Prof. Tolly Mbwette aagwa mkoani Manyara

March 14, 2015

Mwenyekiti wa Serikali ya wanafunzi wa chuo kikuu huria kituo cha Manyara, Mwalimu Pasian Siay akizungumza wakati wa hafla ya kumuaga Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu huria (OUT) Profesa Tolly Mbwette, iliyofanyika jana mjini Babati.
Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Dk Joel Nkaya Bendera, akizungumza jana mjini Babati wakati wa kumuaga Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu huria (OUT) Profesa Tolly Mbwette, (kushoto) na aliyepo kulia ni Mkuu wa wilaya ya Babati Crispin Meela.
Mkurugenzi wa chuo kikuu huria kituo cha Manyara Dk Joseph magali (kushoto) akimpongeza Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu huria nchini (OUT) Profesa Tolly Mbwette (kulia) baada ya kuvikwa vazi la jadi la jamii ya watu wa mkoa wa Manyara jana, kwenye hafla ya kumuaga profesa huyo ambaye amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa vyuo vikuu vya Afrika nzima.
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu huria nchini (OUT) Profesa Tolly Mbwette (kulia) akikabidhiwa cheti cha heshima jana na Mkurugenzi wa chuo kikuu huria kituo cha Manyara kwenye hafla ya kumuaga profesa huyo ambaye amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa vyuo vikuu vya Afrika nzima.
Mkuu wa Wilaya ya Babati Mkoani Manyara, Crispin Meela, akizungumza kwenye hafla ya kumuaga Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu huria (OUT) Profesa Tolly Mbwette, iliyofanyika jana mjini Babati.
Baadhi ya wakazi wa Mjini Babati Mkoani Manyara waliohudhuria hafla ya kumuaga Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu huria (OUT) Profesa Tolly Mbwette, alipoagwa jana kwenye kituo cha chuo hicho mjini Babati.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »