Msanii Maarufu Rwanda Kiziti Mihigo Afungwa Miaka 10 Jela kwa Kupanga Njama njama za kupindua serikali na kuua viongozi wake

March 02, 2015

Muimbaji maarufu wa Rwanda Kizito Mihigo amehukumiwa kifungo cha miaka 10 jela baada ya kushtakiwa kwa njama za kutaka kupindua serikali na kuua viongozi wake na kuonyesha chuki dhidi ya serikali.

Kizito Mihigo awali alisema alikuwa na makosa na kuomba msamaha, akimaanisha hukumu yake ipunguzwe.

Kizito Mihigo amekuhumiwa jela miaka 10 kwa njama za kutaka kupindua serikali na kua viongozi wake.

Mshtakiwa mwenzake, Cassien Ntamuhanga kiongozi wa kituo cha redio ya Kikristo, alifungwa miaka 25 kwa ugaidi na matusi. Ameendelea kukataa mashtaka yote. 

Mihigo alikubali kutumiana ujumbe na kundi la upinzani lenye maskani Afrika Kusini, Rwanda National Congress (RNC). Alifutiwa mashtaka ya ugaidi huku Ntamuhanga alifutiwa kosa la kupanga kumuua Rais Kagame.
chanzo: http://www.newtimes.co.rw

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »