Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa
Dodoma Mh. Adam Kimbisa wakisoma maelezo katika moja ya vibao vilivyopo
katika mashamba darasa ya mahindi kwenye kituo cha mafunzo ya kilimo cha
kisasa kwa wakulima na wafugaji kilichopo Kibakwe wilayani Mpwapwa
mkoani Dodoma, wakati Katibu Mkuu huyo alipotembelea kituo hicho na
kukagua shughuli za maendeleo zinazofanyika kwenye kituo hicho.
Kinana yuko katika ziara ya mkoa wa Dodoma akikagua na kuhimiza
utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 na kuhimiza uhai
wa chama akiongozana na Nape Nnauye Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM
ambapo kesho ataendelea za ziara katika jimbo la Kongwa.(PICHA NA
KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-KIBAKWE)
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dodoma Mh. Adam Kimbisa wakitembelea shamba darasa hilo na kujionea mbegu mbalimbali zilizopandwa katika mashamba hayo.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa
Dodoma Mh. Adam Kimbisa, Mkuu wa mkoa wa Dodoma Kapteni Chiku Galawa
wakishiriki kupanda mti wa mnyaa kwa ajili ya uzio unaozunguka katika
kituo hicho.
Mkuu
wa mkoa wa Dodoma kapteni mstaafu Chiku Galawa akizungumza na
mwanafunzi wa darasa la kwanza katika shule ya msingi ya Ikuyu Baby Anna
John wakati Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana alipotembelea
na kukagua mradi wa ujenzi wa madarasa katika shule hiyo, Kushoto ni
Mkuu wa wilaya ya Mpwapwa Dr, Jasmine Tisekwa.
Mkuu wa mkoa wa Dodoma kapteni mstaafu Chiku Galawa akizungumza na wananchi huku Nape Nnauye akimsikiliza katika moja ya mikutano katika jimbo la Kibakwe.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi wa Marumaru katika ofisi ya mtendaji kata ya Ludi jimbo la Kibakwe.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiangalia kikundi cha ngoma kilichokuwa kikitumbuiza katika mapokezi kwenye tawi la Mtamba jimbo la Kibakwe.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza
na wananchi wa tawi la Mtamba jimbo la Kibakwe wakati alipomtembelea
balozi wa tawi hilo na kuzindua ofisi ya tawi la Mtamba, kushoto ni
Mwenyekiti wa tawi hilo Bw.Enock Ndule.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akitoka katika ofisi ya tawi la Mtamba mara baada ya kuizindua rasmi.
Katibu
wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na wananchi katika
mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa stendi Kibakwe mjini. Mwenyekiti
wa CCM mkoa wa Dodoma Mh. Adam Kimbisa akizungumza na wananchi katika
mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa stendi Kibakwe mjini.