Mkutano wa tatu wa Shirikisho la Vyama vya Wataalamu wa Masuala ya Chakula na Lishe Afrika

May 20, 2015


VY2
Rais wa Chama cha Chakula na Lishe Tanzania (FONATA) Prof. Joyce Kinabo (katikati) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani leo jijini Dar es Salaam, kuhusu Mkutano wa tatu wa Shirikisho la Vyama vya Wataalamu wa Masuala ya Chakula na Lishe Afrika ambao unalenga kutoa fursa kwa wanasansi wa masuala ya lishe ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Kikwete. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Chakula na Lishe Dkt. Joyceline Kaganda na Afisa Mawasiliano wa taasisi hiyo Herbert Gowelle (kushoto).
VY3
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Chakula na Lishe Dkt. Joyceline Kaganda akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) leo jijini Dar es Salaam, kuhusu namna taasisi hiyo inavyotekeleza majukumu yake kwa kuzingatia umuhimu wa lishe nchini kama moja ya masuala muhimu ya kimaendeleo. Kushoto ni Rais wa Chama cha Chakula na Lishe Tanzania (FONATA) Prof. Joyce Kinabo.
VY4
Rais wa Chama cha Chakula na Lishe Tanzania (FONATA) Prof. Joyce Kinabo akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) leo jijini Dar es Salaam, kuhusu kupunguza viwango vya ukondefu kwa watoto walio chini ya umri wa miaka mitano kwa asilimia 50 mwishoni mwa mwaka huu. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa taasisi hiyo Dkt. Joyceline Kaganda.
VY1
Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia mkutano wa taasisi ya chakula na lishe uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »