Mkuu
wa Majeshi ya Ulinzi ya Tanzania mstaafu . Jenerari Mrisho Sarakikya
akisalimiana na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana wakati
alipotembelea kata ya Sing’isi na kuaslimiana na wananchi akiwa katika
ziara yake ya kikazi mkoani Arusha yenye lengo la Kukagua Ilani ya
Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 inayotekelezwa na serikali kwa pamoja na
wananchi na kuhamasisha uhai wa chama cha Mapinduzi , Katika ziara hiyo
Kinana anaongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi.
Katika Mkutano wa hadhara
uliofanyika kata ya Mbunguni akiwahutubia wananchi katika mkutano huo
Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi amemshutumu Waziri wa
Maliasili na Utalii Mh. Lazaro Nyalandu kwa kutosikiliza
ushauri alioutoa Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahman
Kinana akiwa wilayani Loliondo na Ngorongoro kwa mawaziri ambao wizara
zao zinahusika moja kwa moja katika maamuzi na kushughulikia matatizo ya
migogoro ya Ardhi mkoani Arusha ambapo kumekuwa na migogoro karibu
wilaya zote, kati ya mbuga za wanyama na vijiji ama kati ya vijiji na
vijiji.
Nape amesema wakati waziri wa
Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mh. William Lukuvi akiitikia na
kupokea ushauri huo na kuhamishia shughuli zake mkoani Arusha ambapo kwa
sasa yuko mkoani humo akikutana na viongozi mbalimbali pamoja na
wananchi ili kutatua migogoro hiyo, Nyalandu amekaa kimya anaendelea na
mambo yake.
CCM ndiyo yenye mkataba na
wananchi kwani ndiyo iliyoomba kura kwa wananchi na Mh Waziri Nyalandu
ana mkataba na CCM ambayo imempa kazi ya ili atatue matatizo ya wananchi
si sawa, CCM haiwezi kukubali mambo yaiharibike kwa watendaji wa
serikali kutowajibika kwa wananchi kwani ndiyo itakayoadhibiwa na
wananchi, “Hivyo Nyalandu anatakiwa kufanya kazi ambayo CCM imempa na si
kutafuta watu wa kumtetea Nape” Amesema.PICHA NA KIKOSIKAZI CHA
FULLSHANGWE-MERU-ARUSHA
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Tanzania mstaafu . Jenerari Mrisho Sarakikya akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Arusha Mh. Ole Nangole katikati ni Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
Kazi
ni popote Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisaini kitabu
cha wageni kwenye gari wakati aliposalimiana na wananchi katika chuo cha
walimu Patandi mahali ambapo alisoma shule miaka ya nyuma wakati
ikiwani Middle School.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokelewa na wananchi huku
wakiwa na ndoo za maji na matawi ya miti wakati alipofika katika kijiji
cha Kimundo kata ya Nkoarisambu ambao wananchi wanachimba mawe na
kubadilishana na maji kutokana na shida ya maji. Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na askofu wa Meru
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikaribishwa na wananchi wakati alipotembelea Patandi mahali aliposoma.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokea
kati kutoka kwa Nelson Kitomari Katibu wa MC4 Change kanda ya Kaskazini
mara baada ya kukihama chama hicho na kujiunga na CCM katika kijiji cha
Sing’isi. Mwenyekiti
wa Chadema wilaya ya Monduli na Mwenyekiti wa Baraza la Wazee kata ya
akeri Meru Amani Ole Silanga akiwahutubia wananchi katika mkutano
uliofanyika kijiji cha Sing’isi.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimkabidhi kadi ya uanachama wa CCM aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema Monduli Bw. Amani Ole Silanga.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokelewa na wananchi kwa matawi ya miti mara baada ya kumpokea katika kijiji cha Sing’isi.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi wa jengo la mashine za kukoboa na kufungasha mpunga USA River Lekitatu.
Mkuu
wa wilaya ya Arumeru Bi. Husna Mwilima akizungumza na wananchi wakati
akielezea mkakati wa serikali ili kutatuo mgogoro wa ardhi katika kijiji
cha Maweni;
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi wa jengo la Maktaba ya Ardhi MKURAVITA katika kijiji cha Mawezi.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiteta jambo na diwani wa kata ya Mbuguni Thomas Mollel aka Askofu mara baada ya kukagua mradi wa maji Mbuguni kushoto ni Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongozana na wananchi wakati akielekea kwenye mkutano uliofanyika Mbuguni .
Bw. Amani Ole Silanga akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kata ya Mbuguni Meru.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akivishwa Mgorole kama ishara ya heshima ya wazee wa Meru.
Nape Nnauye akivishwa mgorole kama ishara ya heshima ya wazee wa Meru