Washindi watapatikana kwa asilimia
100 ya kura za wananchi zinazoendelea katika hatua hii ambapo wamebaki
washiriki watatu katika kila kipengele.
Kila mshindi atapokea tuzo na zawadi
ya fedha taslimu shilingi milioni moja.
Pamoja na utoaji wa tuzo hizo, hafla
hiyo itasindikizwa na burudani moto moto kutoka kwa wasanii watakaotangazwa
hapo baadaye. Hakuna kiingilio kwenye tuzo hizo bali itatolewa mialiko kwa
baadhi ya watu kwenye tasnia ya burudani na zingine nchini. Pia mialiko 100
itatolewa kwa wananchi waliopiga kura zaidi.
Haya ndio majina yaliyoingia kwenye fainali ya tuzo za watu:
Mtangazaji wa redio
anayependwa
D’Jaro Arungu - TBC FM - TZW1C
Maryam Kitosi – Times FM - TZW1D
Millard Ayo – Clouds FM - TZW1E
Kipindi cha redio
kinachopendwa
Amplifaya – Clouds FM - TZW2B
Hatua Tatu – Times FM - TZW2C
Papaso – TBC FM - TZW2D
Mtangazaji wa runinga anayependwa
Abdallah ‘Dullah’ Ambua – EATV -
TZW3A
Salama Jabir – EATV/Maisha Magic -
TZW3B
Salim Kikeke - BBC Swahili - TZW3C