Serikali yawashauri Vijana Mkoani Ruvuma kujishughulisha na ujasiriamali

May 14, 2015

1
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Bw. Nachoa Zacharia kulia akiongea na ujumbe kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wakati wa Maafisa hao walipokuwa katika ziara ya mafunzo stadi za maisha,ujasiriamali na elimu ya uongozi kwa vijana wa Mkoa wa Ruvuma, kushoto kwake ni Mkuu wa Chuo cha Vijana cha Sasanda kilichopo mkoani Mbeya Bw. Laurian Masele.(Picha na Benjamin Sawe)
2
Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Mh. Charles Mhagama akisisitiza jambo kwa maafisa kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wakati wa ziara ya mafunzo ya stadi za maisha,ujasiriamali, mfuko wa Vijana na elimu ya uongozi kwa vijana wa Mkoa wa Ruvum, kulia Afisa Vijana kutoka Wizarani Bi. Amina Sanga na kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Sheria Bi. Ester Riwa.(Picha na Benjamin Sawe)
3
: Afisa Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, na Michezo Bi. Amina Sanga akitoa mada ya jinsi ya Vikundi vya vijana wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea vilivyokidhi vigezo vinavyoweza kunufaika na mfuko huo,mafunzo hayo yamefanyika mkoani Ruvuma.(Picha na Benjamin Sawe)
4 (2)
Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Sheria Bi. Ester Riwa akitoa mada juu ya Sera ya Maendeleo ya Vijana ya Mwaka 2007, Stadi za Maisha na ujasiriamali kwa Vijana wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma.(Picha na Benjamin Sawe).

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »