kwenye uwanja wa ndege wa Mwalimu J. K, Nyerere Rais Jakaya Kikwete akielekea mkoani Ruvuma na Dk. John Pombe Magufuli akitokea mkoani Mwanza na kufanya mazunguzo mafupi uwanjani hapo kabla ya kuagana.
Dk. John Pombe Magufuli ameendelea na kampeni zake mkoani Dar es salaam ambapo amepokelewa na vyama mbalimbali vya kisiasa kwa kupamba bendera za vyama vyao kufuatia ujio wa mgombea huyo ambaye alikuwa akiendelea na kampeni zake za kuwania Ikulu ya Magogoni mikoani kabla ya kurejea jijini Dar es salaam kuendelea na kampeni hizo ambazo atazifunga rasmi kwenye uwanja wa CCM Kirumba mkoani Mwanza Oktoba 24 mwaka huu tayari kwa watanzania kumpigia kura za ndiyo.
Mgombea huyo amefanya mikutano ya kampeni katika majimbo ya Kigamboni, Mbagala, Temeke, Ubungo na Kinondoni huku akiwanadi wagombea ubunge na udiwani wa majimbo hayo, Uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani unatarajiwa kufanyika jumapili Oktoba 25 mwaka huu.(PICHA NA JOHN BUKUKU-FULLSHANGWE-DAR ES SALAAM)
????????????????????????????????????
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Dk. Jakaya Kikwete akiagana na Dk. John Pombe Magufuli Mgombea Urais kupitia CCM wakati alipokutana kwenye uwanja wa ndege wa Mwalimu J. K, Nyerere mara baada ya mazungumza yao.
????????????????????????????????????
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Dk. Jakaya Kikwete  na Dk. John Pombe Magufuli Mgombea Urais kupitia CCM   wakati alipokutana kwenye uwanja wa ndege wa Mwalimu J. K, Nyerere
????????????????????????????????????
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Dk. Jakaya Kikwete  na Dk. John Pombe Magufuli Mgombea Urais kupitia CCM wakitaniana na mpiga picha wa gazeti la Jambo Leo Bw. Richard Mwaikenda wakati  kwenye uwanja wa ndege wa Mwalimu J. K, Nyerere.
????????????????????????????????????
Dk. John Pombe Magufuli Mgombea Urais kupitia CCM akiwahutubia wananchi na kuomba kura za ndiyo kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye uwanja wa Biafra Kinondoni jijini Dar es salaam
????????????????????????????????????
Baadhi ya wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye uwanja wa Biafra Kinondoni jijini Dar es salaam.
????????????????????????????????????
Jaji mstaafu Joseph Sinde Warioba akimpigia debe Dk. John Pombe Magufuli kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika kwenye uwanja wa Biafra Kinondoni jijini Dar es salaam.
????????????????????????????????????
Dk. John Pombe Magufuli Mgombea Urais kupitia CCM akisisitiza jambo katika mkutano huo.
????????????????????????????????????
Baadhi ya wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika Sinza katika jimbo la Ubungo jijini Dar es salaam.
????????????????????????????????????
Dk. John Pombe Magufuli Mgombea Urais kupitia CCM akiwasili kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika Sinza jimbo la Ubungo jijini Dar es salaam leo.
????????????????????????????????????
Dk. John Pombe Magufuli Mgombea Urais kupitia CCM akipokelewa kwa shangwe na mapambo ya bendera za vyama mbalimbali zilizopambwa kuanzia Ubungo mataa mpaka kituo cha mabasi cha ubungu kufuatia ujio wa mgombea huyo jijini Dar es salaam kwa ajili ya mikutano ya kampeni.
????????????????????????????????????
Dk. John Pombe Magufuli Mgombea Urais kupitia CCM akiwanadi wagombea ubunge na udiwani jimbo la Mbagala kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika uwanja wa Zakhem Mbagala jijini Dar es salaam.
????????????????????????????????????
Umati wa wananchi waliojitokeza katika mkutano wa kampeni wa CCM kwenye uwanja wa Zakhem Mbagala.
????????????????????????????????????
Mgombea Udiwani kata ya Kimbangulile Ndugu Said Fella wa kwanza kushoto akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wagombea wenzake.
????????????????????????????????????
Makada wa CCM wakifurahia Kampeni kwenye uwanja wa Biafra.
????????????????????????????????????
Mbagala Zakhem ikiwa imetema.
????????????????????????????????????
Baadhi ya wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika uwanja wa Machava Kigamboni leo.
????????????????????????????????????
Dk. John Pombe Magufuli Mgombea Urais kupitia CCM akimnadi mgombea ubunge jimbo la Kigamboni Dk. Faustine Ndugulile
????????????????????????????????????
Dk. John Pombe Magufuli Mgombea Urais kupitia CCM akimkabidhi ilani ya uchaguzi na kumnadi mgombea ubunge jimbo la Kigamboni Dk. Faustine Ndugulile.
????????????????????????????????????
Dk. John Pombe Magufuli Mgombea Urais kupitia CCM akiwanadi wagombea ubunge jimbo la Kinondoni  Ndugu Idd Azzan na wagombea wa viti maalum kutoka kushoto na Mama Madabida na Mama Janet Masaburi.
????????????????????????????????????
Dk. John Pombe Magufuli Mgombea Urais kupitia CCM akimnadi na kumkabidhi ilani ya uchaguzi mgombea ubunge Kinondoni Ndugu Idd Azzan.
????????????????????????????????????
Kundi la Orijino Komedi likifanya vitu vyake jukwaani kwenye mkutano wa kampeni wa CCM uliofanyika kwenye uwanja wa Biafra huku Dk. John Pombe Magufuli Mgombea Urais kupitia CCM na viongozi wengine  wakiangalia.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »