WAZEE WA NGWASUMA KUWASHA MOTO LEO JIJINI TANGA

February 12, 2015
BENDI ya mziki wa Dansi nchini ya FM Academia “Wazee wa Ngwasuma”wanatarajiwa kuwagawisha wakazi wa Jiji la Tanga katika onyesho lao la wakati wa siku ya wapendanao Valentine day litakalofanyika February 12 leo.

Onyesho hilo linatarajiwa kufanyika kwenye ukumbi wa Tanga Hotel ambalo litakuwa na zawadi mbalimbali ya CD ya chuki ya nini kwa mashabiki wote watakaoweza kuingia kushuhudia burudani hiyo.

Mratibu wa Onyesho hilo,Kelvin Msinga alisema kuwa maandalizi ya onyesho hilo yanaendelea vizuri na wasanii wanaounda bendi hiyo wapo tayari kuweza kuwapa burudani ya aina yake wakazi wa jiji la Tanga na vitongoji vyake.

Msinga alisema kuwa katika onyesho hilo wakazi wa Tanga watapata fursa ya kusikiliza nyimbo zao kali kama “Chuki ya Nini”,Fataki,Otilia,Ndoa ya Kisasi,Daily Chako Ulaumiwe,Maisha,Neema na Madudu

Hata hivyo aliwataka wapenzi wao kuhakikisha wanajitokeza kwa wingi ili kuweza kushuhudia burudani iliyokuwa na ubora wa aina yake ambayo itakuwa ikitolewa na wasanii hao.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »