NHIF YAENDELEA NA MPANGO WAKE WA KUPELEKA MADAKTARI BINGWA KATIKA MIKOA YA PEMBEZONI.

June 01, 2015

1 
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Bi. Fatma Ali akizungumza na wananchi kabla ya kuzindua mpango wa kupeleka madaktari Bingwa katika mikoa ya pembezoni ili kuwapunguzia wananchi mzigo wa kusafiri umbali mrefu kwenda kufuata huduma hizo katika hospitali kubwa,
2
2. Mwakilishi wa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Bwana Raphael Mwamoto, akitoa maelezo kuhusu mpango wa Madaktari Bingwa wanaopelekwa mikoani na Mfuko huo.
3
Baadhi ya wakazi wa Mtwara wakisubiri huduma za madaktari Bingwa,
4
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Bi. Fatma Ali akiwa katika picha ya pamoja na madaktari Bingwa baada ya kuzindua rasmi huduma ya madaktari Bingwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mtwara,
…………………………………………………………………………………………….
Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya NHIF unaendelea na mpango wake wa kupeleka madaktari Bingwa katika mikoa ya pembezoni ili kuwapunguzia wananchi mzigo wa kusafiri umbali mrefu kwenda kufuata huduma hizo katika hospitali kubwa. Mpango huo pia unalenga kuwajengea uwezo wa kiutendaji madaktari walioko katika hospitali za mikoani ambao watafanya kazi pamoja na madaktari bingwa hao. Madaktari waliokwenda Mtwara ni pamoja na wagonjwa ya akinamama,m magonjwa ya ndani, bingwa wa upasuaji na bingwa wa dawa za usingizi. Zoezi hilo litadumu kwa muda wa siku sita.
Akizindua zoezi hilo Kaimu Mkuu wa mkoa wa Mtwara Bi. Fatma Ali amewahimiza wananchi wa mkoa wa Mtwara kujiunga na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya na Mfuko wa Afya ya Jamii CHF ili kuujengea uwezo zaidi Mfuko huo kupeleka huduma za kibingwa katika mikoa mingi zaidi.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »