Kilichoamriwa na Halmashauri ya Manispaa ILALA kuhusu jengo la ghorofa 15 na watu wanaoishi JANGWANI DAR

February 09, 2015

Kettenbagger_CAT_325C_LN
Kuanguka kwa majengo marefu katikati ya Jiji la Dar es Salaam na sehemu nyingine Tanzania ni moja ya vituambavyovimetajwa kuhatarisha maisha ya watu, kitu ambacho kimesababishwa kuibuka maswali mengi kwamba wenye mamlaka wanakuwa wapi wakati ujenzi wa aina hii ukiwa unafanyika?
Kamati ya Ardhi na Mipango Miji ya Manispaa ya Ilala imefanya maamuzi ya kuvunjwa kwa jingo al ghorofa 15 lililojengwa katikati ya Jiji baada ya kubainika kuwa lilijengwa chini ya kiwango.
Mhandisi wa Manispaa hiyo Bwigane Jafary amesema amri ya Mahakama pia imeagiza kuvunjwa nyumba zote zilizoko mabondeni bila kulipwa fidia baada ya wananchi kushindwa kesi.
“Uvunjaji wa majengo marefu si wasa na uvunjaji wa majengo ya kawaida… jingo lile limebanwa na majengo mengine.. njia pekee ambayo tunatakiwa tuitumie pale ni kutumia excavator yenye mikono mirefu…”—Bwigane Jafary.
Kwa wakazi wale wa jangwani ambao walikuwa wamefungua kesi Mahakamani kuipinga Halmashauri ile kesi imekwenda ba hatimaye wale wakazi wameshindwa…” aliongea Bwigane Jafary kuhusu ishu ya wakazi wa Jangwani, Dar.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »