Mtaalam kutoka kampuni ya
kitanzania ya Derm Electric inayojenga miundombinu ya umeme katika mkoa
wa Dodoma chini ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Azizi Msuya
(kushoto) akiielezea Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini
hatua iliyofikiwa ya ujenzi wa miundombinu ya umeme katika mkoa wa
Dodoma katika eneo iliyopo bohari ya kuhifadhi vifaa vya ujenzi vya
kampuni hiyo, nje kidogo ya mji wa Dodoma. Kamati hiyo inafanya ziara
kwenye miradi ya umeme mkoani Dodoma lengo likiwa ni kujionea
utekelezwaji wake pamoja na kuzungumza na wawakilishi wa wananchi.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya
Bunge ya Nishati na Madini, Richard Ndassa (kushoto) akitoa maelekezo
kwa wataalamu wa Shirika la Umeme Nchini (Tanesco) mara kamati hiyo
ilipofanya ziara ya kukagua miradi ya umeme katika kijiji cha Msanga
kilichopo wilayani Chamwino mkoani Dodoma.
Mtaalam kutoka kampuni ya
kitanzania ya Derm Electric inayojenga miundombinu ya umeme katika mkoa
wa Dodoma chini ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Azizi Msuya (wa pili
kutoka kushoto) akielezea Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na
Madini, wataalamu kutoka Shirika la Umeme Nchini (Tanesco) na wataalamu
kutoka Wizara ya Nishati na Madini hatua iliyofikiwa katika usambazaji
wa miundombinu ya umeme katika eneo la Kibaigwa wilayani Kongwa mkoani
Dodoma. Kamati hiyo iliiagiza kampuni hiyo kuweka miundombinu ya umeme
katika vijiji vilivyosahaulika.
Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya
Bunge ya Nishati na Madini ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Chambani- Pemba,
Yusuph Salim (katikati) akitoa maelekezo kwa wataalamu kutoka Shirika
la Umeme Nchini (Tanesco) na Wizara ya Nishati na Madini (hawapo
pichani)
Meneja wa Shirika la Umeme Nchini
(Tanesco) Dodoma, Zakayo Temu ( wa pili kutoka kulia) akielezea mikakati
ya shirika hilo katika usimamizi wa miradi inayofadhiliwa na Wakala wa
Nishati Vijijini (REA) Awamu ya Pili mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge
ya Nishati na Madini, wataalamu kutoka Shirika la Umeme Nchini (Tanesco)
na wataalamu kutoka Wizara ya Nishati na Madini.
Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya
Bunge ya Nishati na Madini ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu Geita,
Josephine Chagula ( wa tatu kutoka kulia) akitoa ushauri kwa kampuni ya
kitanzania ya Derm Electric inayojenga miundombinu ya umeme katika mkoa
wa Dodoma chini ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wa namna ya
kuboresha kasi ya usambazaji wa miundombinu ya umeme katika mkoa wa
Dodoma.
Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya
Bunge ya Nishati na Madini ambaye pia ni Mbunge wa Kilwa, Murtaza
Mangungu (katikati) akilishauri Shirika la Umeme Nchini (Tanesco) namna
bora ya kuwawezesha wananchi kuunganishiwa na huduma ya umeme mara baada
ya kukamilika kwa ujenzi wa miundombinu ya umeme inayotekelezwa na
Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Awamu ya Pili.