JAMII YATAKIWA KUTOA KIPAUMBELE KWA VIJANA WAKATI WA MIPANGILIO YA BAJETI ZAO

February 08, 2015

2
Mke wa Rais wa Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani Bibi. Daniela Schadt (mwenye nguo nyekundu) akisalimiana na Mkurugenzi wa DSW Tanzania Bw. Peter Owaga mara baada ya kuwasili katika ofisi za Shirika hilo zilizopo Tengeru jijini Arusha alipoenda kuzindua mradi wa BEYOND 2015 hivi karibuni.
3
Mke wa Rais wa Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani Bibi. Daniela Schadt (mwenye nguo nyekundu) akisikiliza maelezo mafupi kuhusu Shirika lisilo la Kiserikali la DSW Tanzania kutoka kwa Mkurugenzi wa shirika hilo Bw. Peter Owaga mara baada ya kuwasili katika ofisi za Shirika hilo zilizopo Tengeru Munasa jijini Arusha juzi.Wa mwisho kushoto ni Mkuwa Wialaya ya Arumeru Mhe. Nyirembe Munasa.
4
Mkurugenzi wa DSW Tanzania Bw. Peter Owaga akizungumza jambo wakati wa hafla ya uzinduzi wa mradi wa BEYOND 2015 juzi jijini Arusha. Kutoka kushoto ni Mke wa Rais wa Shirikisho wa Jamii Dkt. Elizabeth Mapella. BEYOND 2015 ni mradi uliolenga kuongeza hamasa na ushawishi kwa wadau wa maendeleo kutoa kipaumbele kwa vijana husasni katika Elimu, Afya ya uzazi na Ajira.la Ujerumani Bibi. Daniela Schadt, Mke wa Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania Bibi. Wenday Marshall – Kochanke na Mratibu wa Programu za Vijana kutoka Wizara ya Afya, na Ustawi.
5
Baadhi ya washiriki wa hafla ya uzinduzi wa mradi wa BEYOND 2015 wakimsikiliza Mkurugenzi wa DSW Tanzania Bw. Peter Owaga (hayupo pichani).
7
Mke wa Rais wa Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani Bibi. Daniela Schadt akifuarahi mara baada ya kukata utepe na kuzindua rasmi mradi wa BEYOND 2015, juzi jijini Arusha.Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa DSW Tanzania ambao ndiyo watekelezaji wa mradi huu Bw. Peter Owaga. Wengine ni Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Nyirembe Munasa (nyuma ya Mke wa Rais wa Ujerumani) na Mratibu wa Mradi huo Bi. Ester Mwanjesa aliyeshika kitabu.
8
Mke wa Rais wa Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani Bibi. Daniela Schadt akiteta jambo na Mkurugenzia wa DSW Tanzania(katikati) pamoja na Mratibu wa Mradi wa BEYOND 2015 Bi. Esther Mwanjesa mara baada ya kuzindua mradi huo juzi jijini Arusha
9
Mke wa Rais wa Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani Bibi. Daniela Schadt akipokea zawadi ya Kimasai kutoka kwa Mwanamke mjasiriamali Bibi.Salome Samwel wakati alipotembelea maonyesho ya biaadha zao katika hafla ya uzinduzi wa mradi wa mradi wa BEYOND 2015, juzi jijini Arusha.1
Picha ya pamoja
…………………………………………………………………………
Na Mwandishi Wetu, Arusha
Mke wa Rais wa Shirikisho la Jamhuri ya Ujerumani Bibi. Daniella Schadt ametoa wito kwa jamii kuhakiksha wanatoa kipaumbele katika kushirikisha vijana kwenye nyanja mbalimbali za maendeleo. Wito huo umetolewa juzi jijini Arusha wakati Mke huyo wa Rais wa Ujerumani alipokuwa akizindua mradi wa utetezi na ushawishi wa jamii katika kutoa vipaumbele katika sekta za Elimu, Afya na Ajira kwa vijana ujulikanao kama BEYOND 2015 ambapo mradi huo unaratibiwa na Shirika lisilo la Kiserikali la DSW Tanzania. Bibi. Daniela alisema kuwa jamii inapaswa kutoa mkazo katika sekta za Elimu, Afya na Ajira kwa vijana kwa kuwa duniani kote vijana ndiyo nguvu kazi katika kuletea maendeleo ya taifa lolote lile. ‘Tunapaswa kuweka mkazo kwa vijana wadogo, maisha yao ya baadaye yanaanza kuanzia sasa, tuweke mkazo katika Elimu na Afya kwa vijana wetu ili waeze kutambua fursa na kuzitumia.’’ Alisema Bibi. Daniela. Kwa upande wake Mkurugenzi wa DSW Tanzania Bwana Peter Owaga amesema kuwa ni wao kama asasi ya kirai wanashirikia na Serikali katika kuhakikisha utekelezaji wa sera zinazohusu vijana nchini zinaleta tija Owaga ameongeza kuwa Serikali kama msimamizi imepiga hatu kubwa kwa kuwa na Sera na miongozo mbalimbali inayohusu vijana kama vile Sera ya Maendeleo ya Vijana ya mwaka 2007 inayotoa fursa kwa kijana kujitambua. Aidha Owaga aliongeza kuwa mradi wa BEYOND 2015 ambao umezinduliwa na Mke wa Rais wa UjerumaniBibi. Daniela Schadt umelenga kuongeza ushawishi na hamasa kwa washirika wa maendeleo ili kutoka kipaumbele kwa kutenga bajeti kwa ajili ya Elimu , Afya ya Uzazi na Ajira kwa vijana. Akizungumzia mikakati na namna mradi huo utakavyotekelezwa Afisa Muhamasishaji na Mawasiliano Bi. Ester Mwanjesa amesema kuwa mradi huo utatekelezwa kwa mwaka mmoja katika mikoa yote nchini ambapo mijadala mbalimbali itakuwa ikifanyika ili kuongeza hamasa ya uashawishi utakaopelekea kutoa kipaumbele kwa vijana hususan katika nyanja za Elimu, Afya ya uzazi na Ajira. Mradi huu wa BEYOND 2015 ambao ni kifupi cha maneno Building Expert Youth and Organisation for National Postion on the Post 2015 Development umelenga kutatua changamoto za vijana asa baada ya kumalizika kwa muda wa Malengo ya Melenia mapema mwaka huu.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »