Rais
wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi
amewaagiza wasimamizi wa vituo vya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuhakikisha
sheria na taratibu zote za mechi zinafuatwa.
Ligi
Kuu ya Vodacom (VPL) msimu huu 2014/2015 inafikia tamati kesho (Mei 9,
2015) ambapo timu zote 14 zitakuwa viwanjani katika mechi ambazo ndizo
zitakazotoa hatma ya timu zinazoshuka daraja.
Mechi
hizo zitakuwa kati ya Ndanda na Yanga (Uwanja wa Nangwanda Sijaona,
Mtwara), JKT Ruvu na Simba (Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam), Azam na
Mgambo Shooting (Azam Complex, Dar es Salaam), Stand United na Ruvu
Shooting (Uwanja wa Kambarage, Shinyanga), Kagera Sugar na Tanzania
Prisons (Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza), Mbeya City na Polisi Morogoro
(Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine, Mbeya), na Mtibwa Sugar na Coastal
Union (Uwanja wa Manungu, Morogoro).
KUMRADHI WANAHABARI
Katibu
Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini TFF, Mwesigwa Selestine
ameomba radhi kwa vyombo kufuatia madai ya waandishi wa habari kupata
usumbufu wakati wa utoaji wa Zawadi kwa Mabingwa na washindi wa pili wa
Ligi Kuu ya Vodacom.
Mwesigwa
alisema kwa niaba ya TFF anaomba radhi kwa usumbufu wowote uliowapata
waandishi na wadau wote walioshindwa kushuhudia vema tukio hilo.
“TFF
na FIFA vinatambua umuhimu na nafasi ya wanahabri na vyombo vya habari
si tu katika kuutangaza mchezo, bali pia katika kutia chachu maendeleo
ya mchezo wenyewe “ alisema Mwesigwa.
Hali
mbaya ya hewa ilivuruga utaratibu uliokuwa umepangwa awali kuanzia
itifaki ya shughuli za kabla na wakati wa mchezo na zile za utoaji tuzo.
Aidha
Mwesigwa alisema TFF itaendelea kushirikiana vema na jumuiya ya
wanahabari ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kwamba wana mazingira mazuri
wanapofanya kazi kwenye matukio ya mpira wa miguu.
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)