WAZIRI WA AFYA DR.SEIF RASHID MGENI RASMI MAADHIMISHO YA SIKU YA UTEPE MWEUPE TANGA.

March 13, 2015

NA MWANDSHI WETU,TANGA

Waziri wa Afya Dkt Seif Rashid anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika kilele cha maadhimisho ya siku ya utepe mweupe.


WAZIRI WA AFYA NCHINI,DR.SEIF RASHID
MKUU WA MKOA WA TANGA,SAID MAGALULA AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI KUHUSU MAADHIMISHO HAYO

Maadhimisho hayo kwa mwaka huu yanafanyika mkoani Tanga katika viwanja vya Tangamano.
 

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Magalula Said Magalula wakati akiongea na waandishi wa habari hapo jana.
 

   

WAANDISHI WA HABARI WAKIWAJIBIKA,KUSHOTO NI AMINA OMARI KUTOKA GAZETI LA MTANZANIA,


Alisema kuwa maadhimisho hayo yatakwenda sambamba na upimaji wa hiari wa saratani ya shingo ya kizazi na matiti.
 

Aliongeza kuwa pia siku hiyo wananchi wa Tanga watapata fursa ya kuchangia damu kwa ajili ya kutumika kwenye vituo vya afya mkoani hapo.


"Niwaombe wananchi wa Tanga kujitokeza kwa wingi katika kilele cha maadhimisho hayo"alisisitiza Magalula

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »