Na Mwandishi Wetu,Muheza
JESHI la Polisi mkoa wa Tanga linamshikilia mkulima
mmoja na mkazi wa Kijiji cha Machemba wilayani Muheza John Dastan (30) kwa
tuhuma za kuhusika na mauaji ya Abdi Godatha (54) kwa kumpiga fimbo kichwani.
Akitoa taarifa hiyo ofisini kwake jana,Kamanda wa
Polisi mkoa wa Tanga Zuberi Mwombeji alisema lilitokea Septemkba 28 mwaka huu
majira ya saa 5.00 usiku huko kwenye kilabu cha pombe katika kijiji cha
Machemba Kata ya Mkanyageni.
Kamanda Mwombeji alisema kwamba indaiwa siku ya
tukio marehemu ambaye alikuwa akinywa na mtuhumiwa waliingia katika ubishani na
ndipo Dastan alipochukua fimbo na kuanza kumpiga nazo maeneo ya kichwani.
“Chanzo kiuu cha mauaji hayo kwa uchunguzi wetu wa
awali ni kutokana na ulevi huyu mtuhumiwa alikuwa amelewa na waliingia ubishani
na marehemu na ndipo Dastan alipochukua fimbo na kumpiga nazo marehemu kichwani
na kusababisha kifo chake”,alisema Mwombeji.
Hata hivyo alisema kuwa Polisi inaendelea na
uchunguzi wa mauaji hayo na mtuhumiwa anatarajiwa kufikishwa mahakamani mara
baada ya upelelezi kukamilika.
Kamanda Mwombeji alitoa wito kwa wakazi wa mkoa huo
kuacha kujichukulia sheria mkononi kwani kitendo cha kupigana hadharani ni
makosa kwa mujibu wa sheria.
EmoticonEmoticon