Kamishna wa Polisi Elice Mapunda
akila kiapo mbele ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu
baada ya kupandishwa cheo na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania kutoka Naibu Kamishna wa Polisi kuwa Kamishna wa Polisi.
Katikati ni Msemaji wa Jeshi hilo Mrakibu Mwandamizi wa Polisi Advera
Bulimba. Hafla hiyo fupi ilifanyinyika jana Makao Makuu ya Polisi jijini
Dar es Salaam.
(Picha na Frank Geofray-Jeshi la Polisi).
Kamishna wa Polisi Diwani Athumani
akila kiapo mbele ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Ernest Mangu
baada ya kupandishwa cheo na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania kutoka Naibu Kamishna wa Polisi kuwa Kamishna wa Polisi. Hafla
hiyo fupi ilifanyinyika jana Makao Makuu ya Polisi jijini Dar es
Salaam.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini,
IGP Ernest Mangu akimpongeza Kamishna wa Polisi Elice Mapunda mara baada
ya kula kiapo mbele yake kufuatia kupandishwa cheo na Mhe.Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Naibu Kamishna wa Polisi kuwa
Kamishna wa Polisi. Hafla hiyo fupi ilifanyinyika jana Makao Makuu ya
Polisi jijini Dar es Salaam.
…………………………………………………………………………………………………
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa
Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama mhe. Dkt
Jakaya Mrisho Kikwete, amewapandisha vyeo maafisa watatu (3) wa Jeshi la
Polisi kutoka cheo cha Naibu Kamishina wa Polisi (DCP) kuwa Kamishina
wa Polisi (CP) na maafisa wengine 14 kutoka cheo cha Kamishina Msaidizi
Mwandamizi wa Polisi (SACP) kuwa Naibu Kamishina wa Polisi (DCP).
Maofisa waliopandishwa vyeo kutoka
cheo cha Naibu Kamishina wa Polisi (DCP) kuwa Kamishina wa Polisi (CP)
ni pamoja na Kenneth Kasseke, Elice Mapunda na Diwani Athumani.
Maofisa wengine waliopandishwa
cheo kutoka Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) kuwa Naibu
Kamishina wa Polisi (DCP) ni pamoja na Godluck Mongi, Ally Lugendo,
Salum Msangi, Faustine Shilogile, Maulid Mabakila, Albert Nyamhanga,
Daniel Nyambabe, Salehe Ambika, Robert Boaz na Gabriel Semiono. Pia wamo
kamanda wa Polisi mkoa wa Simiyu Charles Mkumbo, kamanda wa Polisi mkoa
wa Mwanza Valentino Mlowola, kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Liberatus
Sabas na kamanda wa Polisi mkoa wa Ilala Maria Nzuki.
Aidha, mhe. Rais amempandisha Juma
Yusuf Msige kutoka cheo cha kamishina msaidizi wa Polisi (ACP) kuwa
kamishina msaidizi mwandamizi wa Polisi (SACP).
Kufuatia kupandishwa vyeo kwa maafisa hao wa Jeshi la Polisi, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu katika hafla fupi ya kuwaapisha makamishina hao wapya, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe. Dkt Jakaya Mrisho Kikwete kwa kutambua mchango wa Jeshi la Polisi katika kuimarisha ulinzi na usalama wa raia na mali zao.
Kufuatia kupandishwa vyeo kwa maafisa hao wa Jeshi la Polisi, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu katika hafla fupi ya kuwaapisha makamishina hao wapya, amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe. Dkt Jakaya Mrisho Kikwete kwa kutambua mchango wa Jeshi la Polisi katika kuimarisha ulinzi na usalama wa raia na mali zao.
Aidha, IGP Mangu amewapongeza
maofisa wote waliopandishwa vyeo na kuwataka kuendelea kufanya kazi kwa
bidii na weledi mkubwa ili kuwa chachu ya mabadiliko katika kuimarisha
usalama wa raia na mali zao. IGP Mangu aliongeza kuwa, cheo ni dhamana
na kuwataka kuwa mfano mzuri katika utekelezaji wa majukumu yao na
usimamizi kwa walio chini yao.
Imetolewa na:
Advera Bulimba -SSP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.
Advera Bulimba -SSP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.
EmoticonEmoticon