TAARIFA YA MAFANIKIO YA JESHI LA MAGEREZA KATIKA KIPINDI CHA SERIKALI YA AWAMU YA NNE(MWAKA 2005 – 2015)

July 08, 2015

download (5)
1.0       UTANGULIZI
1.1.0   Historia ya Jeshi la Magereza Tanzania Bara
Jeshi la Magereza lilianzishwa rasmi mwezi Agosti 25, 1931, Dhima yake kuu ni kuchangia ipasavyo katika kuimarisha usalama wa jamii kupitia usimamizi wa kifungo na huduma za mahabusu, utekelezaji wa program za urekebishaji wa wahalifu na kutoa ushauri wa kisera kuhusu uzuiaji wa wahalifu.
  • Majukumu na malengo ya Jeshi la Magereza
Jukumu la msingi la Jeshi la Magereza ni kuwahifadhi wafungwa na mahabusu wa aina zote na jukumu la urekebishaji wa tabia za wafungwa pia hufanyika kupitia program za mafunzo kwa njia ya vitendo katika miradi ya kilimo, viwanda vidogo vidogo na ujenzi. Vile vile, ushauri nasaha hutolewa kwa wafungwa kwa kutumia waalimu wa dini na maafisa ustawi wa jamii pale inabainika kuhitajika kulingana na hali ya mfungwa husika.
2.0       MAFANIKIO
  • Katika utekelezaji wa majukumu yake katika kipindi cha Serikali ya awamu ya nne mwaka 2005 hadi 2015 Jeshi limepata mafanikio katika maeneo makuu kama yafuatayo:-
  • Uimarishaji wa Magereza yenye Ulinzi Mkali (Central Prison)
Mfano ukarabati wa majengo na uboreshaji wa miundo mbinu ya Magereza yenye ulinzi mkali umefanyika katika Magereza ya Butimba, Uyui, Lilungu, Maweni, Isanga, Keko na Ukonga.
  • Ujenzi, ukamalishaji, upanuzi wa majengo ya Ofisi
Mfano, Ujenzi wa Ofisi za Wakuu wa Magereza Mikoa ya Singida, Ofisi ya Magereza Mkoa wa Dar Es Salaam unaendelea na ukarabati wa Jengo la Makao Makuu ya Magereza lililoanza rasmi kutumika Desemba 31, 2007.
  • Ujenzi wa nyumba za askari
Mfano, ghorofa la kuishi askari takribani familia 16 mkoani Iringa, ujenzi wa nyumba za maofisa na askari unaendelea kufanyika katika Magereza mbalimbali nchini.
  • Maji safi na maji taka Magerezani
Uimarishaji wa miundombinu ya maji safi umefanyika katika Magereza ya Kwamngumi, Kambi Kimbiji, Kikosi Maalum (KMKGM), kambi Chikuyu, Segerea na sehemu zingine unaendelea
  • Kupunguza Msongamano Magerezani
Jeshi la Magereza katika jitihada za kupunguza msongamano Magerezani limefanikiwa kuongeza uwezo wa magereza kutunza wahalifu kutoka nafasi 22,699 zilizokuwapo mwaka 2005 hadi nafasi ya 29,552 zilizopo sasa. Ongezeko hili la nafasi za kulala wafungwa 6,853 ni sawa na asilimia 30.2 ya nafasi zilizokuwepo kabla mwaka 2005.
  • Kuimarisha Viwanda vidogo vidogo
Jeshi la  Magereza limeendelea kuimarisha Viwanda vidogo vidogo kwa kuendelea na ufungaji wa mashine katika karakana ya Uhunzi Ukonga, kiwanda cha viatu Karanga Moshi, nakadhalika.
  • Kuimarisha Mashamba ya Kilimo na Mifugo
Jeshi la Magereza linahudumia ng’ombe wa nyama, wa maziwa pamoja na Mbuzi, Kondoo, Nguruwe, Sungura, Kuku wa mayai na Bata weupe. Aidha, Jeshi la Magereza lina mashamba ya mbegu  bora za kilimo kwa kushirikiana na Wakala wa Mbegu za Kilimo nchini Agricultural Seed Agency (ASA) katika mikoa ya Arusha, Dodoma, Manyara, Lindi, Iringa, Mbeya, Kilimanjaro na Morogoro
  • Matumizi ya Nishati mbadala Magerezani
Jeshi limeendelea na juhudi zake za kupunguza matumizi ya kuni na badala yake kutumia nishati mbadala kama vile gesi itokanayo na tungamotaka (Biogas) na Makaa ya mawe kwa upikaji wa chakula cha wafungwa
  • Mafunzo mbalimbali
Mafunzo mbalimbali yaliendeshwa ndani ya Jeshi  la Magereza na watumishi 7,683 walihitimu kozi mbalimbali, kwa upande wa mafunzo katika vyuo vya nje ya Jeshi watumishi 519 wamehitimu masomo ya  taaluma. Aidha, watumishi wa kada mbalimbali wapatao 169 wamepata fursa ya kusafiri nje ya nchi kwa ajili ya mafunzo mbalimbali au kushiriki kwenye vikao vya kimataifa.
  • Usafirishaji Mahabusu
Jeshi limepanua utekelezaji wa jukumu la kuwapeleka mahabusu Mahakamani kusikiliza kesi. Zoezi hilo lilianza rasmi tarehe 19 Mei, 2008 kwa Mikoa  ya Dar es Salaam na Pwani. Kwa sasa zoezi hilo linaendelea katika Mkoa wa Arusha na baadhi ya Wilaya za Mkoa wa Dodoma.
  • Utoaji wa Huduma za Afya
Kwa kushirikiana na Shirika la PharmAccess International, New life in Christ na baadhi ya Halmashauri hapa nchini tumefaninikiwa kujenga Zahanati na Vituo vya Afya katika mikoa Ishirini (20).
  • Kuwawezesha askari na watumishi kupambana na umaskini
Jeshi limeendelea na mchakato wa kufungua Maduka ya Bidhaa zisizolipiwa kodi (Duty Free Shops) ili kupunguza makali ya maisha kwa watumishi wa Jeshi la Magereza na familia zao. Maduka ya aina hii yamefunguliwa Ukonga – Dar es Salaam, Gereza Isanga – Dodoma, Gereza Karanga – Moshi, Chuo KPF – Morogoro, Gereza Butimba – Mwanza, Gereza Ruanda – Mbeya, Gereza Keko na Gereza Uyui – Tabora.
  • Uhifadhi wa Mazingira
Hadi kufikia Aprili, 2015 miti 4,321,450 imepandwa nchi nzima na katika Miradi maalumu inayofadhiliwa na mashirika mbalimbali kwa mfano UNDP/NORAD ikishirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii Idara ya Tanzania Forestry Fund  (TFF) katika magereza ya Isupilo, Msalato, Idete, Mgagao, Kambi Mkwaya, Kambi Ihanga.
 Imetolewa na:
Kitengo cha Habari na Mawasiliano,
Makao Makuu ya Jeshi la Magereza,
DAR ES SALAAM
8 Julai, 2015

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »