Meneja
Mauzo na Masoko wa Kampuni ya Nuebrand EC, Cathreen Bukuku (kushoto),
akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam leo
asubuhi, kuhusu kongamano la wiki ya huduma za kifedha na uwekezaji
litakalofanyika Agosti 28 hadi 30 mwaka huu, viwanja vya Mnazi Mmoja
jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mkufunzi na Mratibu wa Mipango wa Kampuni
hiyo, Daniel Wadelanga. Kongamano hilo limeandaliwa na Kampuni ya
Nuebrand EC.
Mjumbe
wa Timu ya Mauzo wa Benki ya Uba United Bank for Africa, Tesha Filemon
(katikati), akizungumza katika mkutano huo kuhusu kazi mbalimbali
zinazofanywa na benki hiyo.
Meneja
wa Tawi la Kariakoo wa Benki ya The Peoples Bank of Zanzibar Ltd, Badru
Idd (wa pili kushoto), akizungumza katika mkutano huo kuhusu benki hiyo
na matawi yake.
Ofisa
Usanifu Bidhaa na Usimamizi wa Sharia Amana Benki, Jaffari Kesowani
(kulia), akizungumza na wanahabari kuhusu kazi mbalimbali zinazohusiana
na na benki hiyo.
Mkuu wa Mauzo na Usambazaji wa Jubilee Life Insurance, Adam Samson Namuhisa (kushoto), akizungumza katika mkutano huo.
Msimamizi
wa Masoko wa Kampuni ya Avic Town, Daniel Kure (kulia), akielezea kadhi
kadhaa zinazofanywa na kampuni hiyo katika mkutano huo. Kushoto ni
maofisa wa kampuni hiyo.
Meneja
Masoko na Uhusiano wa Kampuni ya Covenant Bank, Mhina Semwenda
(kulia), akizungumzia shughuli zinazofanywa na benki hiyo.
Wadau mbalimbali kutoka taasisi za kifedha wakiwa
kwenye mkutano huo.