MH. MAKALLA AZINDUA MRADI WA MAJI HANANG

February 11, 2015

Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla, Mkuu wa Wilaya ya Hanang, Christina Mndeme na Inj. Salum Chusi wa Wizara ya Maji (nyuma) wakiangalia pampu ya maji ya mradi wa Simbay katika ziara yake ya kukagua utekelezaji na uzinduzi wa miradi ya maji mkoani Manyara jana.
Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla akiwa kwenye tanki la maji la mradi wa maji wa Simbay, wilaya ya Hanang mkoani Manyara.
Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla akizindua rasmi mradi wa maji wa kijiji cha Simbay, Wilaya ya Hanang, mkoani Manyara katika ziara yake aliyoanza mkoa wa Manyara jana, akiwa pamoja na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Mahusiano na Uratibu na Mbunge wa Hanang, Dk. Mary Nagu na Mkuu wa Wilaya ya Hanang, Christina Mndeme.
Mradi wa maji wa Simbay mara baada ya kuzinduliwa rasmi na Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla.
Mwenyeji wa Kijiji cha Simbay akisoma ripoti ya maji ya kijiji cha Simbay, wilaya ya Hanang, mkoani Manyara kwa Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla kati.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »