KATIBU MKUU WA CCM NDUGU ABDULRAHMAN KINANA AMPOKEA MAKAMU WA RAIS DR. GHARIB BILAL MKOANI ARUSHA

March 28, 2015

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dr. Mohamed Gharib Bilal akiwasili kwenye uwanja wa ndege wa KIA tayari kwa kumpokea Rais wa Zimbabwe Mh. Robert Mugabe ambaye atafungua mkutano wa Vijana Viongozi wa Afrika na China unaofanyika kwenye hoteli ya Ngurudoto mkoani Arusha ukijumuisha vijana kutoka China na nchi za kiafrika. Dr. Gharib Bilal alipokelewa na katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdurlahman Kinana na viongozi mbalimbali wa mkoa wa Arusha.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-NGURUDOTO -ARUSHA)2 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dr. Mohamed Gharib Bilal akiongozana na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa KIA mkoani Arusha kwa ajili ya mkutano wa Vijana viongozi wa Afrika na China, Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Arusha Ndugu Felix Ntibenda na kutoka kushoto ni Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi, Steven Masele Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya mkutano huo na Sadifa Hamis Juma Mwenyekiti wa UVCCM Taifa. 9 
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dr. Mohamed Gharib Bilal akiongozana na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana huku wakiangalia vikundi vya ngoma mbalimbali mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa KIA mkoani Arusha.
8

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »