YONDANI AREJEA YANGA, AANZA MAZOEZI KUWASUBIRI WASWANA

February 11, 2015

Beki wa Yanga, Edward Charles, ametupwa nje  katika kikosi hicho kwa siku kumi, huku mkongwe  Kelvin Yondani akirejea kuivaa BDF XI, siku ya Jumamosi katika raundi ya kwanza ya michuano ya Kombe la Shirikisho.


Charles aliumia katika mchezo wao wa hivi karibuni dhidi ya Mtibwa Sugar ambapo aliumia kifundo cha mguu, akafungwa bandeji nyepesi.

Yondani yeye aliumia kwenye mchezo kati ya timu yake na Polisi Morogoro, lakini ameshapona na yupo fiti kwa mechi hiyo.

“Wachezaji wanaendelea vizuri kama hivi, Yondani na Dilunga, wameanza mazoezi leo kwa ajili ya mchezo wa Jumamosi baada ya afya zao kuimarika lakini Edward yeye ataendelea kuwa nje kwa siku kumi mpaka pale afya yake itakapoimarika.

“Upande wa beki Nadir Haroub ‘Cannavaro’, yeye leo (jana Jumanne), hajafanya mazoezi lakini kesho (leo) ndiyo ataanza rasmi na timu kama kawaida, kwa sababu alipata maumivu kidogo katika mchezo wetu dhidi ya Mtibwa Sugar na sasa yupo vizuri,” alisema Daktari wa Yanga, Sufiani Juma.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »