Mwenyekiti
wa Shirika la World Doctors kutoka Itali Bi. Tanya Niestedt (kulia)
akizungumza na Waganga wa Tiba asili hawapo pichani katika semina ya
siku moja ya yakuwataka waganga hao washirikiane na Madaktari katika
kutibu magonjwa ya Kisukari na Presha, kushoto ni Mkuu wa kitengo cha
maradhi yasiyo ambukiza Zanzibar Dkt. Omar Mwalim, hafla hiyo imefanyika
ukumbi wa Wizara ya Afya Mnazi mmoja Mjini Zanzibar.
Mkuu
wa kliniki ya Kisukari Hospitali ya Mnazi mmoja Dkt. Faiza Kassim
(aliesimama) akizungumza na Waganga wa tiba asili na tiba mbadala kuhusu
mashirikiano ya utibabu wa magonjwa ya kisukari na presha.Ili kuepuka
mgonjwa mmja kutumia dawa za Hospitali na zile zinazotolewa na waganga
hao.
Mmoja
wa Waganga wa Tiba asili Bi. Zahra Hassan Ali akichangia katika semina
hiyo iliyofanyika ukumbi wa Wizara ya Afya mnazi mmoja Mjini Zanzibar.
Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar.