Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasha mtambo wa maji uliojengwa
Chato Mlimani kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji utakaohudumia
wakazi wa mji huo leo wakati wa ziara yake katika mkoa wa Geita , Kinana
anaendelea na ziara hiyo ya kikazi mkoani humo baada ya kumaliza ziara
kama hiyo mkoani Kagera jana, Kinana anaendelea na ziara hiyo
yenye lengo la kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka
2010-2015 na kuhimiza uhai wa chama, kukosoa na kutatua matatizo
mbalimbali yanayokabili wananchi kwa maisha na maendeleo yao kwa ujumla
akiongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi.(PICHA NA
KIKOSI CHA FULLSHANGWE-CHATO-GEITA)
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na Mkuu wa wilaya ya Chato
Rodrick Mpogolo kulia wakipiga makofi mara baada ya kuwashwa rasmi kwa
mtambo huo.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana, Rodrick Mpogolo Mkuu wa wilaya ya
Chato na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi pamoja na viongozi
wa CCM wilaya ya Chato wakipunga mikono na wanaCCM mbalimbali katika
picha ya pamoja.
Baadhi ya wananchi wakigombea kupanda gari kwa ajili ya kuhudhuria mkutano wa hadhara uliofanyika mjini Chato.
Baadhi
ya akina mama wakiwa na ndoo zao tayari kwa kuchota maji mara baada ya
kuzindua rasmi mtambo wa maji Chato Kilimani ambao utahudumia wakazi wa
mjini Chato na baadhi ya vijiji.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimtwisha ndoo ya maji Paulina Sabinati mara baada ya uzinduzi wa mradi huo.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana pamoja na Mkuu wa wilaya ya Chato
Ndugu Rodrick Mpogole, viongozi wa CCM wilaya ya Chato pamija na
mafundi wa Tanesco akishiriki kutandaza waya za umeme katika mradi wa
umeme vijijini REA katika kijiji cha Mkungo.
Msafara
wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana ukisimama baada ya
wananchi wa kijiji cha Mkaurugusi wilayani Chato wakati akielekea kijiji
cha Ihanga.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisoma mabango ya wananchi
waliosimamisha msafara wake wakiomba awasaidia kufanikisha mpango wa
kuwawekea umeme katika kijiji chao cha Makurugusi ambacho laini ya umeme
kuelekea kijiji cha jirani imepitia.
Mwakilishi
wa wananchi hao wa kijiji cha Makurugusi Bw. Shampinga David akielezea
masikitiko ya wananchi hao kutokana na mpango wa umeme vijijini kupita
kijiji chao bila kuwawekea umeme huo Bw. Shampinga amemuomba Kinana
kuhakikisha anawasaidia na wao wanapata umeme katika kijiji chao.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi hao.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipeana tano na wananchi hao mara
baada ya kuwaahidi kuongea na Waziri wa Nishati na Madini ili kijiji
hicho kiwekewe umeme vijiji REA ambapo wanakijiji hao walijawa na
furaha mara baada ya kusikia kauli hiyo kutoka kwa kiongozi huyo wa juu
wa CCM.
Baadhi
ya wananchi wakiwa wamepanda kwenye pikipiki wakielekea kwenye mkutano
wa Kinana katika kijiji cha Ihanga ambako alishiriki katika ujenzi wa
nyumba ya daktari.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiangalia ngoma mara baada ya kuwasili katika kijiji cha Ihanga.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki katika ujenzi wa nyumba
ya daktari katika kijiji cha Ihanga wilayani Chato.
Nape
Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi akipungia mkono wananchi mara
baada ya kuwasili kwenye mkutano wa hadhara mjini Chato.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwasili kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika mjini Chato.
Kwaya ikiimba wakati wa mapokezi ya Katibu Mkuu wa CCM mjini Chato alipowasili katika mkutano wa hadhara.
Wananchi wakinyanyua mikono yao juu juu kumkaribisha Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
Mkuu wa wilaya ya Chato Ndugu Rodrick Mpogolo akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara mjini Chato.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Ndugu Nape Nnauye akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika
Baadhi
ya wananchi wakiwa juu ya magari wakifuatilia hotuba za viongozi
mbalimbali katika mkutano wa hadhara wa CCM uliofanyika mjini Chato
mkoani Geita leo.
Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi akihutubia mkutano wa hadhara mjini Chato.
Nape akisisitiza jambo wakati akihutubia mkutano huo.
Umati wa wananchi ukiwa katika mkutano huo.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia katika mkutano huo.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisisitiza jambo katika mkutano huo.
Baadhi ya wananchi wakirejea nyumbani mara baada ya kumalizika kwa mkutano huo.