MULONGO AZINDUA MASHINDANO YA U13 TAIFA

June 08, 2015


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mh Magessa Mulongo leo hii kwenye uwanja wa CCM Kirumba amefungua mashindano ya Taifa ya vijana umri chini ya miaka 13.

Akifungua mashindano haya Mh Mulongo amewataka vijana hao kujituma katika michezo na masomo kwa kuwa vyote vinakwenda sambamba.

Amelisisitizia Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania TFF kuongeza juhudi katika kuimarisha soka la vijana.

Katika salam zake za utangulizi Rais wa TFF Jamal Malinzi ameeleza kuwa lengo la mashindano haya ni kuibua timu ya vijana wa umri wa miaka 13 ambao watahamishiwa kwenye shule ya Alliance, watakua pamoja hapo kusoma na kufundishwa mpira.

Mpango wa TFF ni kuwa hadi kufikia mwaka 2019 timu hii itakuwa imara kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya fainali za Afrika umri chini ya miaka 17,fainali ambazo zitafanyika Tanzania.

Mikoa yote 25 ya Tanzania bara inashiriki mashindano haya na mkoa wa Dar es salaam umewakilishwa na timu tatu Kinondoni Ilala na Temeke.

TFF inaishukuru Symbion Power kwa ushirikiano wa kuendeleza mpira wa vijana

NB: Picha za uzinduzi zimeambatanishwa

IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF) 

-
Best Regards,
 
Baraka Kizuguto
MEDIA & COMMUNICATION OFFICER
Tanzania Football Federation - TFF
A:I P.O.BOX 1574 Karume Memorial Stadium /Shaurimoyo/Uhuru Street I Dar es salaam I Tanzania  
 

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »